Friday, 4 July 2014

MARADHI YA UGONJWA WA KIMETA ( ANTHRAX)



Kimeta ni ugonjwa wa hatari unasababishwa na vimelea vya bacteria. Bacteria hawa hujulikana kama  Bacillus anthracis,bacteria ambao wana uwezo wa kufanya mbengu.Mbegu hizi ni seli ambazo huweza kukaa kwa miaka kadhaa (karne na  milenia) hata katika mazingira magumu zikiwa zimelala na huweza kurudia hali ya uhai pale zinapopata mazingira ya kufaa.


Maambukizi mengi yanayotokana na ugonjwa huu husababisha vifo. Ugonjwa huu unathiri binadamu pamoja na wanyama. Mbegu za ugonjwa huu huweza kuzalishwa katika maabara na kutimika kutengeneza silaha za kibiolojia

Kuna aina tatu za kimeta kulingana na eneo la mwili lililoathiriwa. Ugonjwa huu unaweza kuathiri ngonzi,mapafu na njia ya chakula.

Unapataje maambukizi?
Kimeta hakiambukizwi kati ya mtu na mtu

Kutoka kwa wanyama.
Binadamu huweza kupata maablmbukizi toka kwa wanyama iwapo watagusana na mazao ya wanyama waliothirika na ugonjwa huu au kuvuta mbegu au kula chakula ambacho hakikuva vizuri kutoka kwa mnyama alieathirika.

Kimeta kama silaha.Kimeta pia kimehusika j  ugaidi.Mwaka 2001 kimeta kilitumiwa nchini marekani na kusababisha vifo.Kutokana na ukweli kwamba kimeta huwezwa kuzalisha maabara ,imekuwa silaha ambaye imekuwa ikitumiwa na magaidi.

Hatari ya ugonjwa huu inategemea sehemu ilipoathirika. Maambukizi kwenye mapafu husababisha kifo kwa kiasi kikubwa.Maambukizi kwenye matumbo ni hatari pia kwani huweza kusabibisha vifo kwa nusu  wagonjwa waliopata maambukizi.Maambukizi ya ngozi hayasababishi vifo kwa kiasi kikubwa kwani asilimia 80 ya wagonjwa hupona hata bila kupata tiba yoyote.

Dalili za kimeta
Dalili hutofautiana hasa kulingana aina ya ugonjwa

Maambukizi ya ngozi: Dalili ya awali ni Kipele kidogo ambacho hufanya lenge. lengelenge hili baadae hufanya kidonda chenye weusi katikati.Vitu hivi vyote haviumi

Njia ya chakula: Dalili za awali ni Kichefuchefu,kukosa hamu ya chakula, Kuhara damu,homa ikifuatia na maumivu makali ya tumbo.

Njia ya hewa: Dalili za awali hujitokeza kama dalili za mafua, maumivu ya misuli,pamoja na homa. Baadae dalili zingine hujitokeza kama kikohozi, pumzi kubana na uchovu.

Dalili hujitokeza ndani ya siku saba tangu mgonjwa akutane na bacteria. Pia dalili baada ya kupata  maambukizi ya njia ya huweza kujitokeza ndani ya wiki moja au hata baada ya majuma sita.

Matibabu ya Kimeta
Antibiotics hutumika katika matibabu ya aina zote tatu za ugonjwa huu. Utambuzi wa awali pamoja na matibabu ni muhimu.

Kukinga baada ya kuambukizwa
Matibabu ni tofauti kwa mtu ambae amepata maambukizi ya kimeta lakini hajaanza kuugua. Wahudumu wa afya hutoa dawa za antibiotics mfano ciprofloxacin au doxycycline pamoja na chanjo.

Matibabu baada ya maambukizi
Treatment after infection.
Kwa kawaida matibabu huchukua siku 60. Mafanikio hutegemea aina ya ugonjwa na muda wa kuanza matibabu.

Kinga.
Kuna kinga ya kuzuia ugonjwa wa kimeta katika  nchi zilizo endelea lakini kwa sasa inatolewa kwa watu walioko kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi.

Related Posts:

  • (WARTS) MARADHI YA NGOZI KWA NJIA YA NGONO Baadhi ya maswali tuliyopokea, mengi yalihusu maradhi ya sunzua ambayo kitaalmu yanajulikana kama warts. Sunzua ni ugonjwa wa ngozi unaofahamika na wengi. Ugonjwa huu husababishwa na virusi ambavyo kitaalamu huitwa humanp… Read More
  • MAGONJWA YA FANGAZI SEHEMU ZA WAZI Eneo lenye maradhi pia hubadilika rangi na kuwa na rangi tofauti kidogo na rangi ya ngozi ya eneo ambalo halijaathirika na maambukizi. Kama mwendelezo wa makala yetu ya maradhi ya ngozi, tuendelee kuangalia maradhi ya n… Read More
  • UJUWE UGONJWA UITWAO MKANDA WA JESHI (HERPES ZOSTER/SHINGLES). Kwa takribani miongo mitatu sasa, tumeshuhudia ongezeko kubwa la mlipuko wa ugonjwa wa mkanda wa jeshi linaloendana na ongezeko la hususani ugonjwa wa UKIMWI. Hali hii imefanya baadhi ya watu kuamini kuwa, ugonjwa huu… Read More
  • KUTOKWA NA MAJIMAJI KWENYE MATITI (GALACTORRHEA) Tatizo hili husimama lenyewe kama ugonjwa ingawa pia inaweza kuwa ni dalili kama mwanamke ni mjamzito, ananyonyesha au ametoa mimba au ameharibikiwa na mimba.Kusimama kwake kama ugonjwa ni pale  yanapotoka wakati mwa… Read More
  • FUKUZA VIDONDA VYA TUMBO FANGASI NA MAPUNYE NI mpapai! Mara nyingi nimekuwa nikiongea kuwa Tanzania tuna miti mingi sana kiasi kwamba bado hata robo yake hatujaijua majina yake, achilia mbali kitu muhimu kama kujua matumizi. Mungu alipomuumba binadamu na… Read More

0 comments:

Post a Comment