Thursday, 12 March 2015

VYAKULA MAARUFU KWA KUZUIA UVIMBE MWILINI


Vyanzo vinavyoweza kusababisha mlipuko wowote wa uvimbe mwilini na magonjwa mengini ya aina hiyo ni vingi, kutokana na aina ya vyakula tunavyokula, mazingira tunayoishi na hata msongo wa mawazo unaosababishwa na kazi tunazozifanya.
Kwa kawaida mwili umeumbwa kujikinga  wenyewe na kuwa na uwezo wa kupambana na kuzuia maambukizi ya maradhi na milipuko kama hiyo. Ili mwili uwe na uwezo huo, unahitaji uupe uwezo kwa kula vyakula vinavyoongeza kinga mwilini, hasa kinga ya kuzuia uvimbe, miongoni mwa hivyo ni pamoja na hivi vifuatavyo:
MAHARAGE
Jamii yote ya maharage, ikiwemo na soya, inaaminika kuwa na kiasi kingi cha protini na virutubisho vingine vingi vinavyohitajika mwilini kuzuia magonjwa ya mlipuko na uvimbe. Pia vyakula hivi vinafaa kwa wagonjwa wa moyo.SAMAKI NA MAFUTA YAKE
Ulaji wa samaki, hasa aina ya jodari, ni muhimu sana, kwani samaki hawa wana kiwango kingi cha virutubisho aina Omega-3 na 6. Ukiweza, pendelea kula samaki kila mara katika mlo wako wa kila siku. Halikadhalika, utumiaji wa mafuta ya samaki, kiasi cha kijiko kimoja au viwili kwa siku ni muhimu ili kuimarisha kinga ya mwili.
VIUNGO
Katika mlo wako wa kila siku, usipuuzie viungo vya mboga vyenye asili ya miti, kama vile bizari, mdalasini, tangawizi na hiriki. Miti hii ina kiwango kikubwa cha virutubisho vyenye uwezo wa kupambana na kutoa kinga dhidi ya magonjwa ya uvimbe. Hivyo hakikisha kwenye mapishi yako, unaangalia namna ya kuchanganya viungo hivi.
VIAZI VITAMU
Viazi vitamu vina kiwango kikubwa pia cha virutubisho vyenye uwezo wa kung’arisha ngozi, kuimarisha kinga ya mwili na pia afya ya moyo. Kwa upande wa kuzuia magonjwa ya uvimbe, viazi pia vimetajwa kuwa na uwezo mkubwa sana. Mbali ya viazi, pia hata maboga na karoti nazo zina virutubisho vingi vya kuimarisha kinga ya mwili.
CHAI
Unaweza kupamba na magonjwa ya uvimbe na kuupa mwili wako kinga ya mwili dhidi ya magonjwa hayo hata kwa kunywa chai, hasa ya majani ya kijani (green tea), ambayo utafiti wa kitabibu unaonesha kuwa na kiwango kingi cha virutubisho vya kuongeza kinga ya mwili.Kwa ujumla, ni vyema kuwa na kawaida ya kula vyakula asili vya aina mbalimbali na bila kusahau mboga za majani ya aina mbalimbali pamoja na matunda ili kujenga kinga ya mwili imara ambayo itakuwa tayari kupambana, siyo tu na magonjwa ya uvimbe mwilini, bali hata magonjwa mengine hatari.

Related Posts:

  • WATU WANENE WACHUNGE KALORI ZAO LAKINI kabla sijaendelea mbele pengine ningechukua fursa hii kuwafahamisha wasomaji wetu maana ya neno kalori. Maana ya ˆkalori kwa mujibu wa fizikia, ni kiasi cha nishati zinazohitajika kuongeza joto la gramu moja… Read More
  • VYAKULA VINAVYOCHANGIA UKOSEFU WA USINGIZI Usingizi ni muhimu kama kilivyo chakula bora. Unaweza kuzingatia sana suala la mlo kamili, kufanya mazoezi na mengine yanayokubalika kiafya, lakini kama hupati usingizi wa kutosha kila siku, afya yako iko hatarini. Kaha… Read More
  • VYAKULA MUHIMU KUKUWEZESHA KUPATA UJAUZITO LISHE bora  ni muhimu kwa kila mtu, mwanamke na mwanaume na watoto wanatakiwa wapate lishe bora. Mwanamke aliye katika umri wa kuzaa anahitaji apate lishe bora ili kumwezesha kupata ujauzito pale anapohitaji. Haitak… Read More
  • MWILI HUJITIBU WENYEWE, UPE VYAKULA SAHIHI TU! NI ajabu lakini ndiyo ukweli wenyewe. Mwili wa binadamu hujitibu wenyewe iwapo unapewa virutubisho sahihi vinavyoweza kutengeneza kinga ya mwili na kutoa ulinzi stahiki. Ni rahisi kulibaini hilo pale mtu anapo… Read More
  • DHIBITI MAUMIVU YA VIUNGO KIASILI ZAIDI KATIKA  makala yaliyopita nilipokea simu nyingi kutoka kwa wazee, wakilalamika na kuomba msaada wa tiba ya kupambana na tatizo la kuumwa viungo vya mwili. Lakini katika siku za hivi karibuni, siyo wazee tu, bali hata vi… Read More

0 comments:

Post a Comment