Monday 22 June 2015

(Colon Cancer) SARATANI YA UTUMBO MPANA NI HATARI





SARATANI YA UTUMBO MPANA NI HATARI


Habari wadau,
Mnaweza shangaa leo kuja na uzi huu wa Saratani ya Utumbo mpana, kifupi mi si tatbibu na wala sina fani yoyote ya namna hiyo, bali mambo haya yakikukuta ndo utayajua, sometime kuliko daktari mwenyewe, hasa ukiwa mtafiti wa kwanini nimepata tatizo hili ama lile, yalinikuta, haikufika kuwa saratani, labda kwa kuwa Mungu hakutaka ifike huko, lakini cha moto nimekiona, hivyo nimeona bora tuelimishane kupitia blog hii ili sote tuwe na tahadhari ya aina fulani hasa kuhusiana na magonjwa haya ya kujitakia, ndio ni ya kujitakia, yanaitwa Lifestyle Diseases ama magonjwa yasababishwayo na mitindo yetu ya maisha. 

"What you eat may play a role in your risk of colon cancer. Colon cancer may be associated with a high-fat, low-fiber diet and red meat. However, some studies have found that the risk does not drop if you switch to a high-fiber diet, so this link is not yet clear.

        


Smoking cigarettes and drinking alcohol are other risk factors for colorectal cancer." kwa mujibu wa U.S National Library of Medicine

Ndio maana nikasema ni ya kujitakia, tafiti zaonesha "90% of chronic diseases come from infection of gastrointestinal" 
na sababu kuu ni tatizo la kukosa choo, mi nilikuwa najiona sawa tu kama sijaenda haja siku moja au mbili, nikidhani ni kawaida, kumbe nilikuwa nalundika matatizo, mtu yeyote ambaye anapata mlo walau mlo mmoja kwa siku na kupitisha siku moja au zaidi bila kupata choo anatatizo la kukosa choo, sasa je weye unaye pata milo mitatu kwa siku bila kutoa uchafu huo je wadhani waenda wapi? kitaalumu tatizo hili lajulikana kama Constipation. 


Wataalamu wanasema sababu ziko nyingi ikiwa ni pamoja na:-

Kukosa mlo kamili ama kula vyakula viingi vyenye kiwango kikubwa cha wanga na mafuta,
Kula vyakula vilivyokobolewa na vilivyo changanywa na madawa ili visiharibike,
mifumo hatarishi ya maisha (Dangeraous Lifestyles) kama vile matumizi ya pombe na sigara kwa wingi,
Ukosefu wa kiwango cha kutosha cha mbogamboga na matunda katika milo yetu,
Maji yasiyo salama,
Kuvuta hewa chafu,


Hizi ni baadhi tu, na hadhari zake zaweza kuwa:-




Chakula kutomeng'enywa vizuri (poor function of digestion system)
Maumivi makali wakati wa kupata choo,
Uchafu uliokaa muda mrefu kugeuka sumu,
Bakteria wenye madhara kuzaliwa na kuathiri utumbo mpana na viungo vingine mwilini.


Hii yaweza sababisha magonjwa sugu kama:
Saratani ya utumbo mpana (Colon Cancer)
Presha (Arteriosclerisis)
Kuongezeka uzito (Obesity)
Tumbo kujaa gesi
Magonjwa ya Ini
Figo kushindwa kufanya kazi vizuri,
Magonjwa ya ngozi,
Kukakamaa kwa mishipa ya damu,
Kisukari,
Magonjwa ya moyo n.k

1 comments:

  1. Thanks for this. I really like what you've posted here and wish you the best of luck with this blog and thanks for sharing. IUD Malaysia

    ReplyDelete