Monday 3 November 2014

SABABU ZA TATIZO LA KUTOKUPATA MIMBA-2


Leo nitaelezea matibabu na ushauri kwa wanandoa wanaokabiliwa na tatizo la mama kutopata mimba.
Miongoni mwa mambo wanayopaswa kuelezwa  wanandoa hao ni kuwapa uzoefu kuhusiana na afya ya uzazi na jinsi ujauzito unavyoweza kupatikana na hatimaye kupata mtoto.
 Pia kuona jinsi ya  kuunganisha familia na kujenga familia bora kama itashindikana kupata mtoto bila mume kumtenga mke au mke kumtenga mume.
Kutumia muda mwingi wa kufuatilia kliniki bila kuchoka na kutumia kiasi cha muda wao kushughulikia uzazi.
Njia tofauti za matibabu (Fertility treatment options)
-Kuhakikisha mayai ya mwanamke yanapevuka.
-Kurekebisha mirija na matatizo ya mji wa mimba kama kuondoa uvimbe.
-Matibabu ya mwanaume mwenye matatizo ya mbegu.-Njia ya kupandikiza mbegu (Assisted reproductive technology).  Dawa zinazotumika kupevusha mayai ni kama Clomiphene citrate, letrozole, tamoxifen, progynora, Inj HCG inj, vaginal progesterone, Human menopausal gonadotropin, FSH, GN-RH, metformin, Bromocriptine, dawa hizi zinasaidia sana kurutubisha mayai bila kuleta madhara yoyote kwa mtumiaji, matatizo ambayo yanaweza kujitokeza ni kama kuzaa mapacha, wakati wa utumiaji wa dawa hizi ni lazima daktari awe mwangalifu wa kuangalia vipimo kama vile damu (vichocheo hormone) Ultrasound kuangalia kifuko cha mayai.
Njia nyingine zinazotumika katika matibabu ni njia ya upasuaji kama vile oparesheni ndogo tumboni kumlika uzazi (laporoscopic techniques).
Kifuko cha uzazi (ovaries) na kuchukua mbegu za mwanaume na kuziunganisha kwenye kifaa maalum (maabara hatimaye kuingiza kwenye mji wa mimba kwa kutumia vifaa maalum kama bomba la sindano.
Mama mhusika anayetakiwa kupandikiza ni lazima asiwe na umri usiozidi miaka 40.

0 comments:

Post a Comment