Saturday 14 June 2014

FAIDA 18 ZA KUTUMIA TUNDA LA MPAPAI KAMA NI DAWA NA CHAKULA.







Watu  wengi hulitumia  tunda la  papai  kwa sababu  ya utamu wake.
Hata  hivyo mbali  na  kuwa na  ladha  nzuri, tunda  la  papai lina  faida lukuki  kwa  afya  ya  mwanadamu.
  

UTAJIRI  WA  VITAMINI

Tunda la papai lina vitamini A,B,C,D, na E  jambo  linalo liweka  tunda  hili  katika  kundi  la  matunda  na  vyakula vyenye  utajiri  mkubwa  wa  vitamin.


Mti  wa  papai

FAIDA  ZA  KIAFYA  ZA  TUNDA  LA  PAPAI

Tunda  la  papai  lina  faida  nyingi  sana  kwa  afya  ya mwanadamu.   Miongoni  mwa  faida  hizo  ni  pamoja  na kuwa  na  uwezo  wa   :

 
Mbegu  za  Papai



1.            Kutibu   tatizo  la Shida ya kusaga chakula tumboni
2.          Kutibu   Udhaifu wa tumbo
3.          Kutibu  Kisukari na asthma au pumu.
4.          Kutibu  Kikohozi kitokacho mapafuni

Mizizi  Ya  Papai

5.          Kutibu  Kifua kikuu
6.          Tunda  hili  huleta  afya nzuri ukitumia kila siku
7.          Maziwa yanayotoka katika jani lake huponya vidonda
8.          Vilevile  yanasaidia  kutibu  sehemu palipoungua moto
9.          Kama  hiyo  haitoshi, maziwa  yanayotoka  katika jani  la  mpapai   yanatibu kiungulia  na  Ugonjwa wa colon (njia ya haja kubwa ndani)

Majani  Ya  Mpapai

10.       Pia  yanasaidia kutofunga choo
11.         Maganda ya  tunda  la  papai  yanasaidia  kutibu tatizo  la   kuungua, vipele  na  saratani  ya ngozi.

12.       Mbegu zake zinatibu ini zikitafunwa 10 – 12 kwa siku 5.

13.       Majani yake yakaushie ndani, yanatibu pumu. Inapoanza kubana yachome majani yaliyokaushwa kisha jifukize, kule kubanwa kutakisha.

14.       Majani yake yanasaidia  katika  kutibu  shinikizo la damu.

15.       Papai likimenywa na kupondwa linafaa Sana katika masuala  ya  urembo  kwani  linaweza kutumika Kama vile unavyotumia lotion kulainisha uso.

16.       Mbegu  za  papai  zina  uwezo  wa  kutibu  homa. Meza mbegu   za  papai  kiasi  cha  kijiko cha chakula mara 3 kwa  ajili  ya  kutibu  homa.

17.       Mbegu   za  papai zilizokaushwa ndani kisha zikasagwa kuwa unga zinatibu malaria, tumia kijiko 1 cha chai changanya na uji, kunywa mara 3 kwa siku 5 Mgonjwa wa kifua kikuu akila matunda haya kwa muda mrefu atapona bila dawa nyingine.

18.       Mizizi yake ikipondwa na kulowekwa katika maji yaliyochemshwa, lita 2 na nusu kwa dakika 15, yanatibu figo, bladder, yanazuia kutapika. Nusu kikombe cha chai kutwa mara 3 kwa siku 5.

0 comments:

Post a Comment