Wednesday, 7 May 2014

DAWA YA MARADHI YA AMOEBA



WATU wengi

wamekuwa wakisumbuliwa na ugonjwa wa Amoeba lakini hupuuzia pale dalili zinapoanza, ni ugonjwa mbaya ambao ukikaa sana

tumboni husababisha madhara makubwa , kama kuhara damu kupindukia, kutapika, kusikia kizunguzungu, kukosa hamu ya kula na kupata homa kali.

Ugonjwa huu mara nyingi husababishwa na maji na vyakula jamii ya mbogamboga kama hutakuwa umesafisha vizuri.

Dalili za ugonjwa

ni pamoja na tumbo kujaa na kukata kwa vipindi fulani, mtu akienda kujisaidia mara nyingi huishia kujikamua sana na akipata choo huwa hajisikii kumaliza.

Hizo ni baadhi ya dalili ila zipo nyingi lakini usitumie dawa mpaka utakapogundua kwa kupima kwani dawa nzuri inanywewa pale mtu anapogundua ana tatizo gani.
Tiba asilia ya Amoeba

Majani ya mpera


Tiba asilia inayotumika kumaliza kabisa tatizo hili ni pamoja na majani ya mpera, unayachukua na kuyakamua kwenye maji masafi ya kunywa ukiwa umeshayaosha vizuri kisha unakunywa nusu kikombe kwa siku mara tatu kwa siku tatu mfululizo.
Kitunguu swaumu

Chukua kitunguu swaumu punje tano menya kisha viweke ndani ya nusu lita ya maji safi na salama, changanya na maji ya limao moja chemsha mpaka maji yapungue, usisahau kuweka chumvi kidogo kwa ajili ya kupata ladha.

Ukishatengeneza kinywaji hicho unaweza kunywa kila siku glasi moja.
Ni tiba nzuri isiyo na madhara kwa mgonjwa.


Related Posts:

  • JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA PUMU (ASTHMA) JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA PUMU Mahitaji:   Karafuu 6  Karafuu  Maandalizi: Zitowe vichwa vyake kisha loweka hizo karafuu katika nusu gilasi ya maji usiku kucha   Matumizi: &nbs… Read More
  • PILIPILI HUIMARISHA UJASIRI NA NGUVU MWILINI! Kama ilivyo kwa matunda na vyakula vingine kuwa na faida kiafya mwilini, pilipili nayo ni moja wapo. Licha ya kuogopwa na baadhi ya watu, lakini ina kiasi kingi cha vitamin C. Umuhimu wa Vitamin C mwilini,  … Read More
  • ZIJUE FAIDA TISA ZA MBEGU ZA MABOGA Unaweza kuzidharau mbegu za maboga, lakini ni miongoni mwa mbegu zenye faida kubwa mwilini, zinazoweza kuzuia na kutibu hata magonjwa hatari yaliyoshindikana hospitalini. Kwa mujibu wa utafiti wa kisayansi uliok… Read More
  • MAAJABU YA KARAFUU (SYZYGIUM AROMATICUM) KUTIBU MAGONJWA MBALIMBALI. ​ Karafuu pamoja na Unga wa karafuu Karafuu ni tumba lililokauka la maua yasiyofunguka yanayopatikana kutoka mti mzuri wa kati na kijani. Mti huu una shina lilinyooka na hukua kufikia kimo cha mita 10 hadi 1… Read More
  • TIBA ASILIA YA TUMBO Watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa na tumbo lisilo la vidonda wala ugonjwa wowote ila utasikia anakwambia tumbo linanikata, huenda akawa anavurugikwa na tumbo au imetokea linasumbua tu. Tiba hii hapa Kwanza k… Read More

10 comments:

  1. POLE NA KAZI. SAMAHANI NAOMBA KUIFAHAMU DAWA YA ASILI NA YENYE UWEZO WA KUTIBU NA KUMALIZA UGONJWA WA "Urinary Track Infections" (U.T.I) Ahsante

    ReplyDelete
    Replies
    1. Dawa ninayo Nitafute nipate kukutibia.Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu. Au bonyeza hapa.https://www.facebook.com/mzizi.mkavu

      Delete
    2. Call dawa ipo kwa namba 0754948109

      Delete
  2. Hayo majani ya mpera kwa tiba ya amiba unayasga kwenye Brenda kwanza ili kuyakamua maji au unayachemsha?

    ReplyDelete
  3. Kama utaweza kuyasaga kwenye mashine ya blenda hayo majani ya mpera utaweka glasi 1 ya maji utasaga pamoja na kuyachuja na kuyanywa pasipo na kuyachemsha.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Je ayo majani ya mpera yawe kiasi gani. Na yale mateke au yaliyo komaa!

      Delete
    2. Je, amoeba inaweza sababisha maumivu ya kiuno kwa muda mrefu

      Delete
  4. Asante kiongozi,je kwa mtu ambae anashida ya homa ya ini anawezatumia hii dawa isilete madhara yaani hii ya kitunguu swaumu na limao katika kutibu amoeba?

    ReplyDelete
  5. Nikichemsha majani ya mpera je aiwezi saidia kutibu amoeba ?

    ReplyDelete
  6. Naomba kufahamu juu ya tiba ya amoeba kwa kutumia vitunguu saum kama ulivyoelekeza hapo juu.Swali langu kuwa,nshitsjika kutumia glass moja kwa muda wa siku ngp?Na swali la pili Imeelekezwa nusu lita msji ichangsnywe na punje tano za kitunguu,Ichemshwe hadi ipungue then ichanganywe na chumvi au asali kuleta Radha,swali lng hapo siitskuwa imebaki kama glass mbili tu ndio itakuwa dose kamili hiyo??

    ReplyDelete