Saturday 3 May 2014

JIFUNZE NAMNA YA ULISHAJI WA MTOTO ALIYEZALIWA NA MAMA MWENYE VIRUSI VYA UKIMWI-2

Kutumia maziwa ya mama
Mama aliyeamua kuchagua kutumia maziwa yake ana njia kuu tatu ambazo anaweza
kuamua ni ipi itakayomfaa yeye na mtoto wake. Njia hizi ni:
·       Kunyonyesha maziwa ya mama pekee tangu mtoto anapozaliwa hadi miezi sita;
·       Kunyonyesha maziwa ya mama kwa muda mfupi (chini ya miezi sita);
·    Kutumia maziwa ya mama yaliyokamuliwa na kuchemshwa.
 
Kunyonyesha maziwa ya mama pekee tangu mtoto anapozaliwa hadi miezi 6
Tafiti zimeonyesha kuwa kumnyonyesha mtoto maziwa ya mama pekee kunapunguza
uwezekano wa mtoto kupata uambukizo wa virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama
yake ukilinganisha na kumnyonyesha mtoto na wakati huo huo kumpa maziwa
mengine, vinywaji au vyakula vingine. Iwapo mama atachagua njia hii anashauriwa:
·    
   Kumnyonyesha mtoto wake maziwa yake pekee kwa miezi sita ya mwanzo bila ya
kumpa mtoto kitu kingine chochote hata maji. Kumpa mtoto maziwa mbadala,
vinywaji au vyakula vingine huweza kuongeza hatari ya uambukizo wa virusi vya
UKIMWI kwa mtoto. Vinywaji au vyakula hivyo huweza kusababisha michubuko
Kwenye utumbo wa mtoto na hivyo kuruhusu virusi vya UKIMWI kupenya kwa
urahisi;
·    Kuhakikisha mtoto ananyonyeshwa kila anapohitaji, usiku na mchana;
·       Kumpakata na kumweka mtoto vizuri kwenye titi ili kuzuia matatizo ya matiti
yanayoweza kujitokeza, kama chuchu kupata mipasuko au michubuko. Matatizo
hayo huongeza hatari ya uambukizo wa virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama
kwenda kwa mtoto.
· 
      Kuacha kabisa kumnyonyesha mtoto baada ya miezi sita. Wakati huo mama
anaweza kukamua na kuchemsha maziwa yake akampa mtoto, huku akimpatia vinywaji na vyakula vingine.
Kunyonyesha maziwa ya mama kwa muda mfupi.
Kumwachisha mtoto kunyonya maziwa ya mama yake mapema husaidia kupunguza
uwezekano wa mtoto kuambukizwa virusi vya UKIMWI kupitia maziwa. Kwa
kufanya hivyo muda wa mtoto kuwa kwenye hatari ya uambukizo wa virusi vya
UKIMWI hupungua.
Iwapo mama mwenye virusi vya UKIMWI atachagua njia hii anashauriwa kuacha
kumnyonyesha mtoto wake mapema iwezekanavyo kabla ya miezi sita. Muda
halisi wa kuacha kumnyonyesha mtoto utaamuliwa na mama mwenyewe kwa kuzingatia uwezekano wa kupata maziwa mbadala na uwezo wa kuyatumia
ipasavyo.
Mama akumbuke kumnyonyesha mtoto maziwa yake pekee bila kumpa maziwa
mbadala, vinywaji au vyakula vingine vyovyote. Uchanganyaji wa maziwa ya
mama na maziwa mbadala, vinywaji au vyakula vingine huongeza hatari ya
uambukizo wa virusi vya UKIMWI kwa mtoto. Mama anashauriwa kumpakata na
kumweka mtoto vizuri kwenye titi ili kuzuia matatizo ya matiti yanayoweza
kujitokeza.
Mama anapoamua kuacha kumnyonyesha mtoto wake ashauriwe kufanya hivyo
katika muda mfupi. Ili kuweza kuzuia hatari ambazo zinaweza kujitokeza katika
kipindi hicho cha mpito au kutokana na mabadiliko ya ghafla, mama ashauriwe
kuanza kukamua maziwa yake katika wiki mbili kabla ya kumwachisha mtoto na
kumnywesha mtoto maziwa hayo kwa kutumia kikombe. Hii itamwezesha mtoto
kuweza kuzoea kutumia kikombe.
Mtoto aliyeachishwa kunyonya maziwa ya mama yake kabla ya miezi sita apewe
maziwa mbadala au mama akamue maziwa yake na kuyachemsha kabla ya kumpa
mtoto. Mtoto anyweshwe maziwa hayo mara tano au zaidi kwa siku, akizingatia
kipimo cha mililita 150 kwa kila kilo ya uzito wake kwa siku.
 
Mama anayeamua kuacha kumnyonyesha mtoto wake mapema anapaswa
kusaidiwa kufanya hivyo kwa ufanisi na usalama ili kuepusha madhara yoyote
yanayoweza kutokea kwa mtoto.
Mama akiwa na hali mbaya, hasa anapopata magonjwa nyemelezi na akawa
mgonjwa sana ni vyema aache kunyonyesha.
Kutumia maziwa ya mama yaliyokamuliwa na kuchemshwa
Virusi vya UKIMWI vilivyoko kwenye maziwa ya mama vinaweza kuharibiwa kwa
kuchemsha maziwa hayo yaliyokamuliwa. Tafiti zimeonyesha kuwa virusi hivyo hufa
bila kuharibu kingamwili zilizopo kwenye maziwa iwapo yatapashwa moto kati ya
nyuzi joto 56°C – 63°C kwa muda wa dakika 20. Lakini katika mazingira ya kawaida
sio rahisi kupima nyuzi joto hizo hivyo inashauriwa kuacha maziwa hayo mpaka
yachemke. Mara tu yakichemka yaipuliwe. Kwa kuchemsha maziwa hayo baadhi ya
kingamwili na virutubishi vilivyomo hupungua. Ni muhimu mama apate ushauri wa
daktari au mtaalamu wa afya kuhusu virutubishi vya nyongeza vya kumpa mtoto.
 
Iwapo mama ataamua kutumia maziwa yake aliyoyakamua na kuyachemsha yafuatayo
ni muhimu.
·   
    Mama aelekezwe njia sahihi ya kukamua maziwa yake bila ya kusababisha maumivu ya titi lake;
·  
     Maziwa hayo yachemshwe na yaipuliwe pindi tu yanapoanza kuchemka;
·     
  Maziwa hayo yapoozwe kwa haraka aidha kwa kutumbukiza chombo chenye
·
       maziwa ndani ya maji baridi au kuweka ndani ya jokofu;
·    Mtoto anyweshwe maziwa hayo kwa kutumia kikombe;
·       Maziwa yachemshwe kiasi cha kutosha mlo mmoja tu. 
Maziwa yaliyochemshwa yasihifadhiwe kwa matumizi ya mlo unaofuata.
·
       Mama anapochagua njia hii kama ilivyo kwa njia nyingine anapaswa kupata unasihi na kusaidiwa.
Kutumia maziwa mbadala
Maziwa mbadala yanaweza kutumika kumlisha mtoto aliyezaliwa na mama mwenye
virusi vya UKIMWI. Maziwa mbadala ni pamoja na maziwa yaliyotengenezwa
maalumu kwa watoto wachanga, maziwa yanayotayarishwa nyumbani kutokana na
maziwa ya wanyama kama ng’ombe au mbuzi, maziwa ya unga yenye mafuta (dried full
cream milk) au maziwa yaliyochevushwa (evaporated milk).
 

0 comments:

Post a Comment