Monday 17 November 2014

JE, KUNA UHUSIANO WOWOTE KATI YA TUMBO KUJAA GESI NA MIUNGURUMO KWA MWANAUME KATIKA TENDO LA NDOA?


Watu wengi wamekuwa wakiwasiliana nasi wakihusisha haya mambo mawili hasa wanaume pasipo kujua kama yanahusiana kwa ukaribu au laa.
Na kwa maana hiyo, leo watu wengi wataweza kujua uhusiano wa haya mambo mawili yaani miungurumo ya tumbo, tumbo kujaa gesi na miungurumo ya hapa na pale katika kushiriki tendo la ndoa au kupungukiwa na nguvu katika kushiriki tendo la ndoa.
Tatizo hili kitaalamu huitwa constipation, yaani mtu kuwa na tatizo la kupata choo kidogo, au kutokupata kabisa, na hii huwatokea watu mbalimbali pasipo kujua vyanzo ni nini, lakini hapa utaweza kujua vyanzo vyake na jinsi gani utajiepusha. Tutaanza na dalili zake.
DALILI ZA CONSTIPATION
Dalili za constipation ni kama zifuatazo;
Ni ile hali ya mwanamke au mwanaume anapokuwa anakula chakula kila siku lakini anakuwa hapati choo, wataalamu wanasema kila chakula kinapoingia basi kuna chakula kingine kinatakiwa kitoke, lakini mtu unapokula kila siku na haupati choo kwa siku mbili au tatu au wiki moja basi ujue kwamba unaandamwa na tatizo hilo.
Ni pale mtu anapopata choo kigumu sana kupita kiasi, na wakati mwingine choo hicho kinaambatana na maumivu makali sana kupita kiasi na wengine wanakuwa wanachanika katika njia ya haja kubwa na pale wanapopatwa na choo  au kusikia haja wanakuwa wanaona kama muda wa mateso umekaribia au umefika na choo chao mara nyingi kinakuwa kinaambatana na damu.
Kukumbwa na uchovu kupita kiasi, hii hutokea sana kwa baaadhi ya watu ambao hukumbwa sana na tatizo hili la kupata choo kigumu kupita kiasi na kupatwa na maumivu makali pia (constipation), na hivyo kupatwa na uchovu sana na wanakuwa kama wamefanya kazi kubwa sana lakini si hivyo basi hii nayo ni dalili kubwa sana ya constipation.
Pia kuna hali ya mtu kuandamwa na homa za hapa na pale, na mara nyingi mtu anashindwa kufanya kazi zake kama kawaida, hii nayo ni dalili kubwa sana ya constipation.
Pia kuna ile hali ya mtu kutokujisikia kufanya kitu chochote, yaani kulala inakuwa ni ngumu kwake, kukaa anapata tabu sana, akienda kwenye kazi zake anakuwa mzito sana, yaani hata kutoka kwenda kufanya ibada nayo inakuwa ni ngumu,  wakati huohuo anaandamwa na kukosa choo kwa muda mrefu nayo ni dalili kubwa sana ya tatizo hili (constipation).
Dalili nyingine kubwa inakuwa ni maumivu chini ya kitovu, na hii huwatokea sana wanaume na vilevile hata wanawake nao huandamwa sana na dalili kama hii, pia kama unakuwa unapatwa na dalili kama hii na wakati huohuo unakuwa hupati choo basi kuna uwezekano mkubwa sana ukawa na tatizo hili la constipation.
Na dalili nyingine kubwa ambayo huwatokea sana wanaume ni ile kali ya kukosa hamu kabisa ya kushiriki tendo la ndoa na hata akishiriki basi inakuwa ni mara moja tu na anashindwa kuendelea kabisa.

0 comments:

Post a Comment