Friday 20 May 2016

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA NYANYA....



FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA NYANYA....
Hili ni tunda mashuhuri na lenye virutubisho ambalo kwa kawaida hutumika kama mbogamboga. Kwa wastani, watu hula takribani kilo 8 za nyanya kwa mwaka.


Nyanya zina aina mbalimbali za viasili vya kurutubisha na visivyorutubisha vinavyohusiana na faida kadha wa 
kadha za kiafya. Hii inajumuisha lycopene, vitamini C, 

A na K, potasiamu, na nyuzinyuzi.

Nyanya moja yenye ukubwa wa wastani inaweza 

kutoa takribani nusu ya kiasi cha kila siku cha vitamini 

C anachohitajika kupata mtu. Viasili mbalimbali vya 

nyanya vinasadikika kufanya kazi pamoja kuleta 

manufaa ya kiafya.

Hii ni pamoja na kusaidia kujenga afya ya meno, afya 

ya mifupa, afya ya ngozi, afya ya nywele, kupunguza 

shinikizo la damu (PB) na kupunguza viwango vya 

lehemu pamoja na kupunguza hatari ya ugonjwa wa

moyo na saratani.

Baadhi ya vionjo vya nyanya kama vile lycopene 

hufyonzwa kwa wepesi mwilini pale nyanya 

zinapochemshwa, iwe kwa kuzipika au kuzichemsha.

Sasa huenda tunazijua faida za kula lishe kamili ya 

kuleta afya ikiwa ni pamoja na kula matunda na 

mbogamboga. Lakini wasichokijua watu wengi ni 

kwamba juisi ya mbogamboga ndiyo inayosaidia 

kudumisha urari (pH) muhimu wa haidrojeni ya mwili.

pH ina maana ya nguvu ya haidrojeni katika mizani ya 

kupimia hali-asidi ya vitu mwilini. Ili mwili ufanye kazi 

vizuri na kuweza kuendelea kuishi, lazima uwe na 

vikemikali vinavyolipuka na vitu vya asidi ili 

kutengeneza chumvi na kutoa umajimaji wenye nguvu 

ya haidrojeni (ya baina ya 7 na 7.5) na uwe na kipimo 

cha haidrojeni chenye urari kamili kwa sababu saba:

1. Kuulinda mwili dhidi ya uharibifu utokanao na 

chembechembe za maradhi na kuukinga na uzee wa 

kabla ya wakati.

2. Kuusaidia mwili kudumisha viwango vya lehemu 

vyenye kuleta afya bora.

3. Kuweka msukumo wa damu katika kiwango bora cha afya.

4. Kuweka katika hali ya kawaida kikemikali cha 

kusawazisha sukari ya damu (insulin) na kuzuia 

ongezeko la uzito wa mwili linaloweza kuhatarisha afya.

5. Kuuwezesha moyo kufanya kazi vizuri.

6. Kuongeza uzalishaji wa nishati

7. Kudumisha mfumo wa kinga ya mwili, mfumo wa 

umeng’enyaji, kudumisha afya ya viungo vya mwili na mifupa

0 comments:

Post a Comment