Wednesday, 23 April 2014
MAAJABU YA ASALI MBICHI NA KARANGA KWA NGOZI YA BINADAMU
. Karanga ni mojawapo ya nafaka muhimu kwa afya ya binadamu. Huweza kutumika kama chakula, mafuta, kiungo na hata kwa ajili ya urembo.
Zao hilo huweza vile vile kufanya maajabu katika ngozi. Bila kubagua jinsia, matumizi ya karanga husaidi katika kuondoa makunyanzi na kulainisha ngozi.
MAHITAJI
Kwa kazi hii ya ngozi, karanga zinazohitajika ni zile mbichi. Kitu kinachohitajika ni kuchukua karanga mbichi ambazo hazijakaangwa kiasi kidogo kama kikombe kidogo cha chai.
MATAYARISHO
Zianike karanga juani kwa muda ili ziweze kumenyeka kwa urahisi bila kukaanga. Saga karanga zako kwa kutumia blenda au kitu chochote kitakachoweza kuzilainisha na kuwa unga laini.
Chukua unga wako wa karanga na uuchanganye na asali mbichi kiasi kidogo, kisha acha kwa muda wa dakika 10 ili vichanganyike.
MATUMIZI
Chukua mchanganyiko wako, kisha paka usoni hasa zile sehemu unazoziona kuwa na mikunjo zaidi.
Subiri kwa dakika kama 10, kisha osha uso wako na sabuni isiyo na kemikali baada ya hapo futa uso wako na kitambaa kisafi na kikavu. Subiri tena kwa dakika 5 halafu paka mafuta au losheni. Unashauriwa kufanya hivi mara moja kwa wiki.
Kiasili njia hii imekuwa ikitumiwa na Wanyamwezi wa Tabora kama kipodozi kwa ajili ya mabinti wadogo pindi wanapokaribia kufanyiwa sherehe maalum.
Unaweza pia kusugua taratibu uso kwa kutumia mchanganyiko wako ili kuondoa takataka katika mwili wako ambapo baada ya kumaliza zoezi hilo unaweza kujipodoa kwa kupaka aina nyingine za vipodozi.
Kwa kuwa hazina madhara, unaweza kufanya hivi kila siku na utafurahia matokeo yake.
Related Posts:
FAIDA 27 ZA KIAFYA ZIPATIKANAZO KWA KUTUMIA ASALI NA MDALASINI MDALASINI NA ASALI Asali inafahamika vema Duniani kote kama mojawapo ya silaha ya kiajabu katika kupigana na magonjwa na matatizo yatokanayo na uzee. Sasa hivi, utafiti mpya umeonyesha kwamba uwezo wa asali unaweza ku… Read More
Top 10 Health Benefits of Honey Honey is a sweet liquid produced by honeybees from the nectar they gather from flowers via the complicated process of regurgitation and evaporation. Honey is made up of glucose, fructose, and minerals such as iron, calcium… Read More
YAFAHAMU MAGONJWA 23 YANAYOTIBIWA KWA MATUMIZI YA ASALI 1. Ugonjwa wa viungo/maumivu na uvimbe. 2. Kukatika kwa nywele. 3. Ukungu wa miguu. 4. Maambukizo kwenye kibofu cha mkojo. 5. Maumivu ya jino. 6. Lehemu (Cholestral). 7. Ugumba 8. Mchafuko wa tumbo. 9. Ugonjw… Read More
MAAJABU YA ASALI MBICHI NA KARANGA KWA NGOZI YA BINADAMU . Karanga ni mojawapo ya nafaka muhimu kwa afya ya binadamu. Huweza kutumika kama chakula, mafuta, kiungo na hata kwa ajili ya urembo. Zao hilo huweza vile vile kufanya maajabu katika ngozi. Bila kubagua jinsia, matumi… Read More
MARADHI 27 YANAYOTIBIWA KWA KUTUMIA ASALI YA NYUKI Matumizi ya asali kama tiba kwa magonjwa mbalimbali ni kitu ambacho kinafahamika kwa karne nyingi zilizopita duniani kote.Vitabu vingi vya zamani vinazungumzia namna watu walivyotibiwa magonjwa mbalimbali kutokan… Read More
Shukrani sana kwa darasa zuri
ReplyDeleteNingesauri pia uruhusu right-click kwenye mada zako maana iko disabled ie mtu hawezi ku-right click
Ukitaka kusoma Messege zangu ubonyeze mahali palipo nadikwa hivi (Read More) unaweza kusoma ukitaka kukopi niambie nitakupatia unayotaka.
ReplyDelete