Tuesday, 17 June 2014

SABABU 18 ZA KUPUNGUZA UZITO




sababu 18 zinazokulazimu upunguze uzito wako na uogope unene na zote ni hizi zifuatazo:
1. Unene unaongeza kiwango cha mafuta mwilini, ambayo huongeza uwezekano wa kupata kansa.
2. Unene unaongeza mafuta mwilini, ambayo hufanya matibabu ya kansa kuwa magumu zaidi.
3. Unene huongeza mafuta mwilini ambayo huushinikiza na kuubana moyo. 
4. Mtu mnene huwa mvivu kufanya mazoezi, suala ambalo humuongezea zaidi unene.
5. Mafuta mengi mwilini yana madhara kwa ubongo.
6.Unene huathiri hata tabia na miamala ya mtu.
7. Unene huongeza uzito katika mifupa na viunga vya mifupa (bone joints).
8. Unene husababisha kibofu cha mkojo kibanwe suala linalosababisha matatizo mbalimbali ya mkojo.
9. Unene hupunguza uwezo wa kujamiiana wa mtu.
10. Unene hupunguza uwezo wa kuzaa na hata kusababisha utasa na ugumba.
11. Unene huweza kuufanya mwili upatwe kwa wepesi magonjwa mbalimbali kama vile kisukari na presha.
12. Watu wanene wanapofika hospitalini upimaji wao pia huwa wa matatizo.
13. Unene husababisha ujauzito kuwa wenye matatizo mengi.
14. Unene huathiri pia afya ya mtoto mchanga anayezaliwa.
15. Unene hufanya matibabu ya pumu (asthma) yawe magumu.
16. Unene hupelekea mtu asilale vizuri na wakati mwingine mtu mnene anapolala hubanwa na pumzi suala linalomfanya aamke mara kwa mara.
17. Unene humfanya mtu ashindwe kuwajibika vizuri kazini na hata kuathiri utendaji kazi wake.
18. Unene hufanya matumizi ya fedha kuwa makubwa unapokumbwa na magonjwa yasababishwayo na unene.

Related Posts:

  • NANMA YA KUMSAIDIA MTU ALIYE UNGUWA NA MOTO Kuungua kwa watoto kwa moto ni moja ya ajali zinazotokea sana mara kwa mara na huwakuta wakiwa majumbani mwao. Asilimia 70 ya kuungua kwa watoto huwa ni wao wenyewe ndio hujitumbukiza katika ajali hi… Read More
  • MAMBO YANAYOHARIBU AFYA YAKO-2 Hali ya miili ya wanawakehutofautiana na wanaume na hatakazi na shughuli wanazozifanyapia huweza kuathiri afya zao kwaujumla. Kwa mfano, kubebamimba na kujifungua, kansa yaovari na kizazi huathiri afya yawanawake katika ha… Read More
  • VYAKULA VYA KUDHIBITI UGONJWA WA GAUTI (GOUT) Juisi za mboga na matundaMboga zina nafasi kubwa sana katika kupambana na maradhi yanayomkabili mwanadamu na huwa ndiyo kinga ya mwili wakati wote zinapotumiwa. Katika kutibu tatizo la Gauti, juisi ya mchanganyiko wa karo… Read More
  • MAMBO YANAYOHARIBU AFYA YAKO Mazingira ni jambo linginelinaloathiri afya. Iwapo majitunayokunywa na kutumia ni safina salama, iwapo hewatunayovuta si chafu, maeneotunayofanyia kazi ni salama na pianyumba tunazoishi, basi afya zetuhuwa salam… Read More
  • USINGIZI NI MUHIMU KWA USTAWI WA UBONGO WAKO Mwili wa mwanadamu unauhitaji usingizi ili uishi maisha marefu, ujengeke, upate hamu ya kula, kunywa na kuvuta hewa. Ogani kubwa za mwili kama vile moyo, figo, ini na mapafu hufanya kazi yake vizuri wakati mtu amelala. … Read More

0 comments:

Post a Comment