Monday 19 May 2014

MAPARACHICHI NA MAPAPAI: WAFALME WA MATUNDA …





Imekuwa kazi sana kupiga picha ya mseto huu mzuri na mtamu leo kabla ya kuushughulikia.
Afrika imejaaliwa mimea, madini, rutuba na hali ya hewa safi.
Takribani vyakula vyote tunavyohitaji wanadamu hupatikana bara hili. Lakini pamoja na hayo uhai wetu mfupi kuzidi wengine duniani. Kufuatana na orodha ya wastani wa maisha iliyotolewa na shirika la Ujasusi Marekani (CIA)na Umoja wa Mataifa mwaka 2011- nchi zinazoongoza kwa maisha marefu ni Japani na chini kabisa ni Afrika.
Machenza na Nanasi
Wajapani wanaishi hadi miaka 90 kuendelea , Ulaya, Marekani na China kati ya 75 hadi 90; nchi za bara Asia (mathalan India) miaka 65 kuendelea; mwisho ni Afrika yenye taifa la Angola mkiani (miaka 40). Tanzania imewekwa na wastani wa miaka 50 hadi 53.
Kombu la Kijapani
Msingi wa sababu zinazowafanya watu wasiishi muda mrefu ni maendeleo ya uchumi-jamii na siasa.
Lakini kiini cha wewe kuishi (mbali na elimu, makazi bora na furaha moyoni )ni CHAKULA BORA NA NAMNA UNAVYOKILA.

Wajapani mathalan wanasifika kwa kula vyema- hawali misosi mikubwa mikubwa kama sisi. Ulaji wao ni mdogo mdogo, wa mara kwa mara- hawajazi sana matumbo. Halafu kuna vitu wanavyokula ambavyo husaidia sana kukarabati na kuhifadhi mwili. Mfano mzuri ni mimea ya baharini. Kuna mmea uitwao Kombu ambao unauchemsha na kuyatumia maji yake kwa kupikia mchuzi, chai, nk. Moja ya faida ya “Kombu” ni kukinga na kuuponyesha mwili kutokana na maradhi; pili, kuongeza nguvu za nywele, ngozi na maisha kijumla. Ndiyo maana nadra sana kumwona Mjapani asiyekua na nywele nyingi, hata akiwa mzee- huwaoni wana mvi. Mvi ni dalili ya ukosefu wa madini mwilini.
Wana afya.
Pumpkin Seeds
Mbegu mbichi kama hizi za Maboga zina faida kubwa sana mwilini : mafuta asilia yasiyodhuru moyo-kama nyama, kinga maradhi, ujenzi na kukarabati ngozi, mifupa, kucha, nywele, kuupa mwili nguvu za rijali nk.
Wenzetu nchi zilizoendelea wanathamini sana matunda na mboga mboga. Si ajabu leo wanaishi maisha marefu kutuzidi.
Sisi tumevijaza vyote hivi, TELE, lakini hatuvithamini.
Zamani nikiwa mtoto ilikuwa kawaida mapishi kuwa na mboga za majani na saladi (kachumbari) leo kutokana na kuingizwa kwa utamaduni wa “vyakula vya haraka “ (“junk”) na “ladha” –vyenye CHUMVI NA MAFUTA MAFUTA MENGI YA KUKAANGA kama chips, nyama choma nk, hatuli sana mboga mbichi mbichi za majani. Na zikipikwa zinachemshwa hadi zinageuka nyani.
Steamed Broccoli-F Macha
Mchanganyiko wa matango na brokoli, nilioutayarisha kwa “mvuke” – yaani kubandika sufuria yenye hizo mboga juu ya nyingine inayochemka chini yake. Upishi huu “barabara” hufanya mboga zisiunguzwe au kuiva sana- zinabakia imara.
Steaming pan-1
Steaming pans
WANGAPI TUNAKULA MATUNDA KWA WINGI AFRIKA?
Kiafya unatakiwa ule matunda aina tano kwa siku kupata faida zake zote mwilini.
Faida za matunda hazihesabaki. Na hayatakiwi yaliwe pamoja na chakula- bali kabla- AU KATI KATI YA MILO MIKUBWA. baadaye. Tabia yetu wengi kuchanganya matunda na milo mikubwa kama wali, ugali, chapati na kadhalika – hausaidii – ni afadhali hata usile kabisa.
Ndizi Mbivu
Ndizi mbivu toka visiwa vya Caribbean – huwa za aina moja tu. Hii ni kama ndizi tunayoita “mchare” kule Uchaggani.
Matunda humeng’enywa kwa vimeng’enyo tofauti na vyakula mama (wanga, protini, nk). Kati ya faida kuu za matunda ni:
1. Zuia maradhi , rutubisha na kinga mwili
2. Sukari , nguvu na mafuta asilia
3. Madini na Vitamin mbalimbali yanayosaidia kujenga, kukarabati na hata kuzuia bakteria na maadui wakubwa wakubwa wa miili yetu mathalan “free radicals”- tunaweza kulinganisha “free radicals” na majivu yanayobakia baada ya moto kuwaka. Hutolewa mwilini kama taka au kuingia mwilini kutokana na uchafu wa mazingira, mioshi ya sigara na magari, taka taka za mashine za kisasa – tena siku hizi wengi tunalala na simu za mkononi zikiwa zimewashwa, tunazibeba kwa wingi. Taka au majivu haya ndiyo kiini kikuu cha maradhi ya kisasa (nchi zilizoendelea) mathalan saratani.

1 comments:

  1. Kutana na mtaalamu wa mitishamba toka tanga anatibu ugumba uzazi uti sugu vumbi z la congo. .nguvu za kiume kiume kukuza uume na kunenepesha uume kukuza hips shape na makalio kwa mvunge. Kuondoa vitambi. Kuondoa harufu mbaya na maji ukeni . kuondoa uchaw zindiko .mpigie dr kupitia 0744903557

    ReplyDelete