Monday 17 November 2014

MAHUSIANO KATI YA TUMBO KUJAA GESI NA MUUNGURUMO-2



Naendelea kuelezea kati ya uhusiano wa tumbo kujaa gesi na miungurumo
inayotokea tumboni nk.Kuna ile hali ya mtu kutokujisikia kufanya kitu chochote, yaani kulala inakuwa ni ngumu kwake, kukaa anapata tabu sana, akienda kwenye kazi zake anakua mzito.
Wakati huohuo, anaandamwa na kukosa choo kwa muda mrefu nayo ni dalili kubwa sana ya tatizo linaloitwa constipation kitaalamu.
Dalili nyingine kubwa inakuwa ni maumivu chini ya kitovu na hii huwatokea sana wanaume na wanawake pia huandamwa na dalili kama hii.Ikiwa unapatwa na dalili kama hii na wakati huohuo unakuwa hupati choo basi kuna uwezekano mkubwa ukawa na tatizo hilo la constipation.
Dalili nyingine kubwa inayowatokea wanaume ni ile ya kukosa hamu kabisa ya kushiriki tendo la ndoa, hata akishiriki inakuwa ni mara moja na anashindwa kuendelea.Kama unakumbwa na dalili hiyo na wakati huohuo unaandamwa na kutokupata choo kwa muda na tumbo kuunguruma basi ujue unaandamwa na tatizo hili la constipation.
Dalili nyingine kubwa ni kupatwa na kitu kinachoitwa bawasili au mgolo, na hii ni ile hali ya kutokwa na kitu kama kinyama mtu anapokwenda haja kubwa.Wakati mwingine kinakua kinauma sana na kuandamwa na choo kigumu, nayo ni dalili ya constipation.
Kama unapatwa na dalili kama hizi basi ni vizuri kuwasiliana nasi kupitia namba zetu ili kulitatua tatizo hili.
Kwa ushauri, vipimo na tiba dokta wetu anapatikana kwenye vituo vyake vya Dar es Salaam, Tanga, Morogoro na Mwanza.

0 comments:

Post a Comment