Thursday, 8 May 2014
MAAMBUKIZI KATIKA VIUNGO VYA UZAZI (PID)
TATIZO hili kwa kirefu huitwa ‘Pelvic Inflammatory Diseases’.
Katika hali hii mwanamke hupata maambukizi kwenye viungo vya uzazi vya ndani zaidi ambavyo ni mirija ya mayai na vifuko vya mayai. Maambukizi haya pia husababisha majipu ya ndani kwa ndani kutokea.
Mwanamke mwenye tatizo hili hulalamika maumivu ya chini ya tumbo yanayosambaa kulia na kushoto, kutokwa na majimaji ukeni yanayoambatana na harufu na muwasho, damu kutoka bila mpangilio.
Tatizo hili likiendelea kwa muda mrefu husababisha ugumba, maumivu sugu ya tumbo chini ya kitovu na kupata mimba nje ya kizazi.
CHANZO CHA TATIZO
Maambukizi katika viungo vya uzazi vya mwanamke ‘PID’ husababishwa na bakteria ambao husambaa kutoka ukeni, huenda hadi ndani ya kuta za ndani za kizazi, kwenye mirija na hadi nje ya kizazi na mirija na husababisha atokwe na uchafu mzito unaotoa harufu mbaya .
Maambukizi katika mirija ya mayai huitwa ‘Salpingitis’ na katika vifuko vya mayai huitwa ‘Oophoritis’.
Matatizo yote haya
hutokea pamoja na kusababisha tatizo hili la ‘PID’ kwa hiyo mwanamke akipewa majibu kwamba ana ‘PID’ maana yake ameshambuliwa katika maeneo yote hapo juu.
Bakteria wanaosababisha tatizo hili ni Neisseria gonorrhea na Chlamydia Trachomatis. Bakteria hawa husambazwa kwa njia ya ngono.
Vilevile husambazwa au kutokea kutokana na maambukizi mengine ya ukeni na ndani ya kizazi mfano baada ya kuharibika au kutoa mimba na maambukizi sugu ya ukeni.
PID hutokea kwa wanawake
walio na umri wa chini ya miaka 35. Huwa haitokei kabla ya kuvunja ungo. Hutokea baada ya kuvunja ungo. Pia tatizo hili la PID halitokei wakati wa ujauzito au mama anapokoma hedhi.
Mwanamke ambaye tayari ameshawahi kuugua ugonjwa huu yupo katika hatari ya kurudiwa tena na tatizo hili endapo tiba haitakuwa makini na ndiyo
Maana baadhi ya wanawake
hulalamikia maumivu ya mara kwa mara ya tumbo chini ya kitovu na kutibiwa mara nyingi bila mafanikio.
Wengine walio katika hatari ya kupata PID ni wale walio katika kipato cha chini wanaoshindwa kumudu gharama za tiba, wanawake wanaoshirikiana kingono na wanaume zaidi ya mmoja na wale ambao wamepata magonjwa ya zinaa.
DALILI ZA UGONJWA
Mwanamke mwenye tatizo la PID hulalamika maumivu ya mara kwa mara ya tumbo chini ya kitovu ambayo wakati mwingine hutibu na kujirudia, hujihisi homa mara kwa mara hasa nyakati za jioni, hutokwa na uchafu ukeni wenye muwasho na kutoa harufu na huwa na rangi ya njano kiasi au rangi ya udongo.
Mwanamke mwenye tatizo hili pia hupata damu ya hedhi bila ya mpangilio wakati mwingine damu hutoka kabla ya tarehe au baada ya tarehe ya kupata hedhi. Hupata maumivu wakati wa tendo la ndoa. Mlango wa kizazi huvimba ambapo anapojisafisha huhisi kizazi kimeshuka kwa kugusa kitu kama gololi ndani ya uke. Maumivu ya chini ya tumbo husambaa kulia na kushoto ya nyonga.
UCHUNGUZI
Vipimo mbalimbali hufanyika kutegemea na hali ya ugonjwa wa mwanamke. Vipimo vya mkojo, damu, Ultrasound na kipimo cha kuangalia ukeni na kuchukua majimaji au uchafu huo kwa ajili ya kupima maabara hufanyika.
USHAURI NA TIBA
Ni vema mwanamke mwenye tatizo hili awahi katika kituo cha afya cha jirani kwa uchunguzi wa awali pia ni vema uwaone madaktari katika hospitali za mikoa kwa uchunguzi wa kina.
Related Posts:
TAMBUA AINA TOFAUTI ZA UVIMBE KWENYE KIZAZI CHA MWANAMKE KATIKA makala haya nitachambua aina tofauti za uvimbe kwenye kizazi cha mwanamke, dalili zake, vyanzo, athari na jinsi ya kujitibu kiasili na pia jinsi ya kuishi ili kuepuka tatizo hili ambalo mara nyingi hus… Read More
MAUMIVU CHINI YA TUMBO Tatizo la maumivu chini ya tumbo huwasumbua baadhi ya wanawake huku vyanzo halisi vya maumivu vikiwa vingi tu. Maumivu chini ya tumbo au chini ya kitovu huweza kusababishwa na mambo mbalimbali kama tutakavyoona. Maum… Read More
TAMBUA AINA TOFAUTI ZA UVIMBE KWENYE KIZAZI CHA MWANAMKE-2 Mada iliyopita nilianza kujadili mada inayohusu aina tofauti za uvimbe kwenye kizazi cha mwanamke. Nilianza na aina ya kwanza kuwa ni fibroid (s ), yaani uvimbe kwenye mji wa mimba. Nilieleza dalili zake ni hedhi … Read More
MADAWA YA KUONGEZA UCHUNGU WAKATI WA KUJIFUNGUA YANAWEZA KUSABABISHA UGONJWA WA AKILI KWA WATOTO (AUTISM) Utafiti wa watoto 625,000 uliochapishwa kwenye jarida JAMA pediatrics nchini Marekani umebaini kwamba watoto ambao mama zao walitumia madawa ya kuongeza uchungu/kusaidia uzazi wakati wa kujifungua wako hatarini kup… Read More
KIUNGULIA NA GAS KWA AKINA MAMA WAJA WAZITO Kila ujauzito uko tofauti lakini kuna baadhi ya vitu ambavyo wanawake wengi huwa wanaexperience katika ujauzito wao hivi ni pamoja na kiungulia(Heartburn) na kusikia gesi tumboni. Leo tutaongelea jinsi ya kuepukana … Read More
0 comments:
Post a Comment