Monday 3 November 2014

FANYA MAMBO 5 ILI UWEZE KUJIKINGA NA MARADHI.



 1. Jitahidi kadiri uwezavyo kufanya mambo haya matatu: kula vizuri, kufanya mazoezi ya kutosha, na kupumzika vya kutosha.
 
 2. Dumisha usafi. Wataalamu wa afya husema kwamba kunawa mikono ndiyo njia bora ya kujikinga na magonjwa au kuepuka kueneza maambukizo.
 
 3. Hakikisha kwamba chakula mnachokula na familia yako ni salama. Hakikisha mikono yako na mahali unapotayarishia chakula ni safi. Pia, hakikisha kwamba unatumia maji safi kunawa mikono na kusafisha chakula. Kwa kuwa viini huzaana ndani ya chakula, pika nyama kabisa. Hifadhi vyakula vizuri.
 
 4. Katika maeneo ambayo magonjwa hatari huenezwa na wadudu wanaoruka, epuka kuwa nje usiku au mapema asubuhi wakati ambapo wadudu ni wengi. Jikinge kwa chandarua sikuzote.
 
 5. Kupata chanjo kunaweza kuimarisha mfumo wako wa kinga ili upambane na viini vinavyopatikana mahali unapoishi.

0 comments:

Post a Comment