Saturday, 20 December 2014

NJIA BORA ZA ASILI ZA KUKUZA NYWELE ZAKO MAMBO UNAYOTAKIWA KUYAFANYA



Kwa wale ambao tuna nywele asilia a.k.a natural hair,tayari tunafahamu changamoto kadhaa tunazokumbana nazo.Kwa wale mnaofikiria kuanza kuwa na nywele asilia,karibuni sana tuendelee kujuzana namna ya kutunza nywele zetu kama tulivyopewa na Mungu.
Katika mada ya leo,nitakwenda kuzungumzia vitu vya kuzingatia ili kuikuza nywele yako asilia kwa haraka zaidi.Je,unazifahamu nywele zako vizuri?Una nywele za aina gani?Zina tabia gani?Zinataka nini?
1.Kuzikubali kama zilivyo na kuzipenda.
Utasikia ..hiki kipilipili changu ni steelwire ya kimataifa, ..hakitikisiki hata upepo wa dunia yote ungevumia pande hizi.Mwingine oh..nywele zangu kama miti ya mibuyu kichwani…hazishikiki.Tatizo ni kwamba hamjafahamiana vizuri yani wewe na nywele zako.Hata mimi niligombana nazo sana huko nyuma kabla ya kuzielewa vizuri.Jenga mahusiano mazuri tu na nywele zako,zielewe,ukifikia hapo utaanza kuzipatia hata hazitakusumbua.
2.Usafi wa ngozi ya nywele na nywele zenyewe.
Nywele zenye afya huanzia kwenye ngozi safi ya nywele.Nafahamu unataka nywele zako zisidumae kwa hiyo zioshe vizuri.Wakati uliopita nilizungumzia kuziosha kwa product zilizo rafiki( ‘friendly’) .Ngozi safi ya nywele itasababisha nywele kupata njia ya kujitokeza nje kwa urahisi.Unapoziacha chafu,ule uchafu unaziba matundu ya nywele zako na kuzuia njia,kama ambavyo matundu ya uso yakiziba unapata machunusi maana uchafu unajaa basi kwa nywele hazitakua vizuri.
3.Linda unyevu wa nywele zako
Kila mtu akisikia kiu hunywa maji.Nywele zako zinahitaji kulindwa zisisikie kiu.Unapoziosha,yale mafuta asilia ya kuzilinda huondoka na uchafu.Nywele inabaki ikiwa na udhaifu fulani maana haiwezi hata kushikilia hayo maji yaliyopo vizuri,na zikikauka zinakua kavu sana.Ni vizuri kabla hazijakauka vizuri,ukazi-’condition’.Kwa nywele ambazo ni nyepesi na chache,pia kuna product za kuzisaidia ziweze kutunza vizuri unyevu na hivyo kuwa na afya nzuri.
4.Zifahamu nywele zako
Yani hapa ndo shule ilipolalia kabisaa maana ukizijua tu basi utazihudumia kwa usahihi.Unatakiwa kuangalia namna gani nywele zako zinanyonya unyevu.Unajuaje?
Chukua kikombe,kijaze maji safi.Ukipata glass itakuwa vizuri zaidi.
Chomoa unywele mmoja kichwani,hakikisha unatoka na kale kamzizi kake keupe keupe hivi.
Tumbukiza unywele wako kwenye glass yako ya maji hakikisha imeingia yote.Kama ikizama hapo hapo na hainyanyuki tena,basi nywele zako zinanyonya unyevu kwa haraka kabisa.Kama inachukua muda kuzama,au haizami kabisa,nywele zako zinanyonya unyevu taratibu au zinanyonya kwa shida.(Wala usihofu,zipo namna ya kuzifanya zinyonye unyevu kwa haraka,tutajuzana.)Ni kwamba ‘cuticle’ zake zimefunga haswa,ndio maana unyevu au maji haviingii kwa haraka.
Kwa hiyo ukifanya ‘deep conditioner’ kwa kutumia joto kama la drier lakini uwe moto mdogo sana au ufanye ‘hot oil treatment’ itakusaidia ‘cuticle’kufunguka na unyevu kupita.
Mbadala,unaweza baada ya kuosha suuza na maji ya uvuguvugu halafu weka mafuta ya kimiminika.Inasaidia sana.
Mimi nina aina gani?..Nina nywele zinazonyonya unyevu haraka.
5.Mafuta ya Kupaka kichwani.
Ni ya muhimu mnoo!.Nimefanya utafiti wa kina nimeona mafuta ya nazi yanaweka afya nzuri kwa nywele  aina nyingi hivyo na mimi nikaanza kuyatumia.Kwangu mimi,mafuta ya nazi ya kutengeneza mwenyewe yamenikubali sana.Japo huwa nanunua pia mafuta kama ya Zaituni Olive(extra virgin) na ya Tea tree.
6.Kuzichambua vizuri kabla ya kuchana.
Uwe mkarimu na mwenye subira kwa nywele zako.Mimi zikijifunga huwa nazichambua kwa mikono taratibu wakati mwingine nazilowesha na maji kwa mbali halafu nachana kwa chanuo lenye mapana sio ambalo reli zake zimebanana.sio kitana.Chanuo kubwa(wide toothed comb).
7.Usizisumbue mara kwa mara na usuke mitindo ya kuzitunza zikue.
Kama unataka zikue haraka,usizisumbue sana.Unaweza ukasuka mitindo mizuri tu ukakaa nazo wiki nzima au kadri zitakavyodumu.Au upunguze kuzichana mara kwa mara lakini utafute siku kama wikiendi ukae uzichambue taratibu na vidole kuondoa mafundo.Kuchana mara kwa mara zinapukutika,zinaanguka.Zitakua lakini sio kwa kasi ya kama ukizisuka ukaziacha kwa muda.
8.Punguza matumizi ya vitu vya moto kwenye nywele zako kama pasi ya nywele na vingine vya hivyo.Mimi dryer la nywele situmii zaidi ya mara mbili kwa mwezi.Mara nyingi naziacha zikauke na hewa hata kama nimezifunga rollers natoa kesho baada ya masaa 24.
Kwa leo naishia hapa.Tukutane tena wakati ujao kwenye kujuzana zaidi.Unakaribishwa kwa maoni,ushauri na kupendekeza mada yoyote izungumziwe kuhusu nywele asilia.
Mada ijayo tutazungumzia aina za nywele zilizopo humu duniani kwa ujumla.
Nakutakia mapenzi mema ya nywele zako,natumaini mmefahamiana kiasi sasa.

7 comments:

  1. I am very happy to read this. Appreciate your sharing
    run3unblockedgame.com

    ReplyDelete
  2. I started on COPD Herbal treatment from Ultimate Life Clinic, the treatment worked incredibly for my lungs condition. I used the herbal treatment for almost 4 months, it reversed my COPD. My severe shortness of breath, dry cough, chest tightness gradually disappeared. Reach Ultimate Life Clinic via their website www.ultimatelifeclinic.com . I can breath much better and It feels comfortable!

    ReplyDelete
  3. I am now leaving a healthy life after using the herbal medicine to cure myself from herpes, i am now herpes disease free after the application and usage. You can contact him for your herbal medication from via Email Robinsonbuckler11@gmail com. Thanks and God Bless you for your help, referring people with herpes disease to use this herbal remedy__________________________🌿🌿🌿

    Good for the following

    Shingles,

    Cold sore,

    HPV,

    HSV1&2,

    ReplyDelete
  4. i was diagnosed with HERPES VIRUS for 4 years ago i lived in pain with the knowledge that i wasn't going to ever be well again i contacted so many doctors and visit many hospital on this issue and wasted a large sum of money but my condition never got better i was determined to get my life back so one day i saw miss Katrina post on how Dr oriane saved her from the same VIRUS with his herbal medicine i contacted Dr oriane on his email address droriane6@gmail.com we spoke on the issue i told him all that i went through and he told me not to worry that everything will be fine again so he prepared the medicine and send it to me through courier service and told me how to use it,after 19 days of usage I went to see the doctor for test ,then the result was negative,am the happiest person on earth now. This testimony is real.Thanks to Dr oriane God bless you. or chat on whats-app +2349031652461

    ReplyDelete
  5. Hello everyone i was diagnosed of herpes simplex virus for about 8 months ,I’ve lost all hope and my doctor said there is no possible cure and I have been taken antiviral to sustain myself I have had several out break from the time I was diagnosed till I got to know about Dr. Oriane through a friend who he cured of Herpes . I contacted him and he sent me his herbal remedy which I took as he directed me to do for some days and I went to the hospital after consuming his Herbal medicine and I was confirmed Herpes Negative after 8 months of pains and depression , it was indeed a miracle, Dr. Oriane is a great man, I have heard so much about how he has helped a lot of people, He also cures ALS, HEPATITIS B, CANCER, HERPES, DIABETES and lots more. If you have any issues you can contact him for help add him on whatsapp +2349031652461. or via email:Email droriane6@gmail.com

    ReplyDelete
  6. There is no problem without a solution, And today God has used Dr. Oriane to solve my own problem with his herbal medicine, i was diagnosed with Herpes virus 2 years ago, and i was told it has no cure that i have told me taking drugs, this break my heart because i hate drugs, this made me started looking for ways and means to get this virus out of my body, and i started making research and one day i came across a man who was sharing testimony how Dr. Oriane Cure him and his wife from Herpes Virus, hearing this news Gladys my heart and i quickly collected the contact of the doctor he posted and message him, and after telling him all my problems he said he can help me and told me the cost of the medicine and said i will have to pay for the delivery first that when i receive the medicine before i will pay for the medicine and then i send him my address. This makes it two weeks now that I have finished taking his treatment and have done 3 different tests and all came out negative and I'm now living a normal life free from drugs. You can also contact this Doctor for any health issues or challenges for a solution. Here is his contactEmail Address: droriane6@gmail.com or whatsapp him on +2349031652461 Congratulations as you find solutions to all your health problems.

    ReplyDelete