Sunday, 29 June 2014

MARADHI YANAYOMSIBU BINAADAMU NA TIBA YAKE: MARADHI YA VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS)





Maradhi ya VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS): Haya ni maradhi ambayo hufanya vidonda upande wa ndani ya ukuta wa tumbo. Kuna Duodenal ulcer na Gastric ulcer.
DALILI: (1) Kupata maumivu makali chini ya kifua kwa

upande wa ndani. (2) Kuchoka bila sababu. (3) Kuumwa kwa mgongo au kiuno. (4) Kupungua kwa nguvu za kiume. (5) Kuwa na kichefuchefu baadhi ya wakati. (6) Kuwa na kiungulia . (7) Tumbo kujaa gesi. (8) Tumbo kuwaka moto. (9) Kukosa choo na wakati mwingine kupata choo kigumu kama cha mbuzi. (10) Kukosa hamu ya kula. (11) Kutapika damu au wakati mwingine kutapika nyongo. (12) Maumivu makali baada ya kula vitu vikali au chakula cha moto.



TIBA: Kanuni ya kwanza: Chukua asali robo lita uchanganye na unga wa arki susi vijiko vinne vikubwa kisha ukoroge kwa kijiko. Chukua vijiko viwili vikubwa vya mchanganyiko huu ukoroge ndani ya kikombe cha maji ya moto. Yakishapoa unywe kikombe kimoja kutwa mara tatu.
Kanuni ya pili: Chukua viazi vya mviringo (vya chipsi) kama vitatu halafu uvikoshe na kuvimenya. Baada ya kuvimenya upate juisi yake kwa kuvisaga kwenye blenda. Kunywa vijiko vitatu vikubwa vya chakula kutwa mara mbili. 
Kanuni ya tatu: Chukua lozi gramu 30 halafu usage iwe unga.
Changanya lozi hii yote ndani ya kikombe kidogo cha maziwa ya moto kisha uongeze asali vijiko viwili vikubwa. Kunywa kikombe kimoja robo saa kabla ya kula chakula cha asubuhi. Fanya hivyo kwa muda wa mwezi na utapata shifaa.


Related Posts:

  • JUISI YA MATUNDA MCHANGANYIKO KAMA TIBA Katika ulimwengu wa vyakula, inafahamika na kuaminika kuwa chakula ni dawa. Chakula unachokula leo ndicho kinachoamua hali yako ya kiafya kesho. Unaweza kuishi bila kuugua kama ukila vyakula vyote muhimu vinavyohita… Read More
  • NAMNA YA KUDHIBITI MAUMIVU YA VIUNGO KIASILI ZAIDI KATIKA  makala yaliyopita nilipokea simu nyingi kutoka kwa wazee, wakilalamika na kuomba msaada wa tiba ya kupambana na tatizo la kuumwa viungo vya mwili. Lakini katika siku za hivi karibuni, siyo wazee tu, bali h… Read More
  • TIBA YA DAWA KUWA MACHO MEKUNDU TIBA(1) Weka macho yawe safi na uyakoshe kwa maji ya waridi kila wakati. Epusha macho kutokana na joto, baridi, moshi, vumbi, macho yasitumie nguvu sana kama vile kusoma sana. Tumia dawa za kulainisha choo ikiwa … Read More
  • MATIBABU YA CHUNUSI (TREATMENT OF ACNE) Lengo la tiba ya chunusi ni kupunguza uzalishaji wa mafuta ya sebum usoni pia kutibu vijidudu vya bakteria ambavyo hushambulia ngozi ya uso na kusababisha viupele vinavyowasha  na wakati mwingine kuleta maumivu usoni. … Read More
  • KUTIBU MARADHI YA MASIKIO Sikio (Ear) limegawika katika sehemu tatu kuu. Sehemu ya nje ya sikio, sehemu ya kati ya sikio na sehemu ya ndani ya sikio.   Kuna aina mbili ya matatizo ya masikio nayo ni:   i.    &n… Read More

0 comments:

Post a Comment