Saturday 10 May 2014

FAIDA ZIPATIKANAZO KWA KUTUMIA LIMAO KIMATIBABU



Limau lina manufaa chungu nzima kama vile kutuliza, kutibu, kupunguza sumu mwilini n.k.

Shinizo la Mawazo: 
Huondoa uchovu wa akili, kisunzi, na pia wasiwasi. Limau lina uwezo wa kutuliza akili kwa kuondoa mawazo. Aidha unapumua harufu ya limau unaweza kujiongezea umakinifu.

Usingizi: 
Utumiaji wa limau husaidia kumpa mtu usingizi na kuepusha tatizo la kupata usingizi.

Mfumo wa Kinga: 
Limau lina kiwango kikubwa cha Vitamini kwa hivyo ni zuri kwa kuimarisha kinga mwilini, kwa kuzipa nguvu chembechembe nyeupe za damu, na kuimarisha mzunguko wa damu mwilini.

Homa: 
Linaweza kutumika kuponya maradhi ya kuambukiza kama homa, malaria na homa ya matumbo.

Matatizo ya Tumbo: 
Hutibu maradhi tofauti ya tumbo kama shida za usagaji chakula, , maumivu ya tumbo, na mshipa.

Kupunguza Uzani: 
Hutumika na wengi kupunguza Uzani.

Pumu: 
Inaaminika kwamba limau linasaidia kutibu pumu.

Nywele: 
Aidha limau hutumiwa kwa utunzaji nywele. Limau huzifanya nywele kuwa na afya na za kuvutia, na huondoa uyabisi.
Ngozi: 
Limau hutumiwa kutunza ngozi, kwa kuipa afya. Hutibu vidodosi na mba.

0 comments:

Post a Comment