Monday, 5 May 2014

MATATIZO YANAYOAMBATANA NA UKOMO WA HEDHI



UKOMO wa hedhi, ni kipindi ambacho mwanamke anaacha kuziona siku zake kama ilivyokuwa tangu anavunja ungo. Kitaalamu, hiki ni kipindi ambacho mwili wa mwanamke unaacha kuzalisha homoni za Estrogen na Testosteron ambazo ndizo zifanyazo kazi ya kupevusha mayai kila mwezi.

Mwili unapoacha kuzalisha homoni hizi ambapo kwa wastani huwa ni katika umri wa kuanzia miaka 40- 45 (wengine wanaweza kuwahi au kuchelewa), kuna mabadiliko mengi yanayotokea kwenye mwili wa binadamu ambayo humsababishia mhusika matatizo mbalimbali ya kiafya.
Yafuatayo ni baadhi ya matatizo yanayowakumba sana wanawake waliofikia au wanaokaribia kufikia ukomo wa hedhi.

Kupoteza msisimko wa mapenzi

Hili ni tatizo linalowasumbua wanawake wengi hasa wale ambao wapo katika ndoa. Kutokana na mwili kuacha kuzalisha homoni za Estrogen na Testosteron, atika kipindi hiki, mwanamke hukosa kabisa msisimko wa kimapenzi hata kama mumewe atajitahidi kumuandaa kwa kiasi gani.
Wengine hufikia hatua ya kuwachukia waume zao, jambo ambalo kama hakuna mwenye uelewa wa kinachotokea, huweza kusababisha matatizo makubwa kwenye ndoa.

 Mabadiliko ya kihisia

Wanawake wengi husumbuliwa na tatizo la mabadiliko ya kihisia katika kipindi hiki. Wengi hupandwa na hasira  kwa urahisi, hushambuliw ana msongo wa mawazo, mwili huishiwa nguvu na wengine hukumbwa na tatizo la kutojiamini.
Katika hatua hii, inabidi kuwasaidia wahusika kwa kuwafundisha mbinu za kupambana na msongo na kudhibiti hasira pamoja na mbinu za kujiamini upya sambamba na mazoezi ya viungo.

 Kukosa usingizi

Tatizo lingine ni kukosa usingizi ambapo mwanamke hujikuta akishindwa kulala mpaka usiku wa manane au wakati mwingine mpaka alfajiri.

Related Posts:

  • KUTOKWA NA MAJIMAJI SEHEMU ZA SIRI Tatizo hili huwatokea wanawake na wanaume. Mwanaume hutokwa na majimaji katika njia ya mkojo, mwanamke hutokwa na majimaji haya katika njia ya mkojo au ukeni.Majimaji haya yanaweza kuwa mepesi au mazito, pia yanaweza kuwa… Read More
  • SABABU ZA TATIZO LA KUTOPATA MIMBA - 3 Naendelea kuelezea mambo yanayosababisha mwanamke kutopata mimba. Endelea... Kipimo cha upevushaji wa mayai kupima mirija ya uzazi, upasuaji mdogo kwenye tumbo na kumulika ndani ya mwili wake pia kipimo cha Ultrasound kit… Read More
  • MAGONJWA NYEMELEZI KWA WANAWAKE- 6 Ugonjwa huu huanza ghafla na dalili zake ni kama homa kali, kikohozi, maumivu wakati wa kupumua, baridi na kutetemeka. Ugonjwa wa Ngozi:Huu husababishwa na vimelea vya Staphylococcus aureus.Vimelea hivi huishi katika mw… Read More
  • SABABU ZA TATIZO LA KUTOPATA MIMBA - 2 Mpenzi msomaji, naendelea kuelezea sababu za mwanamke kutoweza kupata ujauzito. Tuwe pamoja...Wanaume wengi wanashindwa kumpa mimba mwanamke kutokana na kutumia dawa  hovyohovyo au kuwa na matatizo ya tezi za thyroid… Read More
  • MATATIZO YANAYOSABABISHA MWANAMKE ASISHIKE MIMBA MWANAMKE kutoshika mimba kumegawanyika katika makundi makubwa mawili. Kwanza ni hali iitwayo ‘primary Infertility’ ambapo mwanamke hana historia ya kupata ujauzito. Pili kuna hali iitwayo ‘Sekondari Infertility’, hapa m… Read More

0 comments:

Post a Comment