Saturday 3 May 2014

JIFUNZE NAMNA YA ULISHAJI WA MTOTO ALIYEZALIWA NA MAMA MWENYE VIRUSI VYA UKIMWI



Uambukizo wa virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama 

kwenda kwa mtoto

Kwa kawaida sio wanawake wote wenye virusi vya 

UKIMWI 

huwaambukiza watoto

wao. Inakadiriwa kuwa kiasi cha asilimia 60 hadi 70 ya 

watoto wanaozaliwa na

wanawake wenye virusi vya UKIMWI hawaambukizwi 

kabisa hata kama hakuna hatua

zozote zilizochukuliwa kupunguza uwezekano wa 

uambukizo. Inakadiriwa asilimia 30

hadi 40 ya watoto huambukizwa virusi vya UKIMWI ambapo:
·      
 Asilimia 5 – 10 ya watoto wanaambukizwa wakati wa ujauzito
·        
Asilimia 10 – 20 wanaambukizwa wakati wa uchungu na kujifungua
·        
Asilimia 5 – 20 wanaambukizwa wakati wa kunyonyeshwa

Mambo yanayochangia kuongeza hatari ya uambukizo wa 

virusi vya UKIMWI

kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto:
·        

Mama kuambukizwa virusi vya UKIMWI wakati wa 

ujauzito au wakati wa kunyonyesha. Wakati mama 

anapoambukizwa, huwa na virusi vingi mwilini kwa hiyo 

uwezekano wa kumwambukiza mtoto ni mkubwa zaidi.
·        

Mama kuwa na UKIMWI.  

Uwezekano wa kumwambukiza 

mtoto ni mkubwa kwani mama atakuwa na virusi vya 

UKIMWI vingi mwilini mwake.
·        

Mama kuwa na maambukizo ya magonjwa ya ngono wakati 

wa ujauzito. Magonjwa ya ngono husababisha 

michubuko ukeni ambayo huongeza hatari ya uambukizo wa 

virusi vya UKIMWI iwapo mama hafanyi ngono salama.
·        

Taratibu zinazotumika wakati mama anapojifungua. Kwa 

mfano kuongeza njia ya uzazi, uchanaji mapema wa utandu, 

mtoto kunyonywa uchafu baada ya kuzaliwa.
·        

Hali ya lishe ya mama. Mama mwenye hali nzuri ya lishe 

huwa na mfumo thabiti wa kinga ambao huchelewesha mama 

huyo kupata UKIMWI.
·    
  
 Hali ya matiti ya mama. 

Matiti yenye vidonda au 

michubuko, chuchu zinazotoa damu na majipu ya titi 

huongeza hatari ya mama kumwambukiza mtoto wake iwapo 

mtoto ananyonyeshwa.


·     
  Ulishaji wa kuchanganya maziwa ya mama na vinywaji 

au vyakula vingine. Vyakula na vinywaji kama maziwa 

mbadala, maji, chai, uji, maji ya matunda, n.k. huweza 

kusababisha michubuko kwenye utumbo wa mtoto na hivyo 

kutoa mwanya kwa uambukizo wa virusi vya UKIMWI.
·       

 Muda wa kunyonyesha. 

 Kadiri kipindi cha kunyonyesha 

kinavyokuwa kirefu, ndivyo uwezekano wa kumwambukiza 

mtoto unavyoongezeka. Hatari huongezeka zaidi iwapo 

mama mwenye virusi vya UKIMWI atamnyonyesha mtoto 

wake kwa zaidi ya miezi sita kwani wakati huo mtoto 

hupewa vyakula vingine.
·        
Hali ya kinywa cha mtoto. Vidonda vya kinywani au kooni na 
utandu mweupe kinywani kwa mtoto huweza kuongeza 

hatari ya uambukizo wa virusi vya UKIMWI kupitia 

sehemu hizo zenye vidonda.

 

“Ikumbukwe kuwa njia kuu ya kuzuia mtoto kupata virusi 

vya UKIMWI ni wazazi kuzuia wasiambukizwe virusi hivyo. 

Jukumu hilo ni la baba na mama.”

Kumlisha mtoto mchanga aliyezaliwa na mama 

mwenye virusi vya UKIMWI (miezi 6 ya 

mwanzo)
 

Tamko rasmi lililotolewa na mashirika ya kimataifa 

(WHO/UNAIDS/UNICEF)

linasisitiza mambo muhimu yafuatayo:

• Mama mwenye virusi vya UKIMWI aelekezwe kikamilifu 

kuhusu hatari ya

kuambukizwa mtoto kupitia maziwa ya mama na njia 

nyingine;

• Wanawake wahimizwe na wapewe huduma za ushauri 

nasaha na kupima virusi vya

UKIMWI kwa hiari (VCT);

• Mwanamke mwenye virusi vya UKIMWI apewe taarifa 

muhimu na zilizo sahihi,

kumwezesha kufanya uamuzi sahihi wa njia ya kumlisha 

mtoto wake, iwe ni

kunyonyesha kwa maziwa yake au kutumia maziwa mbadala.

KUMBUKA

Ni muhimu kuhakikisha kwamba wanawake ambao 

hawajaambukizwa virusi vya

UKIMWI na wale wasiojua hali zao za uambukizo 

wanaendelea kushauriwa

kunyonyesha maziwa yao, na wasishawishike kutumia 

maziwa mbadala kwa
kuwaona wengine walioshauriwa na kuamua kutumia maziwa hayo.

Njia zinazoweza kutumika kumlisha mtoto 

mchanga tangu anapozaliwa

mpaka miezi sita kwa mama anayeishi na 

virusi vya UKIMWI

Kumbuka kuwa katika miezi sita ya mwanzo ya maisha ya 
mtoto yeyote, maziwa ndiyo

chakula pekee na muhimu sana. Maziwa hayo yanaweza 

kuwa ya mama au maziwa

mengine. Ikiwa mtoto hanyonyeshwi maziwa ya mama basi 
apate maziwa mengine

kiasi cha mililita (ml.) 150 za maziwa kwa kila kilo moja ya 

uzito wake kwa siku. Kwa

mfano mtoto mchanga mwenye kilo tano anahitaji mililita 

(ml.) 750 za ujazo za maziwa

(yaani ml. 150 x kilo 5) kwa siku, kiasi hiki kinaweza 

kugawanywa katika milo mitano

au zaidi kwa siku. Ni muhimu kutumia kikombe kumlisha 

mtoto badala ya chupa ya

kunyonya.
Hii hupunguza hatari ya maradhi ya kuhara kwani ni rahisi kusafishakikombe kuliko chupa.

Kuna njia kuu mbili zinazoweza kutumika kumlisha 

mtoto 

aliyezaliwa na mama

mwenye virusi vya UKIMWI. Njia hizi ni kutumia 

maziwa ya mama na kutumia

maziwa mbadala.

inaendelea sehemu ya pili ..

0 comments:

Post a Comment