Monday 3 November 2014

SABABU ZA TATIZO LA KUTOPATA MIMBA - 3



Kipimo cha upevushaji wa mayai kupima mirija ya uzazi, upasuaji mdogo kwenye tumbo na kumulika ndani ya mwili wake pia kipimo cha Ultrasound kitafanyika.
Vipimo kwa upande wa wanaume
Baada ya kuchukuwa historia  ya mgonjwa kwa urefu  kinachofuata ni vipimo vya kuangalia kama yupo kawaida  au kama kuna hitilafu. Vipimo hivyo ni kumchunguza  mwanaume kwa ujumla hali ya afya yake kwa kumpima kuanzia kichwani hadi miguuni.
Kupima mbegu zake,  kupima vichocheo vyake vya uzazi, kupima na Ultrasound kwenye korodani zake.
Ushauri 
Muda wa kufanya   Mwanamke anashauriwa kulalia mgongo huku ameinua magoti baada ya kufanya tendo la ndoa kwa muda wa dakika 20.
Kutotumia mafuta yoyote ya kulainisha uke kwani baadhi ya mafuta huua mbegu za kiume.
Kuacha kuvuta sigara kwa mwanaume na mwanamke  kwani uchunguzi huonyesha  kuwa uvutaji wa sigara  unasababisha ugumba na utasa.
Kupunguza uzito kwa mwanamke na mwanaume na kutumia vidonge vya madini  ya foric acid kwa ushauri wa daktari kumeonyesha msaada mkubwa kwa akina mama wanaopata shida ya kupata mimba.
Upimaji wa mbegu za kiume
Mbegu za kiume baada ya kutolewa zinatakiwa kufikishwa maabara kabla ya dakika 30 kwa upimaji.
Mwanaume anashauriwa kukaa siku 3 bila kufanya tendo la ndoa ndipo atoe mbegu zake. Ujazo au wingi wa mbegu kawaida ziwe zaidi ya milioni mbili. Kwa kawaida wingi wa mbegu ni zaidi ya milioni 25.

0 comments:

Post a Comment