Showing posts with label MATUMIZI YA HABBAT SAWDA. Show all posts
Showing posts with label MATUMIZI YA HABBAT SAWDA. Show all posts

Saturday, 3 January 2015

Black Cumin Seed Oil – The Most Powerful Oil In The World?

Black Cumin Seed (Nigella Sativa) oil has been used in traditional medicine since the beginning of civilization. It was called Panacea (which roughly translates to ‘cure-all’) in Ancient Egypt; it was found in the tomb of King Tut and it is said that Cleopatra used it as a beauty treatment. Hippocrates, the famous Greek physician, used it to cure digestive and metabolic disorders. The Prophet Muhammad called it “a remedy for every illness except death.
The oil has also been recommended by practitioners of Ayurveda and Chinese Traditional Medicine for thousands of years for conditions from diabetes to indigestion to cancer. In recent years, it has been put to the test of modern science and several studies confirm its long reported health benefits. Black Cumin Seed Oil is also known as Blackseed, Black Onion Seed, Black Caraway Seed and Black Sesame Seed. If you find a product labeled under one of these names, be sure it is real Nigella Sativa before purchasing.

What Makes it So Magical?

The main active compound in the oil is called crystalline nigellone, which you’ve likely never heard of as it is only found in certain black seeds.  It also contains several nutrients, essential acids and compounds including:
Beta Sitosterol
Calcium
Copper
Folic Acid
Iron
Oleic, Linoleic and Linelenic Acids (Omegas 3 & 6)
Palmitol
Phosphorous
Protein
Stearic Acid
Thymoquinone
Vitmins B1, B2 & B3
Zinc

Black Cumin Seed Oil as a Cancer-Fighter 

Nigella Sativa has been involved in hundreds of studies regarding health, and particularly cancer treatment and prevention. One of the active ingredients listed above, Thymoquinone, has been found to be particularly effective in reducing the size of existing tumors. In studies on rats and humans, researchers found that Black Cumin Seed Oil:
  • Inhibited tumor growth by up to 50%
  • Increased the growth of healthy bone marrow cells by 250%
  • Helps to protect the body against damage from chemotherapy and radiation
  • Has strong anti-bacterial and anti-inflammatory properties
  • Aides in the production of natural interferon
  • Can even deactivate or kill certain types of cancer cells

Miraculous Results for Many Conditions through Improved Immune Function

Overall, the greatest benefit of Black Cumin Seed is its effect on the immune system and metabolism – which, in turn, supports all the functions of the body. The active compounds in the oil have been proven to fight several diseases by naturally boosting the body’s production of immune cells, bone marrow, and natural interferon. It also protects the liver (your body’s filtering system) from toxicity. Even for people in the best health, regular supplementation with Black Cumin Seed Oil can greatly increase their overall sense of health and well-being.
Some of the many conditions successfully treated with regular ingestion of Black Cumin Oil, over an extended period of time (6 months or more), include:
Allergies and Sinusitis
Anxiety and Nervous Tension
Bronchitis
Colds and Flus
Colic (babies)
Diabetes
Diarrhea, Indigestion and Heartburn
Hair Loss
Headaches and Migraines
High Blood Pressure
Insomnia
Intestinal Parasites
Lethargy and Depression 

How to Take Black Cumin Seed Oil 

Health experts and natural physicians generally recommend taking one teaspoon of the oil twice a day, about one hour before a meal. You can take the oil on its own, mixed in juice, or followed by hot tea – as it has a bit of a spicy flavor to it. If you purchase oil, make sure to buy the first cold pressed variety. Most people choose to take the oil in capsule form, which gives the same benefit. You can easily find high quality Black Cumin Seed Oil in liquid or capsule form on Amazon.

Black Cumin Seed Oil as a Skin Treatment and Beauty Trick

People who consume Black Cumin Seed Oil for health often report an unexpected side effect – their skin, hair and nails are noticeably healthier after just a few months. To those who know the oil well, it’s not too surprising, as for thousands of years (remember Cleopatra) people have been using it as an ingredient in beauty creams.
There are some beauty products and skin treatments on the market, commonly found in Indian and Lebanese markets or online, that contain Black Cumin Seed Oil (check out this one from Nadina). But many people prefer to mix a small amount of the oil into their favorite face cream. People who have tried it, generally swear by it. I know some who recommend it to everyone, and some who try to keep it as their very own beauty secret.
The oil-cream mixture helps to prevent blemishes, fine lines, age spots, dry or oily skin, and always leaves their skin looking young, soft and supple. It’s also great for the rough skin that can develop on hands, feet, elbows and knees. The solution is not only effective as a beauty treatment, it can treat several serious skin conditions when applied directly to problem issues. It has been proved effective on:
Acne
Backache, arthritis and rheumatism
Burns
Eczema
Fungal and other Infections
Joint Pain
Psoriasis
Sore Muscles

Where To Buy Black Cumin Seed Oil

There are a number of different varieties of Black Cumin Seed Oil available to buy. Make sure you buy the cold pressed variety. You can see a number of different brands of Black Cumin Seed Oil here on Amazon.com

Wednesday, 9 July 2014

Black Seed Extract 'Cures' HIV Patient Naturally




There are words you don't use in medicine today, such as "cure." But a remarkable case study in an HIV positive patient treated with black seed extract resulted in a sustained remission, indicating a safe, accessible and affordable alternative to highly toxic antiretroviral HIV drugs may already exist.
Nigella Sativa, also known as 'black seed,' has been studied for a wide rage of health benefits, but not until recently was it discovered to hold promise as a curative agent against potentially lethal viral infections, including Hepatitis C[i] and now HIV.
A remarkable case study published in August of this year in the African Journal of Traditional, Complementary, and Alternative Medicine described an HIV patient who after undergoing treatment with a black seed extract experienced a complete recovery, with no detectable HIV virus or antibodies against HIV in their blood serum, both during and long after the therapy ended.[ii]
This was a remarkable and unexpected observation, described by the researchers as follows:
"Nigella sativa had been documented to possess many therapeutic functions in medicine but the least expected is sero-reversion in HIV infection which is very rare despite extensive therapy with highly active anti-retroviral therapy (HAART). " [emphasis added]




Despite its commonplace use as the standard of care for HIV treatment globally, anti-retroviral therapy remains highly controversial, in part because the adverse health effects of the drug class may outstrip those associated with the HIV infection itself.  This is especially true in cases where the infection was treated 'early,' having been discovered through routine blood work in asymptomatic and otherwise still healthy patients. Drug therapy can also produce selective pressure on the HIV virus to mutate and gain resistance, with the net effect that a stronger, more drug-resistant form of HIV is produced in the body at the same time that the drugs have done severe and even irreversible damage to the patient's immune system.  Sadly, however, the decline and ultimate death of the patient is rarely if ever attributed to the treatment (and its many iatrogenic effects) but rather to the "disease" itself – a well-known problem in our failed 'war against cancer' where the victim (patient) and the 'the cancer' gets blamed for the incessant failure and even disease-promoting properties of chemotherapy, radiation and surgery. 
This is all the more reason why the possibility that an ancient healing food like black seed -- which the research shows is generally safe, affordable and accessible -- can cure HIV is so exciting.   

The 'Miraculous' Recovery

At the outset of the study, the patient presented with classical symptoms of symptomatic HIV infection, "with [a] history of chronic fever, diarrhoea, weight loss and multiple papular pruritic lesions of 3 months duration." Examination identified moderate weight loss, with laboratory confirmed tests showing 'sero-positivity' to HIV infection with a "pre-treatment viral (HIV-RNA) load and CD4 count of 27,000 copies/ml and CD4 count of 250 cells/ mm(3) respectively."
CD4 cells are essential for the adaptive immune response in the body against a wide range of opportunistic infections and is the primary target of HIV infection. CD4 cell count and status therefore represent a primary diagnostic marker for the severity of HIV infection and the patient's prognosis.
The patient was administered a black seed concoction of 10 mls twice daily for 6 months, resulting in a rapid improvement in symptoms, and significant reductions in viral load:
"Fever, diarrhoea and multiple pruritic lesions disappeared on 5th, 7th and 20th day respectively on Nigella sativa therapy. The CD4 count decreased to 160 cells/ mm3 despite significant reduction in viral load (≤1000 copies/ml) on 30th day on N. sativa."
By the 187th day on black seed therapy, testing indicating the blood was entirely cleared of signs of infection, a so-called 'sero-negative status'. The post-therapy CD4 counts increased from baseline to a normalized 650cells/ mm(3) with an undetectable viral (HIV-RNA) load.
Follow up tests revealed that even after 24 months without herbal therapy the patient's HIV tests remained normal, without any indication of infection or associated immune suppression.
They concluded:
 "This case report reflects the fact that there are possible therapeutic agents in Nigella sativa that may effectively control HIV infection."
Black seed is only one plant ally in the vast array of natural compounds with experimentally confirmed anti-HIV properties. GreenMedInfo.com's database contains research on natural substances capable of reducing antiretroviral drug toxicity, as well as that directly inhibit the replication of the HIV virus.

[i]  Eman Mahmoud Fathy Barakat, Lamia Mohamed El Wakeel, Radwa Samir Hagag. Effects of Nigella sativa on outcome of hepatitis C in Egypt.  World J Gastroenterol. 2013 Apr 28;19(16):2529-36. doi: 10.3748/wjg.v19.i16.2529.
[ii] Abdulfatah Adekunle Onifade, Andrew Paul Jewell, Waheed Adeola Adedeji. Nigella Sativa Concoction Induced Sustained Seroreversion in HIV Patient. Afr J Tradit Complement Altern Med. 2013 Aug 12;10(5):332-5. Source.http://www.greenmedinfo.com/blog/black-seed-extract-%27cures%27-hiv-patient-naturally?page=2


Tuesday, 29 April 2014

TUMIENI MAFUTA YA HABBAT SAWDA KWA KUTIBU MARADHI MBALI MBALI







MATUMIZI ya mafuta ya habat soda ni mengi sana katika mwili wa binadamu lakini leo utajifunza na kufaidika na haya machache ambayo ninayaandika hapa chini:

KWA AFYA
Kunywa kijiko kimoja cha mafuta haya asubuhi na usiku, tena asubuhi unaweza kunywa kabla ya kifungua kinywa. Unaweza kunywa kijiko kimoja cha mafuta peke yake au ukachanganya na kijiko kimoja cha asali safi.

HAMU YA KULA
Kabla ya kuanza kula, jipatie kijiko kimoja cha mafuta hayo kisha kunywa maji ya kawaida au yaliyochanganywa na siki kidogo.


VIPELE, CHUNUSI NA NGOZI

Changanya na pasha moto kwa dakika mbili kikombe kimoja cha habat soda iliyosagwa, ½ (nusu) kikombe cha maganda ya komamanga yaliyosagwa, na ½ (nusu) kikombe cha siki ambayo inatokana na juisi ya tufaha (apple). Paka sehemu inayotakiwa kabla ya kwenda kulala kila usiku mpaka vipele (chunusi) vitakapoondoka. Mchanganyiko huu unaweza kukaa mpaka wiki tatu, ni lazima uuweke katika hali ya baridi.

PUMU
Weka kijiko cha habat soda iliyochemshwa katika maji yaliyochemshwa kisha unywe ikiwa ya moto.

KUTIBU MGONGO
(sehemu ya chini)

Changanya asali pamoja na ¼ (robo) kijiko cha habat soda kunywa kabla hujala kitu chochote wakati wa asubuhi.

KIBOFU/FIGO

Kama unasumbuliwa na kibofu cha mkojo au figo, tumia asali kila asubuhi kabla ya kufungua kinywa. Changanya vikombe viwili vya habat soda iliyosagwa na ½ (nusu) kikombe cha asali safi.

Kunywa kijiko kimoja cha mchanganyiko huu pamoja na kikombe kimoja cha maji ya moto kila asubuhi kabla ya kufungua kinywa. Mchanganyiko wa asali na habat soda unaweza kukaa kwa siku 15 tu na hifadhi kwenye baridi.

KIKOHOZI

Tumia matone matatu au manne ya mafuta ya habat soda kwenye kahawa au chai.
Kunywa kijiko kimoja cha habat soda na asali mchana na usiku. Pia kwa wenye matatizo ya kutokwa na haja ndogo (mkojo): Kunywa kijiko kimoja cha habat soda pamoja na asali, kisha kunywa maji ya uvuguvugu.

NGOZI KAVU
Kwa wale wenye ngozi kavu changanya asali pamoja na robo kijiko cha mafuta ya habat soda, kunywa wakati wa asubuhi kabla ya kufungua kinywa.

MINYOO:
Kunywa habat soda pamoja na siki kuondoa minyoo ya aina yoyote ile, inaweza kuwa ya limao au ya tufaha ‘apple’.

KICHWA
Kama unasumbuliwa na kichwa, chukua unga wa habat soda, karafuu iliyosagwa nusu, kijiko cha habat sauda kisha uchanganye.
chukua kijiko kimoja cha chai kisha kunywa na mafuta yake unaweza kupaka kichwani.

USINGIZI
Kama una tatizo la kukosa usingizi, chukua kijiko kimoja cha habat soda changanya na maziwa glasi moja pamoja na asali kijiko kimoja kikubwa kisha kunywa.

SIKIO
Chukua tone moja la mafuta ya habat soda nyunyizia ndani ya sikio husaidia kulisafisha na kuliponya kabisa.

MALENGELENGE
Chukua mafuta ya habat soda jipake mpaka yaishe.

MARADHI YA WANAWAKE
Tumia mafuta ya habat soda, kunywa kwenye kila kinywaji cha moto, unaweza kuweka kijiko kimoja kwenye maziwa, kwenye maji ya moto, kwenye supu n.k.
Mbali na matatizo hayo pia inasaidia kusafisha kizazi na ni rahisi kwa mwanamke asiyezaa kushika mimba kwa haraka.

KUSIKIA VIZURI
Mtu mwenye ugonjwa wa kutosikia achemshe habat soda na karafuu, anywe bila kuongeza kitu chochote mara tatu kwa siku atapona.

VIDONDA
Kama una kidonda changanya matone kumi ya mafuta ya habat soda katika kikombe cha asali na kijiko kimoja cha maganda ya komamanga yaliyokaushwa na kusagwa. Kula mchanganyiko huu kabla ya kula chakula baadaye kunywa glasi ya maziwa yasiyotiwa kitu chochote.

Saturday, 26 April 2014

Matumizi Ya Kunufaisha Ya Habbat Sawdaa (Haba Soda - Chembe Nyeusi )




((Habbat-Sawdaa inatibu kila kitu isipokuwa mauti)).
Yafuatayo hapa chini ni baadhi ya matatizo na magonjwa ambayo yanaweza kutibika kwa kirahisi kwa kutumia Habbat-Sawdaa.
Kwa faida ya Afya kwa ujumla:
Kunywa kijiko kimoja cha mafuta ya Habbat-Sawdaa asubuhi na usiku, au kunywa japo asubuhi kabla ya kifungua kinywa, unaweza kunywa kijiko kimoja cha mafuta peke yake au ukachanganya na kijiko kimoja cha asali safi.
Vipele (chunusi) Na Ngozi:
Changanya na pasha moto kwa dakika mbili kikombe kimoja cha Habbat-Sawdaa iliyosagwa, ½ (nusu) kikombe cha maganda ya komamanga yaliyosagwa, na ½ (nusu) kikombe cha siki ambayo inatokana na juisi ya tofaha (apple). Paka katika sehemu inayotakiwa kabla ya kwenda kulala kila usiku mpaka vipele (chunusi) vitakapoondoka. Mchanganyiko unaweza kukaa mpaka wiki tatu na ni lazima uwekwe katika hali ya ubaridi.
Upara (Alopeshia):
Sugua mafuta ya Habbat-Sawdaa katika mabaka yanayokusumuba.
Pumu:
Tia ½ (nusu) kijiko cha Habbat-Sawdaa iliyochemshwa katika maji ya yaliyochemshwa kisha unywe moto.
 Kuumwa kwa Mgongo (Sehemu ya Chini):
Changanya asali pamoja na ¼ (robo) kijiko cha Habbat-Sawdaa na iwe kitu cha kwanza kunywa wakati wa asubuhi kabla ya kufungua kinywa.
Mwiba Wa Nyuki Na Nyigu:
Tia ½ (nusu) kijiko cha Habbat-Sawdaa iliyochemshwa katika maji ya yaliyochemshwa kisha unywe moto.
 Kibofu cha Mkojo/Figo:
Kunywa maji ya moto yaliyochanganywa na½ (nusu) kijiko cha Habbat-Sawdaa pamoja na asali kila asubuhi kabla ya kufungua kinywa. Changanya vikombe viwili vya Habbat-Sawdaa iliyosagwa na ½ (nusu) kikombe cha asali safi. Kunywa kijiko kimoja cha mchanganyiko pamoja na kikombe kimoja cha maji ya moto kila asubuhi kabla ya kufungua kinywa. Mchanganyiko unaweza kukaa kwa siku 15 na ni lazima uwekwe katika hali ya ubaridi.
Jiwe La Figo:
Kikombe kimoja cha Habbat-Sawdaa iliyochanganwa pamoja na gilasi (bilauri) moja ya asali, vitunguu saumu vitatu vilivyosagwa na karafuu. Changanya vitunguu saumu pamoja na asali na Habbat-Sawdaa. Kunywa kijiko kimoja kabla ya kula chakula na kwa pendekezo kula limau (bila ya kumenywa). Rudia haya kwa wiki moja Insha-Allah jiwe litaondoka.
Maathiriko Ya Figo:
Changanya baadhi ya Habbat-Sawdaa pamoja na mafuta ya alizeti. Chukua mchanganyiko na weka katika sehemu ambapo figo limeathirika. Kunywa kijiko cha Habbat-Sawdaa asubuhi. Rudia haya kwa muda wa wiki moja Insha-Allah maathiriko yatatibika.
Mafua:
Chukua mbegu za Habbat-Sawdaa 21, ziweke katika kitambaa na roweka usiku. Tumia kama matone kwenye pua siku ya pili nusa poda ya Habbat-Sawdaa iliyomo katika kitambaa.
 Kikohozi:
Tumia matone matatu au manne ya mafuta ya Habbat-Sawdaa kwenye kahawa au chai.
Bawasiri:
Kula unga wa Habbat-Sawdaa pamoja na maji.
Shinikizo la damu (high blood pressure):
Changanya kijiko kimoja cha Habbat-Sawdaa iliyosagwa, kijiko kimoja cha asali safi na kitunguu kiasi kidogo. Chukua mchanganyo kabla ya kufungua kinywa kwa siku ishirini.
 Uwasho Na Maumivu Ya Jino Na Ufizi:
Chemsha Habbat-Sawdaa katika siki na itumie kwa kusukutulia meno na ufizi. Na jikinge kutumia dawa za msuwaki za kibiashara na tumia dawa za msuwaki ambazo zinatengenezwa kutoka kwenye nyuzi za mboga za mti wa siwak ambao kwa karne ulikuwa unatumiwa na Wahindi, Waafrika na Waarabu, ni msuwaki wa kiasili.
Kumbukumbu (memory):
Kunywa kijiko kimoja cha unga wa Habbat-Sawdaa na changanya na asali mara mbili kwa siku.
Utaratibu Wa Ulinzi Wa Mwili:
Kula kijiko kimoja cha Habbat-Sawdaa na asali mchana na usiku Kutoweza kuzuia haja ndogo (mkojo): Kunywa kijiko kimoja cha Habbat-Sawdaa pamoja na asali, kisha kunywa maji ya vugu vugu.
Jaundice:
Tumia Habbat-Sawdaa pamoja na maziwa.
Maumivu Sugu ya kichwa (Maumivu ya kichwa ya upande mmoja, maumivu ya kichwa):
Kaanga Habbat-Sawdaa na iweke katika kitambaa cha pamba, funga au weka tu kitambaa katika kikomo (kipaji cha uso). Roweka Habbat-Sawdaa ndani ya siki wakati wa usiku, siku ya pili ivuruge kufanya unga. Ingiza katika pua halafu vuta pumzi.
Ngozi kavu:
Changanya asali pamoja na robo kijiko cha Habbat-Sawdaa na iwe kitu cha kwanza kunywa wakati wa asubuhi kabla ya kufungua kinywa.
Upepo:
Changanya asali pamoja na robo kijiko cha Habbat-Sawdaa na iwe kitu cha kwanza kunywa wakati wa asubuhi kabla ya kufungua kinywa.
Minyoo:
Kunywa Habbat-Sawdaa pamoja na siki kuondoa minyoo.

Kunyonyoka Nywele
Ataukanda unga wa Habbat-Sawdaa katika juisi ya chirichiri   pamoja na kijiko cha siki nyepesi na kikombe cha mafuta ya zeituni, halafu asugue kichwani kwa mafuta hayo kila siku jioni pamoja na kukiosha kichwa kwa maji na sabuni kabla ya kupaka.
Maumivu ya Kichwa
Atachukua unga wa Habbat-Sawdaa, karafuu iliosagwa nusu ya kiwango cha Habbat-Sawdaa  na anisuni (anise), halafu achanganye pamoja. Achukue kiasi cha kijiko kimoja (cha chai), wakati wa kuumwa na kichwa, na ale na maziwa lala (mala), pamoja na kupasugua mahala paumapo kwa mafuta ya Habbat-Sawdaa .
Ukosefu Wa Usingizi
Atachukua kijiko cha Habbat-Sawdaa, achanganye na gilasi ya maziwa moto  yaliochanganywa na asali, baada ya kupoa kiasi atakunywa.
Chawa Na Mayai Yake
Atachukua unga wa Habbat-Sawdaa uliosagwa vizuri aukande kwenye siki mpaka uwe kama marhamu, halafu ajipake kichwani – baada ya kunyoa nywele au kuisugua marhamu kwenye mashina ya nywele, halafu aketi katika mwanga wa jua kitambo cha robo-saa. Na hataosha kichwa ila baada ya masaa matano. Atafanya hivyo kila siku kwa muda wa wiki moja.
Kisunzi Na Maumivu Ya Sikio
Tone moja la mafuta ya Habbat-Sawdaa ndani ya sikio husafisha sikio, pamoja na kuyanywa na kusugua sehemu za panda na nyuma ya kichwa, humaliza kisunzi.
Upaa Na Mabaka
Utachukua kijiko cha unga wa Habbat-Sawdaa, siki kiasi cha kikombe kimoja na juisi ya kitunguu saumu kiasi cha kijiko kidogo, vyote hivyo utavichanganya na vitakua namna ya   marhamu, utajipaka baada ya kunyoa sehemu ya nywele na kuchanja kidogo – kisha utafunga bendeji, utaiacha mpaka asubuhi, baadae utajipaka mafuta ya Habbat-Sawdaa,utaendelea hivyo kwa muda wa wiki moja.
Malengelenge ya Neva katika Ngozi
Atajipaka – sehemu ya malengelenge – mafuta ya Habbat-Sawdaa mara tatu kila siku mpaka iondoke kwa Uwezo wa Allah.  
Maradhi Ya Wanawake Na Uzazi
Dawa kubwa inayosahilisha kuzaa ni Habbat-Sawdaa iliochemshwa ikachanganywa na asali na kiziduo cha babunaji (chamomile). Habat sawdaa  ni kama burashi katika uke wa mwanamke yenye faida kubwa kwao pamoja na kutumua mafuta ya Habbat-Sawdaa katika kila kinywaji cha moto kwa maradhi yote ya wanawake.
Meno Na Maumivu Ya Mafido na Koo
Kiziduo cha Habbat-Sawdaa na kutumia kwa kusukutua kwa kugogomoa, husaidia mno maradhi yote ya mdomo na koo, vivyo hivyo pamoja na kubugia kijiko cha Habbat-Sawdaa na kumeza kwa maji yenye vuguvugu kila siku na kujipaka mafuta yake sehemu ya koo kwa nje na kuusugua ufizi kwa ndani. 
Maradhi Ya Tezi
Atachukua unga wa Habbat-Sawdaa na aukande kwa asali na mkate wa nyuki kila siku, kwa kipindi cha mwezi mmoja. 
Chunusi (Acne)
Atachukua unga wa Habbat-Sawdaa aukande katika mafuta ya ufuta (simsimu) pamoja na kijiko cha unga wa ngano. Vyote hivyo atajipaka usoni kuanzia jioni hadi asubuhi, halafu ataosha kwa maji yenye vuguvugu kwa sabuni. Ataendelea kufanya hivyo kwa muda wa wiki moja. Na awe akinywa mafuta ya Habbat-Sawdaa katika kinywaji chochote cha moto.
Maradhi Yote ya Ngozi
Atachukua mafuta ya Habbat-Sawdaa, mafuta ya waridi (marashi jabali) na unga wa ngano asili, vyote hivyo  kwa viwango sawa, ule unga wa ngano uwe zaidi kuliko mafuta, halafu aukande vizuri. Kabla ya kujipaka, apanguse sehemu yenye ungonjwa kwa kitambaa kilichoroweshwa siki nyepesi, halafu aketi kwenye jua, baadae ajipake dawa hio kila siku. Lakini ajizuie na kila chenye kuchochea hisia kama vile, samaki, mayai, maembe na mfano wake.                                                  

Chunjua (Wart)
Atachukua unga wa Habbat-Sawdaa aukande katika siki nzito na asugue kwa kitambaa cha sufi au katani mahala pa sugu asubuhi na jioni kwa muda wa wiki moja.
Kuung`arisha Uso Na Kuurembesha
Ataukanda unga wa Habbat-Sawdaa katika mafuta ya zeituni, na atajipaka usoni halafu apigwe na mwanga wa jua kidogo. Tiba hiyo ataifanya wakati wowote katika mchana na siku yeyote.
Kuunganisha Mvunjiko Haraka
Supu ya adesi (dengu), kitunguu maji pamoja na yai la kuchemsha na kijiko kikubwa cha unga wa Habbat-Sawdaa , utachanganya na supu hiyo japo siku baada ya siku; halafu anywe. Na atasugua sehemu zilizo karibu na mvunjiko kwa mafuta ya Habbat-Sawdaa, na baada ya kufungua bendeji atajisugua kwa mafuta ya Habbat-Sawdaa yenye vuguvugu; kila siku.
Mvilio Wa Damu (Contusion)
Atachemsha vizuri konde moja la Habbat-Sawdaa katika chombo cha maji, kisha atakiingiza kiungo kilichovilia damu ndani ya maji hayo- yenye vuguvugu- kwa muda wa robo-saa au zaidi pamoja na kukitaharakisha kiungo hicho. Baada ya hapo atajipaka mafuta ya Habbat-Sawdaa bila ya kufunga kitu. Lakini hatakiwi kukipa uzito kiungo hicho au kukitaabisha. Tiba hiyo ataifanya kila siku kabla ya kulala.
Baridi Yabisi (Rheumatism)
Atachemsha mafuta ya Habbat-Sawdaa na atasugua kwayo ile sehemu yenye ugonjwa, atasugua kwa nguvu kama kwamba anasugua mfupa wala sio ngozi! Na atayanywa baada ya kuyachemsha vyema na kuyachanganya na asali kidogo. ataendelea na tiba hiyo huku akiwa ni mwenye imani na yakini kuwa Allah atamponya.
(Ki) Sukari (Diabetes)
Utachukua unga wa Habbat-Sawdaa kiasi cha kikombe kimoja, manemane (myrrh) iliosagwa kiasi cha kijiko kikubwa, habbarrashad nusu kikombe, komamanga iliosagwa kiasi cha kikombe kimoja, mzizi wa kabichi uliosagwa baada ya kukaushwa kiasi cha kikombe kimoja na kijiko kidogo cha mvuje. Vyote hivyo atavichanganya na atakula kabla ya kula chakula kiasi cha kijiko kimoja, atakula na maziwa lala ili iwe rahisi kumeza.
Shinikizo la Damu (High Blood)
Kila unywapo kinywaji cha moto, tia matone machache ya mafuta ya Habbat-Sawdaa. Pia ujipake mafuta hayo mwili wote, japo wiki mara moja.
Uvimbe Wa Figo (Nephritis)
Atatengeneza kibandiko (cha kitambaa) kutokana na unga wa Habbat-Sawdaa uliokandwa katika mafuta ya zeituni, atabandika sehemu yenye maumivu ya figo pamoja na kubugia funda la kijiko cha Habbat-Sawdaa kila siku kabla ya kula chakula kwa muda wa wiki moja tu; uvimbe utakwisha insha Allah.
Kuvunjavunja Vijiwe Vya Tumboni
Atachukua unga wa Habbat-Sawdaa kiasi cha kikombe kimoja kisha aukande katika kikombe cha asali, na atasaga kitunguu saumu punje tatu; atakua akichukua nusu yake akila kabla ya kula chakula kila siku. Pia itakua bora lau atakula limau kila baada ya kula dawa; kwani husafisha kabisa.
Kukojoa Kwa Maumivu (Dysuria)
Atapaka mafuta ya Habbat-Sawdaa juu ya kinena kabla ya kulala pamoja na kunywa kikombe cha mafuta hayo yaliochemshwa na kutiwa asali; kila siku kabla ya kulala.  
Jongo (Edema)
Ataweka kibandiko (cha kitambaa) cha unga wa Habbat-Sawdaa uliokandwa katika siki juu ya kitovu, kwanza ataweka kitambaa. Pia atakula Habbat-Sawdaa kijiko kimoja asubuhi na jioni kwa muda wa wiki moja.
Kifuko Cha Nyongo Na Vijiwe Vyake
Atachukua Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kimoja, manemane iliosagwa robo kijiko na asali kiasi cha kikombe kimoja; vyote hivyo atavichanganya viwe mraba (kama jamu); halafu awe akila kila asubuhi na jioni.
Wengu
Ataweka kibandiko (kilichopashwa moto) cha Habbat-Sawdaa iliokandwa katika mafuta ya zeti katika ubavu wa kushoto; jioni. Na wakati huo huo ata kunywa kikombe cha kiziduo cha uwatu kilichochanganywa na asali na mafuta ya Habbat-Sawdaa kidogo, ataendalea na dawa hiyo kwa muda wa wiki mbili mfululizo.
Maradhi Yote ya Kifua na Baridi
Atachukua mafuta ya Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kikubwa atie kwenye maji halafu ayaweke juu ya moto mpaka ianze kufuka moshi, hapo aanze kuuvuta ule moshi puani huku akiwa amejifunika kichwa ili ule moshi usiende upande mwingine. Atafanya hivyo kila siku kabla ya kulala, pamoja na kunywa kiziduo cha zaatari kilichochanganywa na unga wa Habbat-Sawdaa; asubuhi na jioni.
Moyo na Mzungukoa wa Damu
Kuwa na imani katika maneno ya Mtume (Swalla Llahu 'alayhi wa sallam) Kwa sababu jambo hili ni katika muktadha wa imani. Mtume (Swalla Llahu 'alayhi wa sallam) alipotuambia kuwa Habbat-Sawdaa ni dawa ya kila ugonjwa, basi hakuna shaka hata chembe kuwa ni dawa ya maradhi yote yanayomfika mwanaaadamu. Mgonjwa wa moyo asikate tamaa kutokana na rehma ya Allah; ni juu yake akithirishe kutumia Habbat-Sawdaa kwa namna yoyote iwayo; iwe ni kwa kula nzima au kwa kunywa wakati wowote uwao.
Mchango (Msokoto Wa Tumbo) (Colic)
Atachemsha vyema anisuni (anise)kamun ( cumin) na nana kwa vipimo sawa na atatia asali kidogo, halafu atie matone saba ya Habbat-Sawdaa ; atakunywa kinywaji hicho kikiwa na vuguvugu pamoja na kupaka mafuta ya Habbat-Sawdaa mahala panaposokota. Baada ya muda mchache maumivu yataondoka.
Kuhara
Atachukua juisi ya chirichiri iliochanganywa na unga wa Habbat-Sawdaa kijiko kikumbwa, atakunywa kiasi cha kikombe kimoja mara tatu kwa siku.
Uziwi
Atachemsha Habbat-Sawdaa pamoja na karafuu, na atakunywa bila ya kuongeza kitu; mara tatu kwa siku.
Gesi Na Maumivu
Atabugia unga laini wa Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kimoja kabla ya kula chakula akifwatisha gilasi ya maji yenye vuguvugu iliotiwa asali kiasi cha vijiko vitatu; atakariri kila siku kwa muda wa wiki moja.
Asidi (Acidness)
Matone kadhaa ya mafuta ya Habbat-Sawdaa yaliotiwa kwenye maziwa ya moto na asali; humaliza asidi.  

Uvimbe Wa Tumbo
Atachukuwa unga wa Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kimoja na kijiko cha urkusus (licorice) hivyo atavichanganya na juisi ya pea iliotengenezwa pamoja na kokwa zake; halafu anywe; ataona nafuu kubwa.
Maradhi Ya Macho
Atapaka mafuta ya Habbat-Sawdaa sehemu za panda kandokando ya macho na kope, atafanya hivyo kabla ya kulala pamoja na kunywa matone kadhaa ya mafuta ya Habbat-Sawdaa katika kinywaji chochote cha moto au katika juisi ya karoti.

Amiba (Vijidudu) (Amebiasis)
Atachukua unga wa Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kimoja pamoja na kijiko cha kitunguusaumu kilichosagwa, atachangana katika kikombe cha juisi ya nyanya iliotiwa chumvi kidogo; atakunywa kila siku kabla ya kula chakula kwa muda wa wiki mbili mfululizo.

Kichocho (Bilharziasis)
Atakula Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kimoja asubuhi na jioni, yawezekana kuila Habbat-Sawdaa katika chakula kama vile mkate pamoja na kujipaka mafuta yake katika ubavu wa kulia. Ataendelea na dawa hio kwa muda wa miezi mitatu mfululizo. Baadae atapata nguvu na nishati.

Kutoa Wadudu Tumboni
Atakula sandwichi moto ya vitu hivi: kijiko kimoja cha unga wa Habbat-Sawdaa, punje tatu za vitunguu, kijiko kimoja cha mafuta ya zeti, pilipilimanga kidogo na punje kumi za boga (calabash), asubuhi atakunywa kinywaji cha shimari au mafuta ya mbono mara moja pekee.

Utasa
Atachukua unga wa Habbat-Sawdaa, unga wa uwatu na mbegu ya figili kwa vipimo sawa, atakula kijiko kimoja asubuhi na jioni ilihali imekorogwa katika nusu kikombe cha asali, baadae atafuatisha kunywa kikombe kikubwa cha maziwa ya ngamia; basi inshaAllaah itakuwa kheri.

Tezikibofu (Prostate gland)
Atajipaka mafuta ya Habbat-Sawdaa chini ya mgongo na atajipaka chini ya korodani (mapumbu) na kusugua kwa mzunguko pamoja na kula unga wa Habbat-Sawdaa kijiko kimoja, na robo kijiko kidogo cha manemane katika nusu gilasi ya asali iliotiwa katika maji yenye vuguvugu; kila siku na wakati wowote apendao.

Pumu (Asthma)
Atanusa moshi wa mafuta a Habbat-Sawdaa asubuhi na jioni. Pia atakula unga wake asubuhi na jioni kabla ya kula chakula kila siku na pia kujipaka mafuta yake kifuani na kooni kabla ya kulala kila siku.

Kidonda
Atayachanganya matone kumi ya mafuta ya Habbat-Sawdaa, katika kikombe cha asali na kijiko kimoja cha maganda ya komamanga yaliyokaushwa na kusagwa. Atakula kila siku kabla ya kula chakula; baadae atakunywa gilasi ya maziwa yasiyotiwa chochote.

Saratani (Cancer)
Atapaka mafuta ya Habbat-Sawdaa mara tatu kila siku na kula kijiko cha unga wake kila amalizapo kula katika kikombe cha juisi ya karoti. Ataendelea hivyo kwa muda wa miezi mitatu.

Nguvu Za Kiume
Atachukua  unga wa Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kimoja achanganye (apige) ndani ya mayai saba ya kienyeji; atafanya hivyo siku baada siku kwa muda wa mwezi mmoja. Basi hata kama ana miaka 120 atapata nguvu za barobaro!

Udhaifu kwa Ujumla
Atachukua unga wa habat soda kiasi cha kikombe kimoja, uwatu mfano wake na ambari (ambergris) ilioyeyushwa kiasi cha kijiko kidogo, vyote atavichanganya katika chombo chenye asali iwe kama jamu; halafu awe akila kama jamu kila siku na wakati wowote apendao lakini kwa mkate wa ngano asili.
Kuleta Hamu Ya Kula
Kabla ya kuanza kula, jipatie Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kidogo na uitafune kwa meno yako, na unywe maji ya kawaida yaliochanganywa na siki kidogo.

Kutibu Ulegevu Na Uvivu
Atakunywa- kabla ya kula – juisi ya machungwa iliochanganywa matone kumi ya mafuta ya Habbat-Sawdaa. Ataendelea hivyo kwa muda wa siku kumi.  Baada ya hapo ataona nishati na uchangamfu.

Nishati akilini Na Wepesi Wa Kuhifadhi
Atachemsha nanaa (mint leaf), aichanganye na asali na aingize matone saba ya mafuta ya Habbat-Sawdaa; anywe kinywaji hiki kikiwa na vuguvugu wakati wowote apendao. Basi ataionea namna fahamu itakavofanya kazi.