Showing posts with label MARADHI YA MDOMO. Show all posts
Showing posts with label MARADHI YA MDOMO. Show all posts

Sunday, 8 March 2015

MAGONJWA YA UTANDO MWEUPE KINYWANI



ziko sababu nyingi zinazoweza kusababisha hali hii ya kutokea kwenye kinywa, lakini chanzo chake kikubwa ni maradhi yanayosababishwa na fangasi.

Maradhi ya fangasi ya kinywa huweza kuathiri koo pia. Vijidudu vinavyoathiri hujulikana kama oral candidiasis na wale wanaoshambulia koo huitwa oesophageal candidiasis.

Utando wa kinywa ni maradhi ni maradhi yanayosababishwa na vimelea vya fangasi aina ya hamira ambao hushambulia eneo la ndani ya kinywa na koo.
Kwa kawaida kinga ya mwili pamoja na vimelea vinavyokaa mwilini vya aina ya bacteria huzuia fangasi hawa wasiongezeke.

Inapotokea uwiano huu wa kinga ya mwili na vimelea aina ya bacteria kushindwa kuzuia ongezeko la vimelea hivyo vya fangasi ndipo hali huwa mbaya na kusababisha utando mdomoni.

Maradhi haya ni kawaida kuonekana kwa watoto wachanga. Maradhi haya hutokea kutokana na hali ya kutokuwa na uwiano sahihi kati ya kinga ya mwili wa mtoto na vimelea aina ya bacteria.

Inapotokea yakatokea kwa mtu mzima, basi mara nyingi huwa kuna viashiria hatarishi kama vile upungufu wa kinga.

Mfano ni watu wenye maradhi ya muda mrefu kama saratani, kisukari na ukimwi au mwanamke wajawazito, hali hiyo hushusha kinga zao.

Tatizo hili huwapata pia watu wanaotumia dawa kwa muda mrefu hususani dawa za vijiuasumu (antibiotic) au za maradhi yanayotibiwa kwa muda mrefu kama vile saratani.
Kinachoweza kusababisha hali hiyo pia ni msongo wa mawazo wa muda mrefu.

Maradhi haya kwa kawaida siyo ya kuambukiza ingawa mtoto mchanga mwenye maradhi haya huweza kuyaambukiza matiti ya mama yake.

Dalili ni utando mweupe ambao huonekana kwenye kinywa eneo la ulimi na mashavuni kwa ndani. Kwenye koo huonekana kwenye kuta zake.

Mara nyingi eneo lenye rangi nyeupe huzungukwa na eneo lenye rangi nyekundu na lililovimba kidogo. Hii hutokana na mashambulizi ya fangasi.
Maeneo haya yaliyoshambuliwa huwa hayana maumivu makali lakini huweza kutoa damu kama yakiguswa au kusuguliwa.

Dalili nyingine za maradhi ni pamoja na kuonekana kwa sehemu ndogo zenye rangi nyeupe ndani ya kinywa, kupasuka kwa midomo, midomo kuongezeka ukubwa, hisia za kukwama kwa chakula kwenye koo, kuvimba kwa fizi, ladha ya chakula kubadilika na pumzi yenye kutoa harufu.

Kwa watu ambao kinga kinga ya mwili imeshuka, maradhi haya huweza kusambaa kutoka kwenye kinywa na kushuka kwenye koo la chakula mpaka kufikia kwenye tumbo.

Hii inapotokea, mgonjwa hupata maumivu wakati wa kumeza chakula.
Dalili za hatari ni mgonjwa kupata homa kali ikiambataan na kutetemeka mwili na kushindwa kabisa kumeza chakula.

Mgonjwa akifikishwa hospitali maradhi haya hutambulika kirahisi kutokana na dalili zake kuweza kutambukiwa kwa kuangalia kwa macho.

Matibabu ya maradhi haya hutegemea na kilichosababishwa. Iwapo kilichosababisha kinaweza kuepukwa au kutibika, basi nayo yataisha, kama mtu ameyapata kutokana na kuugua kisukari, ni vyema akakitubu kisukari kwanza.

Watoto wachanga hawahitaji matibabu ya aina yeyote kama dalili zitaanza kuisha kabla ya wiki nne hazijaisha.



Tiba Mbadala Ya Fangasi Kwenye Ulimi tumia Dawa Hii Hapa:

Kula Kitunguu Saumu kibichi kutwa mara 3 kwa muda wa siku 7 utapona , Pendelea kunywa Mtindi pia utasaidia hayo matatizo ya Fangasi ya mdomo. Tafuta Mafuta yanayoitwa Oregano Oil uwe unatia kwenye glasi ya maji kijiko kidogo au kijiko cha kulia wali unakunywa kutwa mara 3 kwa muda wa siku 3 utapona inshallah hiyo Fangasi kwenye ulimi.

Tuesday, 6 January 2015

KUTOKWA NA VIDONDA MDOMONI NA MATIBABU YAKE








Vidonda mdomoni husababisha sana maumivu makali pamoja na kumfanya mtu asiweze kuongea vizuri na watu.Vidonda hivi husababishwa na kutafuta kwa muda mrefu hasa bigijii au kitu chochote, uvutaji wa sigara,maambukizi ya virusi, bakteria na fungasi sambamba na ukosefu wa madini na virutubisho vya folic, zinc, vitamin c,vitamin B12, na madini ya chuma. 


Vidonda hivi huwaathiri sana watu wengi na hutokea sana kwenye lips, ulimi , mashavu, kingo na kuta za meno ambapo pia huweza kusambaa hadi kwenye koromeo endapo havitatibiwa mapema.




Pamoja na kutembelea hospitali ambapo dawa kama za antibiotiki, fangasi, virusi na zile za kupunguza maumivu na uvimbe huweza kutolewa kulingana na ukubwa wa tatzo pia unaweza kufanya yafuatayo kujitibu nyumbani

  • Epuka vyakula na vinywaji vya moto au baridi sana kwani huchelewesha kupona kwa vidonda
  • Kunywa juice ya matunda mbali mbali itakayokuwezesha kupata virutubisho na madini ambayo huongeza kinga ya mwili
  • Kunywa maji mengi kila siku ambayo sio ya moto wala baridi
  • Piga mswaki mara kwa mara na taratibu ili kuepuka kukwangua na kutonesha sehemu zenye vidonda
  • Kula sana matunda asa machungwa, machenza na malimao kwani yana kiasi kikubwa cha vitamin ambayo huongeza kinga ya mwili. Pia yana asidi ambayo inaweza kuua wadudu wanaokuwepo mdomoni
  • Unaweza kununua pia Maltivitamini dawa yenye mchanganyiko wa virutubisho vingi ambavyo huweza kusaidia kurudisha kinga ya mwili katika hali ya kawaida
  • Kama vidonda vinaambatana na maumivu makali tumia dawa ya kutuliza maumivu au kuweka barafu ambayo hupunguza maumivu kwa muda
  • Tumia Asali ambayo husaidi kuua vimelea, kuponya makovu na kulainisha sehemu zenye vidonda
  • Kunywa maji ya nazi(madafu) ambayo upoza mwili na huua wadudu hatari mdomoni sambamba na kupaka mafuta ya nazi kwenye kidonda ili kupona haraka.

Kumbuka vidonda visivyopona kwa muda zaidi ya wiki mbili vinaweza kuashiria tatizo kubwa na sugu mwilini hivyo inakupasa kufika hospitali ambapo utapewa dawa za bakteria, fungasi, virusi au dawa nyingine zozote kulinga na ukubwa na visababishi vya tatizo.

Friday, 14 November 2014

HOME REMEDIES FOR DRY MOUTH

Dry mouth, medically known as xerostomia, is a very common problem faced by many. Dryness in the mouth can be due to a change in the composition of saliva or reduced salivary flow.
It is often a symptom of the salivary glands not working properly as is often associated with aging, dehydration, stress, anxiety, snoring, depression, smoking or drinking alcohol. Pregnant or breastfeeding mothers may also experience dry mouth due to dehydration and hormonal changes.
Dry mouth can also be a side effect of certain medications used to treat depression, nerve pain (neuropathy) and anxiety, as well as some antihistamines, decongestants, muscle relaxants and pain medications. Other possible causes include chemotherapy, radiation therapy, diabetes, nerve damage and autoimmune diseases.

Some of the symptoms of dry mouth include a parched feeling in the mouth, thick or stringy saliva, a rough tongue, excessive thirst, mouth sores, bad breath, loss of taste, cracked lips and difficulty chewing, speaking or swallowing.
Dry mouth can be very irritating, particularly due to the sticky feeling in the mouth. People sometimes refer to this as having “cotton mouth”. This problem can be easily treated with simple lifestyle changes and home remedies. Make sure to follow the remedies daily until the symptoms disappear.

Here are the top 10 home remedies for dry mouth.

1. Increase Fluid Intake

Dehydration is one of the most common reasons behind dry mouth. So, the best thing you can do is increase your fluid intake to keep your body hydrated. Proper hydration will make it easier for your body to produce more saliva and help get rid of the symptoms of dry mouth.
  • Consume an ample amount of water throughout the day. If you cannot drink water, suck on small pieces of ice.
  • Eat partly frozen chunks of water-based fruits and vegetables like pineapple, watermelon and cucumber.
  • Drink smoothies, fruit juice or vegetable juice.
  • Drink 1 to 2 glasses of coconut water daily.
  • Drink herbal teas like green tea, chamomile tea, or others.
  • Eat soft and liquid foods like stews and soups.
Avoid caffeinated beverages, sodas and alcoholic drinks as they can contribute to dehydration.

2. Cayenne Pepper

Cayenne pepper stimulates saliva production, making it one of the best remedies for dry mouth. Also, it will help bolster the taste buds so you can better distinguish sour, sweet, salty and bitter flavors.
  • Press a little bit of ground cayenne pepper on a wet finger, then rub it around your tongue. This may cause a burning sensation for some time, but it will stimulate your salivary glands.
  • Also, sprinkle cayenne pepper powder in your soups, salads and other dishes.
  • Alternatively, you can take cayenne pepper capsules after consulting your doctor.

3. Fennel Seeds

The flavonoids in fennel seeds stimulate the flow of saliva and hence help get rid of dry mouth. Plus, their aromatic flavor helps combat bad breath that accompanies dry mouth.
  • Munch on fennel seeds several times a day to treat dry mouth.
  • You can also mix together equal amounts of fennel seeds and fenugreek seeds. Dry roast them in a pan, grind them thoroughly and add a little salt. Eat 1/2 teaspoon of this mixture after each meal.

4. Slippery Elm

Slippery elm contains mucilage. Due to this substance, it becomes a slick gel when mixed with water. This gel helps coat and soothe the mouth as well as the throat. Plus, it can effectively relieve many discomforts associated with dry mouth.
  • Add 1 to 2 tablespoons of slippery elm to a cup of hot water. Cover and allow it to steep for 10 minutes. Strain, add honey and drink this tea twice daily.
  • Another option is to prepare a paste with some slippery elm bark powder and enough water. Apply it inside the mouth, leave it on for a few minutes and then rinse your mouth with water. Do this once or twice daily.

5. Oil Pulling

Oil pulling, an ancient Ayurvedic practice, helps keep your mouth moist and thus is very helpful in treating dry mouth. It is also beneficial in maintaining oral health and eliminating bad breath. Oil pulling can be done with coconut oil, sesame oil or any other edible vegetable oil.
  1. Put 1 tablespoon of extra-virgin coconut oil in your mouth.
  2. Swish the oil around your mouth thoroughly for about 15 minutes.
  3. Spit it out and rinse your mouth with warm water.
  4. Brush your teeth as usual.
  5. Repeat the process daily, in the morning before eating anything.
Note: Do not gargle or swallow the oil.

6. Aloe Vera

An age-old remedy to treat dry mouth is aloe vera. It also helps protect the sensitive tissue in the mouth and enhances the taste buds.
  • Drink ¼ cup of aloe vera juice daily to cure dry mouth.
  • You can also rinse your mouth with aloe vera juice a few times a day.
  • Alternatively, apply pure aloe vera gel around your mouth using a cotton swab. Leave it on for several minutes and then rinse your mouth with cold water. Do this 2 or 3 times a day.

7. Grapeseed Oil

grapeseed oil
Grapeseed oil is another effective remedy to eliminate symptoms of dry mouth. Its moisturizing property helps coat your mouth and keeps it moist for a reasonable amount of time. Plus, being high in vitamin E, it will help heal any sores you may have in your mouth.
  1. Use your fingers to rub some grapeseed oil on your tongue and the inside of your cheeks.
  2. Leave it on overnight.
  3. The next morning, rinse your mouth with warm water and then brush your teeth as usual.
  4. Repeat daily before going to bed.

8. Lemon

lemon

Lemon juice can stimulate saliva production and relieve dry mouth. Plus, its acidic nature can help cleanse your mouth and eliminate bad breath.
  • Add the juice of half a lemon and a little honey to a glass of water. Sip this water throughout the day to stay hydrated.
  • You can also drink homemade lemonade to treat dry mouth. Be sure to use lemonade that does not contain sugar.
  • Also, sprinkle a little salt on a small piece of lemon. Rub it on your tongue to enhance your taste buds.

9. Cardamom

cardamom
An Ayurvedic remedy to fight dry mouth is cardamom. Chewing a pod of cardamom will moisten the mouth as well as eliminate bad breath.
  • Chew a pod of cardamom thoroughly after every meal or whenever your mouth is dry.
  • Alternatively, add 1 teaspoon of cardamom powder to a glass of hot water. Let it steep for 10 minutes and then drink it. Do this once or twice daily.
  • You can also rinse your mouth with lukewarm cardamom tea twice daily.

10. Ginger

ginger slices

You can also use ginger to treat dry mouth. Ginger seems to be very effective in stimulating saliva and can make your mouth feel fresh longer.
  • Chew a small piece of fresh ginger slowly. Do this several times a day to fight dry mouth symptoms.
  • You can also drink 2 to 3 cups of ginger tea mixed with honey daily to stimulate your salivary glands.
Additional Tips
  • Avoid smoking and chewing tobacco as it hampers saliva production.
  • Suck on sugar-free candies or chew sugar-free gum to promote saliva production.
  • Sleep in a room with a humidifier or vaporizer to keep your mouth moist all night long.
  • Breathe through your nose, not your mouth.
  • If you have an option then avoid taking medicines like diuretics, antihistamines and decongestants that can cause a dry mouth.
  • Gargle with warm salt water 3 or 4 times a day.
  • Occasionally inhale steam to help moisturize your nasal passages and airways.
  • In addition to brushing and flossing your teeth, clean your tongue daily. Use toothpaste and mouth rinse with fluoride in it.
  • Drink water while eating and chew your food thoroughly before swallowing. After eating a meal, rinse your mouth with warm water.
  • Lower your intake of spicy and acidic foods as they can irritate the inside of the mouth. Also, cut down on sugary foods and beverages as they may increase the risk of tooth decay.
  • Munch on snacks that have high water content like celery sticks to stimulate the saliva glands and add moisture to your mouth.

Monday, 3 November 2014

JINSI YA KUJIKINGA NA KUONDOA HARUFU MBAYA MDOMONI!


WATU wengi husumbuliwa na tatizo la kunuka mdomo bila hata kujijua hivyo kuwa kero kwa wenzao na wakati mwingine hujishushia hadhi mbele ya jamii. Mara nyingi ugonjwa wa kunuka mdomo (Halitosis) husababishwa na uchafu wa kinywa na ulaji wa vyakula usiosahihi lakini ni tatizo linalotibika.
Ni rahisi kulizuia na kuliondoa tatizo la kunuka mdomo iwapo utaamua kufuata kanuni za usafi wa kinywa na unywaji wa maji kwa kufuata kwa makini muongozo ufuatao:
KUPIGA MSWAKI
Kitu cha kwanza kufanya ni kupiga mswaki kwa ukamilifu kila uamkapo asubuhi. Wakati wa kupiga mswaki, utatakiwa siyo tu kusugua meno, bali pia ulimi, sehemu ya katikati hadi karibu na koromeo kwa kusugua vizuri.
Vile vile kila uamkapo baada ya kulala mchana au jioni, hakikisha unapiga mswaki, kwani bakteria wa kinywani, hutawala kinywa kila ulalapo. Mara baada ya kupiga mswaki na kusugua ulimi sawaswa, hakikisha unasukutua vizuri kwa maji, kwani hapa ndipo baadhi ya watu hukosea kwa kupiga mswaki bila kusukutua kwa maji.
KUNYWA MAJI MENGI
Maji ni muhimu sana karibu kila eneo la mwili wa binadamu. Unywaji wa maji ya kutosha kila siku utakusaidia kudhibiti na hatimaye kuondoa tatizo la kunuka mdomo. Unywaji wa maji mengi ni muhimu, hasa kwa wale watu wenye ugonjwa wa kukauka midomo (xerostomia).
Mara nyingi harufu itokayo mdomoni, hutokea tumboni na siyo kinywaji peke yake kama unavyoweza kudhani. Hivyo, kama tumbo litakuwa chafu, hata kama utasafisha kinywa vizuri bado harufu mbaya inaweza kuendelea kutoka.
Harufu mbaya ya tumboni hutokea pale tumbo linapokuwa chafu kutokana na kutopata choo kwa muda mrefu. Miongoni mwa mambo yanayochangia kukosekana kwa choo kwa muda mrefu ni pamoja na tabia ya kutokunywa maji ya kutosha kwa siku, hivyo hakikisha unakunywa maji, kiasi kisichopungua 

lita moja na nusu hadi mbili au zaidi, kutegemeana na kazi unazozifanya.
Ukiwa na tatizo la kukaukiwa maji mwilini kila mara, mwili hujaribu kutumia njia zake za kiasili kupunguza uzalishaji wa mate ili kuhifadhi maji kwa ajiili ya matumizi mengine, kitendo hicho huchangia kunukisha mdomo kwa sababu ndani ya mate huwa kuna kinga muhimu dhidi ya baktetria wanaonukisha kinywa.
Kwa upande mwingine, ili kuzuia kinywa kunuka pale mdomo unapokuwa umekaukiwa na mate, ni vizuri kutafuna vitu kama bazooka au ‘chewing gum‘ yoyote ili kuzalisha mate ambayo huhitajika katika kudhibiti bakteria.
Mwisho, hakikisha unasukutua sawaswa baada ya kula chakula chochote, hata kama ni juisi isipokuwa unapokunywa maji tu ya kawaida. Bila shaka, ukizingatia haya, tatizo ulilonalo la kunuka mdomo litataoweka na kubaki historia.

Thursday, 9 October 2014

JUA UGONJWA WA GOITA,DALILI PAMOJA NA TIBA YAKE




Baada ya somo mwanafunzi ajue mambo yafuatayo:-
1. Maana ya upungufu wa madini joto mwilini
2. Dalili za upungufu wa madini joto mwilini
3. Sababu za kupata upungufu wa madini joto mwilini
4. Jinsi ya kuzuia upungufu wa madini joto mwilini na
5. Matibabu ya upungufu wa madini joto mwilini.
1. Maana ya upungufu wa madini joto mwilini.



Huu ni uvimbe usio wa kawaida katika kikoromeo(Thyroid Gland) ambao hutokea mbele ya shingo)



2. Dalili za upungufu wa madini joto mwilini (Goita)
i. Uvimbe mbele ya shingo
ii. Mama wajawazito kuharibu mimba
iii. Kudumaa mwili na akili
iv. Mtoto kufia tumboni
v. Kuzaliwa mtoto njiti (uzito pungufu au premature)
vi. Kutetemeka na kuwa na wasiwasi.
vii. Macho kutoka nje



3. Sababu za kupata upungufu wa madini joto mwilini.
i. Kupungua kwa IODINE katika chakula
ii. Lishe duni
4. Jinsi ya kuzuia upungufu wa madini joto mwilini
i. Kutumia chumvi yenye Iodine (ayodini) hasa ile ya baharini
ii. Kutumia vyakula vyenye Iodine(ayodini) kwa wingi kama vile dagaa, maziwa nk.
iii. Kutoa elimu ya afya kwa jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora na
iv. Kumpeleka mgonjwa hospitali iwapo ameshaanza dalili



5. Matibabu ya upungufu wa madini joto mwilini
i. Mgonjwa ataagiziwa dawa ya Iodine na daktari
ii. Tumia dawa kama utakavyoagizwa na

iii. Operesheni itakayofanyika kama tezi imekuwa kubwa na athari zake zimeonekana 

Tuesday, 30 September 2014

USAFI WA KINYWA NA UTUNZAJI WA MENO





leo tutazungumzia usafi wa kinywa na umuhumu wake na jinsi utunzaji wa sehemu hiyo ya mwili unavyoathiri afya ya mtu kwa ujumla. Karibuni.

Afya ya kinywa ina umuhimu mkubwa zaidi ya unavyoweza kufikiria na kwa ujumla inaweza kutoa ufahamu kuhusiana na jinsi afya yako ya mwili ilivyo. Kuelezewa uhusiano uliopo kati ya afya ya kinywa na afya ya mwili mzima kunasaidia kufahamu umuhimu wa kutunza kinywa na hasa meno na fizi. Kama zilizo sehemu nyingine za mwili, kinywa nacho kimejaa bakteria ambao wengi wao hawana madhara. Kwa kawaida mfumo wa kulinda mwili na utunzaji mzuri wa kinywa kama vile kupiga mswaki na kutumia uzi kuondoa uchafu katika meno kunaweza kudhibiti bakteria walioko kinywani wabakie katika hali ya kawaida na kutodhuru kinywa. Lakini bila kutunza vyema kinywa, bakteria hao wanaweza kusababisha maambukizo na kusababisha meno kuoza na maradhi ya fizi.

Afya ya kinywa inajumuisha siha na namna ya utunzaji wa sehemu zote za mdomo hasa meno na fizi. Mbali na kinywa kutuwezesha ipasavyo kula, kuzungumza na hata kuwa na muonekano mzuri wa uso, meno na fizi zinapaswa zisiwe zimedhurika na kuwa na matatizo kama vile meno kuoza, magonjwa ya fizi, kung'oka meno na mdomo kunuka. Kuoza meno na meno kuwa na matundu ni matatizo ya kinywa yanayoshuhudiwa sana miongoni mwa watu. Sababu zinazoweza kuzuia matatizo hayo ya meno ni kudumisha usafi wa kinywa, kupata fluoride ya kutosha na kutokula kwa wingi vyakula vinavyoweza kudhuru meno na kusababisha matundu.


Afya ya meno na kinywa kwa ujumla inahusiana na afya ya mwili mzima kwa njia tofauti. Kwanza kabisa uwezo wa kutafuna chakula na kukimeza ni muhimu ili mwili uweze kupata virutubisho muhimu vya kujenga mwili. Halikahalika kuwa na kinywa chenye matatizo kunaweza kuathiri namna mtu anavyozungumza na hata kujiamini kwake. Matatizo ya meno yanaweza kumsababishia mtu gharama kubwa ya matibabu na ukarabati wa meno.


Sababu zinazoweza kuathiri afya ya kinywa

Uimara wa meno na fizi unatofautiana kati ya mtu na mtu, na umbo la taya, mdomo, meno na hata kiasi cha mate. Hayo yote ni mambo muhimu yanayoweza kuainisha kwa nini baadhi ya watu meno yao yanaoza zaidi kuliko wengine. Baadhi ya meno yanaweza kuwa na vishimo na nyufa zinazoweza kuruhusu bakteri na tindikali kupenya kwa urahisi na baadhi ya wakati umbo la taya huweza kuzuia meno yasisafishike vizuri na

kuondoa vyema uchafu kinywani. Kiwango na namna mate yalivyo pia huweza kuathiri uozaji wa meno. Kwa mfano matundu na nyufa huwa haziko sana katika meno ya mbele ambako kuna mate mengi ikilinganishwa na meno ya nyuma. Bakteria wote walioko kinywani wanaweza kubadilisha wanga kuwa tindikali lakini aina ya streptococci na

Lactobacili wana uwezo mkubwa wa kutengeneza tindikali. Kuwepo kinywani vijidudu vya aina hii huongeza uwezekano wa meno kuoza. Baadhi ya watu wana kiasi kikubwa cha bakteria wanaosababisha meno kuoza kuliko watu wengine na hii ni kutokana na kuzembea katika kutunza na kuimarishwa usafi wa kinywa.


Wataalamu wanatwambia kuwa, usafi wa kinywa na matumizi ya dawa za meno zenye fluoride hupunguza kasi ya meno kuoza. Usafi wa meno ni pamoja na kupiga mswaki kila siku kwa kutumia dawa za meno zenye flouride, kutumia uzi wa meno kusafisha eneo lililo kati ya meno, kuchokonea meno kwa kijiti ili kundoa mabaki ya chakula na kufanyiwa uchunguzi wa meno mara kwa mara. Flouride huzuia kupungua madini katika molekuli za meno, kuongeza madini hayo kwenye meno na kuimarisha meno ili yasiathiriwe na tindikali. Matumizi ya fluoride kwa kiwango

kinachotakiwa huzuia na kudhibiti matundu kwenye meno. Flouride inaweza kupatikana kutoka katika maji ya kunywa na baadhi ya vinywaji vilivyoongezwa mada hiyo. Pia mada hiyo hutiwa katika dawa za mswaki, geli na dawa za kusafishia kinywa. Katika baadhi ya nchi mada ya fluoride huongezwa hata katika chumvi na maziwa. Kiwango cha flouride katika maji ya kunywa na vyakula kinapaswa kuzingatiwa kwa mujibu wa mahitaji ya mwili. Suala hili ni muhimu kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 6 ambao meno yao bado yanakua. Kutumiwa sana au kwa kiwango kikubwa mada hiyo husababisha matatizo katika enamel au mfupa wa jino hali inayojulikana kinaalamu kama kama fluorosis.


Vyakula na athari yake katika kuoza meno

Ijapokuwa katika nchi nyingi kuoza meno kumekuwa kukiambatanishwa na matumizi ya fluoride na utunzaji wa kinywa, aina ya vyakula anavyokula mtu pia ni jambo muhimu linalochangia meno kuoza. Jinsi chakula chenyewe kilivyo kwa mfano kama kinanata na kung'ang'ania kwenye meno pia husababisha meno kuoza. Vyakula

vinavyong'ang'ania kwenye meno kama vile bisikuti na crips huongeza uwezekano wa kuoza meno kwani hubakia juu ya meno kwa muda mrefu zaidi kuliko vyakula vingine. Pia vyakula vyenye sukari zinazoyeyuka kwa haraka husafishwa kwa wepesi kinywani na mate, na kila vyakula vyenye wanga vinavyokaa muda mrefu kinywani na kuzunguka meno, ndivyo bakteria wanavyopata fursa zaidi ya kutengeneza tindikali na kuondoa madini katika meno. Kila tunapokula vyakula vyenye wanga, bakteria walioko kwenye kinywa huanza kutengeneza asidi suala linalopelekea meno kuoza. Mwenendo huu huendelea hadi baada ya dakika 10 hadi 20 baada ya kula au kunywa. Katika kipindi tusichokula au kunywa mate huzimua tindikali na kusaidia kurejesha madini katika meno. Iwapo

vyakula au vinywaji vitaliwa mara kwa mara na kinywa kisipate muda wa kurejesha madini kwenye meno, hapo ndipo meno huanza kuoza. Kwa ajili hiyo tunashauriwa kutokula na kunywa wakati wote na pia kupunguza kula vyakula vyenye wanga na sukari kwa uchache tusile vyakula hivyo zaidi ya mara 6 kwa siku. Pia tunashauriwa kuhakikisha kuwa tunapiga mswaki meno kwa kutumia dawa za meno zenye fluoride, kwa uchache mara mbili kwa siku.


Mmomonyoko wa meno

Mmomonyoko wa meno ni kuharibika tishu ngumu ya juu ya meno kutokana na acidi bila kuathiriwa na bakteria wanaosababisha meno kuoza. Kuna vyakula na vinywaji vingi vyenye tindikali katika lishe zetu na kuna uwezekano suala hilo likatuathiri. Kwa mfano kupendelea sana kula vyakula au kunywa vinywaji vyenye tindikali husababisha mmomonyoko wa meno. Tatizo hilo lisiposhughulikiwa huweza kuathiri ufanisi wa kinywa na hutofautiana baina ya

watu. Ili kuepukana na tatizo hilo tunashauriwa kujiepusha kupenda sana kunywa vinywaji au kula vyakula vyenye acidi na kupiga mswaki kwa uchache mara mbili kwa siku kwa kutumia dawa ya mswaki yenye fluoride. Pia tunashauriwa kutopiga mswaki mara tu baada ya kunywa au kula chakula chenye acidi kwani kufanya hivyo huweza kuyafanya meno yaharibike kutokana na kusugua meno wakati tindikali ikiwemo kinywani. Pia ni bora tujizoeshe kutafuna chingamu au ubani mara tu baada ya kula vyakula vyenye acidi ili kufanya mate yatengenezwe ambayo husaidia kuondoa acidi mdomoni.

MARADHI YA FIZI NA MENO




Aina za maradhi ya fizi na dalili zake

Kupiga mswaki na kutunza meno sio suala gumu na iwapo tutapiga mswaki ipaswavyo pamoja na kutumia nyuzi kusafisha katikati ya meno, tunaweza kuzua maradhi ya fizi na pia meno kuoza. Maradhi ya fizi husababishwa na utando kwenye meno unaotengenezwa na bakteria, ute na chembechembe nyinginezo zinazoganda kwenye meno. 

Kwa mujibu wa Taasisi ya Meno ya Marekani (ADA) iwapo utando katika meno hautaondolewa huwa mgumu na kuwa ugwagwa wa meno au tarter inayotumiwa na bakteria. Mchanganyiko wa utando na ugwagwa katika meno husababisha uvimbe kwenye fizi hali inayojulikana kitaalamu kama gingivitis. Ukoga wa meno au ugwagwa 

unaweza kundolewe na daktari wa meno au dentist.Maradhi ya fizi yana awamu tatu. Awamu ya kwanza kama tulivyosema ni gingivitis, ambapo fizi huwa nyukundu, huvimba na hutokwa na damu kwa urahisi. Iwapo hali hiyo itagundulika mapema inaweza kutatuliwa kwa kupiga mswaki vizuri na kutumia nyuzi kusafisha katikati ya meno.Awamu ya pili ya ugonjwa wa fizi ni hali ijulikanayo kama Periodontitis ambapo uvimbe hutokea kuzunguka 

jino. Awamu hii ni iliyoendelea zaidi ya ugonjwa wa fizi inayotokea wakati sumu ya bakteria katika utando inapoharibu fizi zilizoshikilia jino. Suala hilo husababisha fizi ziachane na jino na kutengeneza mada haribifu. Baadhi ya wakati mfupa ulioliwa kuzunguka jino unaweza kuonekana. Matibabu ya maradhi haya ya fizi ni muhimu sana ili kuzuia mmomonyoko wa mfupa na kung'oka meno.Awamu ya tatu ya maradhi ya fizi ni periodontitis iliyoendelea. Katika steji hii uharibifu wa fizi huwa mkubwa zaidi kuliko kabla na mfupa wa jino hulika. Pia meno huweza kung'oka na baadhi ya wakati huhitaji kung'olewa iwapo matibabu hayatosaidia.

Dalili za maradhi ya fizi

Hapa linajitokeza swali kwamba ni zipi dalili zinazojitokeza wakati mtu anapokuwa na ugonjwa wa fizi ulioendelea? Dalili za advanced periodontitis ni kuwa na harufu mbaya ya mdomo ambayo haiishi. Fizi kuvimba, kuwa nyekundu na laini. Dalili nyingine ni fizi kusogea mbali na meno, kuhisi maumivu wakati wa kutafuna na kupoteza hisia katika meno.

Sababu za maradhi ya fizi

Kuna sababu mbalimbali zinazoweza kumfanya mtu awe katika hatari ya kupatwa na magonjwa ya fizi. Miongoni mwa sababu hizo ni kuvuta sigara au kutafuna tumbaku. Mbali ya kuwa uvutaji sigara unaathiri mwili wa binadamu kwa njia tofauti, moja ya athari za ufutaji sigara hudhihirika katika kinywa cha mtu. Kwa kuwa moshi wa sigara 

hupita kwenye meno na fizi, kinywa cha mvuta sigara huwa kituo cha nicotine ambayo huharibu muonekano wa meno kwa kuyabadilisha rangi na kuacha harufu mbaya kinywani. Si hayo tu bali uvutaji sigara pia huathiri tishu za fizi na kupunguza mtiririko wa damu katika fizi, na kuleta uharibifu unaosababisha fizi zisogee mbali na 

meno.Wataalamu wanatuarifu kuwa, asilimia 75 ya watu wanaosumbuliwa na ugonjwa wa fizi ni watu wazima huku wale wanaovuta sigara wakiwa kwenye hatari ya kusumbuliwa na ugonjwa huo mara 7 zaidi ikilinganishwa na watu wasiovuta sigara.Sababu nyingine inayochangia katika kupata ugonjwa wa fizi ni mabadiliko ya homoni kwa wasichana na wanawake. Wanawake wako katika hatari zaidi ya kupata matatizo ya kinywa na meno kuliko wanaume kutokana na mabadiliko ya homoni yanayosababishwa na maumbile yao. Sio tu mabadiliko ya homoni 

kwa wanawake na watoto huathiri mtiririko wa damu katika tishu za fizi, bali pia huchangia katika suala zima la kupatikana ugando kwenye meno au plague unaosababisha meno kuoza. Mabadiliko ya homoni huwafanya wanawake wawe kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa fizi wanapokuwa katika hali tofauti kwenye maisha yao ambazo ni wakati wa kubalehe, wakati wa hedhi, wanapotumia vidonge vya kuzuia mimba, wanapokuwa 

wajawazito na wakati wanapoacha kupata hedhi yaani menopause. Hayo yote husababishwa na mabadiliko yanayoshuhudiwa katika homoni za estrogen na progesterone kwenye vipindi hivyo. Kwa sababu hiyo tunaweza kusema kuwa, watoto wa kike, wasichana na wanawake kwa ujumla wanapaswa kuzingatia zaidi usafi na utunzaji 

wa fizi na meno ili kuepusha uharibifu wa meno unaowapata zaidi kutokana na jinsia yao kuliko wanaume.Sababu nyingine inayoweza kumfanya mtu apatwe na maradhi ya fizi ni ugonjwa wa kisukari. Madaktari wanatuambia kuwa, watu walio na ugonjwa wa kisukari ambao hawadhibiti vyema ugonjwa huo, wako katika hatari zaidi ya kupata matatizo ya meno na maambukizi katika fizi. Hii ni kwa sababu ugonjwa wa kisukari hupunguza mtiririko wa 

damu kwenye fizi na pia kiwango cha juu cha sukari kwenye damu husababisha kinywa kiwe kikavu na kuzidisha ugonjwa wa fizi. Upungufu wa mate mdomoni huongeza bakteria wanaoharibu meno na kuleta utando. Iwapo mtu mwenye kisukari atadhibiti ipasavyo kiwango cha sukari kwenye damu, hatari ya kupata matatizo ya meno hupungua.

Namna ya kuzuia maradhi ya fizi

Suala muhimu zaidi linaloweza kuzuia mtu asipatwe na maradhi ya fizi na kuoza meno ni kupiga mswaki na kutumia nyuzi kuondosha uchafu katikati ya meno kwa uchache mara moja kila siku. Suala hilo linaweza kuzuia maradhi ya fizi, meno kutoboka na kung'oka. Licha ya kusafisha meno kila siku, jambo jingine muhimu ni kufanyiwa uchunguzi na daktari wa meno kwa uchache mara moja kwa mwaka. Hii ni kwa sababu hata kama tunajitahidi kwa kiasi gani kupiga mswaki, lakini mgando na ugwagwa hujitokeza na kusababisha matatizo katika fizi.


Je, ni Namna gani tupige mswaki kwa njia iliyo sahihi?
Kwanza kabisa tunashauriwa kupiga mswaki asubuhi na kabla ya kwenda kulala. Ikiwezekana piga mswaki baada ya kula chakula. Kama hauwezi, piga mswaki baada ya kula vyakula vya sukari. Tunapaswa kutumia mswaki laiini na wa wasitani, kwani mswaki mkubwa hautafika kwenye meno ya nyuma ilhali ule ulio mdogo utakufanya utumie 

wakati mwingi sana katika kusugua meno. Ikiwa unahitaji usaidizi katika kuchagua mswaki, pata ushauri kutoka kwa daktari wako wa meno. Tumia dawa ya meno iliyo na floraidi. Watoto wanapaswa kutumia kiasi kidogo cha dawa ya meno na watu wazima watie dawa ya meno kulingana na urefu wa nywele za mswaki.Wataalamu 

wanatushauri kubadilisha mswaki pindi ule tunaotumia unapochoka, kila baada ya miezi mitatu au minne. Pia tunashauri kuwa ni vizuri kubadilisha mswaki mpya kila baada ya kupata mafua, uvimbe katika koo na magonjwa mengineyo kama hayo.

Kumbuka kusugua pande zote za meno kwa njia ifuatayo:
Sugua meno yako polepole bila kutumia nguvu kutoka sehemu ya nyuma hadi mbele. Sugua karibu na ufizi kwa mwendo wa mviringo, ili mswaki ufike sehemu ambapo meno na ufizi zinakutanika mahali ambako chembechembe za chakula hujificha.Sugua sehemu zote za meno, sehemu ya nje, sehemu ya kutafunia chakula na 

sehemu ya ndani ya meno.Tumia sehemu ya juu ya mswaki kusafisha sehemu ya ndani ya meno ya juu, kwa mwendo wa juu na chini.Sugua ulimi wako kwa upole ili kuondoa vijidudu au viini vinavyosababisha harufu mbaya.Sukutua na hifadhi mswaki wako sehemu nzuri na salama kwa matumizi ya baadaye.