Tuesday 15 May 2018

UGONJWA WA PRESHA KUTOKANA NA UMRI WAKO.(BLOOD PRESSURE CHART BY AGE)





Presha ya kawaida isiwe zaidi ya 140/90mmlHg. 
Presha ikiwa haitibiwi huharibu mishipa ya damu katika macho, misuli ya moyo kuwa minene , kusababisha mshutuko wa moyo (heart attack), mshipa ya damu safi kuwa migumu, figo kushindwa kufanya kazi (kidney failure) na kiharusi (stroke). 
Presha kwa mwanamke mjamzito inaweza kusababisha kifafa cha mimba na kufanya hata kiumbe kufa tumboni. Hivyo ni muhimu kuchunguza presha ya wanawake wote wajawazito.

Visababishi vya presha kuwa juu 


Chumvi nyingi
Unene uliozidi
Umri mkubwa au uzee
Figo ikiwa haifanyi kazi
Historia ya ugonjwa wapresha kwenye familia
Ugonjwa wa kisukari
Dalili ya mtu mwenye ugonjwa wa presha
Mara nyingi presha haina dalili hadi ilete madhara na hivyo huitwa( silent killer ) muuaji wa kimyakimya 


kichwa kuuma
kizunguzungu
kubanwa na pumzi
kutokuona vizuri
kichevuchevu

Vitu vinavyo changia hali presha kuwa mbaya zaidi ni


Kula chumvi nyingi
Unene uliozidi
Kutofanya mazoezi mara kwa mara
Kunywa pombe nyingi
Uvutaji wa sigara
Tiba ya ugonjwa wa presha


Mojawapo ya tiba ya presha ni kuacha vyakula vyenye chumvi kabisa kama itatumika iweke kidogo ya ladha wakati chukula kipo jikoni.
Pia mazoezi kwa ajili ya kupunguza uzito ni muhimu kwa tiba ya ugonjwa wa presha. Jitahidi kutenga mda wa mazoezi angalau dakika 30-60 mara tatu kwa wiki.
Epuka vyakula vyenye mafuta na lehemu maana vinaganda kwenye mishipa ya damu na kusababisha presha.
Daktari atakapo baini kuwa presha yako ipo juu, kulingana na aina na kiwango cha presha atakushauri kuhusiana na vyakula na jinsi ya kubadili mwenendo wa maisha au atakuanzishia dawa mara moja. Ni muhimu uelewe kuwa utakao anzishiwa dawa hutakiwi kuziacha maisha yako yote vinginevyo hali ya presha itarudi kama mwanzo.

2 comments:

  1. Very significant Information for us, I have think the representation of this Information is actually superb one. This is my first visit to your site. Men's Health Clinic

    ReplyDelete
    Replies
    1. I am FRED and i want quickly recommend DR NCUBE for a Job well done by
      curing me from the genital herpes disease that have be giving me sleepless night. if you want to contact him, Simply do that via email drncube03@gmail.com or 
      call/whatsapp +2348155227532
      he also have #herbs for
      #hiv/aids
      #cancerdisease 
      #fibroid 
      #diabetes

      Delete