Saturday 27 September 2014

NAMNA YA KUISHUGHULIKIA NA KUISHINDA HOFU-3-4



Usijiogopeshe kwa vitu ambavyo hutokea kwa nadra sana.
Njia bora ya kuyatengeneza mawazo yetu yanayofikiri sana juu ya hatari ambazo hutokea kwa nadra sana ni kwa kuwaza kuwa wewe hautakuwepo pale hatari hiyo itakapo tokea katika eneo hilo, na hivyo haitakuathiri.

Kwanini uwaze kwamba wewe una bahati mbaya sana na vyote vibaya vitakapotokea vitakukuta wewe tu. Najua inawezekama kabisa lakini nafasi za kuwezekana huko ni ndogo sana. Mfano. Kwanini uwaze kuwa unapotembea msituni peke yako, mti unaweza kukuangukia. 

Au unapokuwa kwenye ndege au meli, ajali yaweza kutokea, au hata unapokuwa safarini kwa gari, jiulize mabasi mangapi yametoka kule unakotokea na kufika salama kule unakokwenda bila shida yoyote, wewe je huwezi kuwa mmoja wa waliokuwa salama?
Kuna mambo mengi ya kuogopesha yanayotokea katika maisha yetu ya kila siku, na kama ukiogopa na kuhofu kila kitu na kutofuata ushauri unaotolewa hapa, basi kila siku utatembea na kuishi kwa hofu tu.

Usiwaze sana juu ya matukio yasiyoweza kuepukika
Yako matukio katika maisha ambayo kamwe hatuwezi kuyaepuka. Matukio haya yanakuja katika maisha yetu, yanapita na kusahaulika. Kitu cha muhimu ni kuishi maisha yako vema na kiusalama zaidi ili usijiweke katika hatari za kiafya na taratibu ukijiandaa kiuchumi na kijamii kwa uzee ulioko mbele yako.

Pia usisahu kutenda mema na kuishi sawa sawa na imani yako inavyokutaka ili uweze kupata maisha mema tena baada ya haya ikiwa unaamini hivyo.

Baada ya kufanya maamuzi haya usiweke sana mawazo yako kwenye mambo yanayohusiana na uzee, kustaafu au kifo. Acha mawazo au fikra hizo zielee zenyewe tu akilini mwako pasipo kuanza kuzichambua kwa kina.

Amua nini utakifanya pale vile unavyo viwazia sana na kuvihofu vitakapotokea
Kama unaona ni kazi ngumu kutowazia sana mawazo ya vile unavyovihofia, na unashindwa kujisahaulisha akilini mwako, basi pata muda wa kuvichambua kwa kina. 

Kwa asili, woga kututisha pale tunapojaribu kuwaza kuhusu mwisho au hatima ya baadhi ya mambo au matukio fulani, kwahivyo jaribu kufikiria nini utafanya pale ambapo hofu zako zitakapotokea. 

Kwakufanya hivi utaona kuwa pale vile unavyovihofia vinapotokea, basi maisha yataendelea kama kawaida, na mambo yatakuwa ya tofauti na vile yalivyo sasa.

Kama unadhani kuna tahadhari ya kuchukua au maandalizi ya kufanya katika vile unavyovihofia basi fanya hivyo kwa umakini mkubwa na mengine yote umwachie Mungu. Baada ya kufanya hili utaona dhahiri kuwa hofu na woga ulionao haukutesi tena.

Wacha kulilia maziwa yaliyokwisha kumwagika
Ni kawaida kulia pale unapopoteza kile ulichokithamini au kukipenda, au pale kile ulichokiwekea jitihada kisipoleta matokeo uliyoyadhania. Hata hivyo, huna haja ya kujiumiza kichwa wala moyo, maana hutobadili chochote kwa yaliyokwisha kutokea. Usiweke mawazo sana katika vile ulivyopoteza au kuvipatia hasara. Ni kweli kwamba yamkini maisha yangekuwa bora zaidi kama kile au vile ulivyopoteza visingepotea, lakini pia hakuna mwenye uhakika na hili. 

NAMNA YA KUISHUGHULIKIA NA KUISHINDA HOFU-4

0 comments:

Post a Comment