Sunday 15 May 2016

FAIDA YA MBEGU ZA TIKITIMAJI





Faida ya kutafuna mbegu za tikiti maji

TIKITI MAJI ni moja ya matunda yanayolimwa sana 

katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania tofauti na miaka iliyopita.

Hii inaashiria kwamba tunda la tikiti maji linaliwa 

sana katika maeneo hayo kutokana na faida 

inayopatikana kwenye tunda hilo.

Pamoja na kuongezeka kuliwa kwa tunda la tikiti maji 

lakini wengi wa wateja wanaokula tunda hilo huwa 

hawajui faida ya mbegu za tunda hilo.

Kutokana hali hiyo wengi wanaokula tikiti maji 

wanatema mbegu hizo na huenda wengi walikuwa na 

imani potofu inayokataza kula mbegu za tunda.

Hivyo badala ya kuzitafuna mbegu hizo wengi 

huzitema na kuona ni kitu kisicho na faida yoyote 

katika mwili wa binadamu.

Lakini mbegu hizo zinatakiwa kutafunwa wakati 

unapokula tunda lenyewe na hii ni kutokana na faida zake kiafya.

Unapokula tunda la tikiti maji unachotakiwa kufanya ni 

kuzitoa mbegu zake na kuziweka kwenye chombo 

kimoja mpaka zichipue yaani kuanza kutoa mizizi.

Baada ya hapo unatakiwa uzikaushe tayari kwa 

kuzitumia kutoka na faida hizi zifuatazo:

Mbegu za tikiti maji zina protini nyingi hivyo kuzitafuna 

kunaweza kumpatia mlaji chanzo cha protini.

Pia aunzi mmoja tu (takriban ujazo wa 1/8 wa 

kikombe) inakupa virubutisho vya protini vya gramu 10.

Hii ni sawa sawa na kiwango kinachopatikana kutoka 

katika yogati ya Kigiriki wakati wa kustaftahi.

Mbegu ‘zilizochipua’ zimemea na mara nyingi zina 

virutubisho vya hali ya juu kuliko zile ambazo hazichipua.

Kuchipua kunaondoa mchanganyiko katika chakula 

ambacho husababisha ugumu wa kufyonza 

virutubisho vyote.

Mbegu za tikiti maji zilizochipua zikitafunwa huongeza 

msongamano wa virutubisho na kusababisha urahisi 

kumeng’enya chakula.

Kuhusu tikitimaji, mbegu hutolewa ngozi nyeusi ya juu 

na kubaki ikifanana na mbegu zilivyo.

Katika mbegu za zamani hili halipatikana lakini 

umegundulika kwamba kweli mbegu hizi zinaleta afya kwenye mlo.

Mbegu za tikiti maji zilizochepua zina protini, vitamin B, 

Magnesia, na mafuta ambayo hayakoleza.

Wataalamu wa masuala ya chakula wanasema 

mafuta yaliyokolezwa mara nyingi hayana viwango vya 

lehemu na muasho na yanaondoa hatari ya kupata 

ugonjwa wa moyo na kiharusi.

Kama umeshawahi kutafuna mbegu za matikiti maji 

wakati ukila tunda hilo uligundua ladha yake ni sawa

na tunda lenyewe.

Mbegu za matikiti maji ni sawa na mbegu za alizeti 

kwa ladha, lakini haina lozi kubwa.

Zinakuwa na ladha nzuri zaidi zikiwa kwenye 

kachumbari, iliyochanganywa pamoja au ukiila ikiwa mkononi mwako.

Jungu na mbegu nyingi ni nzuri kwa mwili wa 

mwanadamu, lakini ukilinganisha ukubwa wa lishe 

unaopatikana basi mbegu za matikiti maji zinaongoza.

0 comments:

Post a Comment