Wanawake wengi hujua wameshika mimba aghalabu wiki 3 baada kushika mimba. Mwili wenyewe utakuonyesha/utakutabiria kama:
Hedhi yako itakoma/itakuwa nyepesi
Utasikia uchefuchefu/utatapika (ugonjwa wa asubuhi – ‘morning sickness’ – na inaweza kutokea wakati wowote wa siku pia).
Matiti yako yataanza kuwasha, kufura au yataanza kuwa makubwa.
Chuchu (ncha ya titi) na sehemu zilizokaribiana zitaanza kuwa nyeusi na zizizoweza kuvumilia.
Itakubidi kwenda haja ndogo mara kwa mara.
Utasikia uchovu
Kusokotwa na tumbo
Kama umeona baadhi ya dalili hizo, unaweza kuwa na mimba. Pata jaribio/uchunguzi kipimo cha mimba ili kupata yakini! Unaweza pimwa bure katika kliniki iliyokaribu nawe au ununue kifaa vya kujipmia nyumbani kutoka duka la dawa. Daktari wako anaweza kukupima pia au atakuelekeza kwa mtaalamu kama hauna.
Umuhimu wa kunyonyeasha
Pindi tu baada ya kujifungua,kumung’unya wa kujirudia rudia wa mtoto hutoa oksitoksini kutoka kwa teziubongo wa mama.Homoni hii haiashirii tu matiti kumtolea mtoto maziwa (hii inajulikana kama tendohiari la utoaji wa maziwa ama “let-down), lakini wakati huo huo husababisha mkunyato katika mji wa mimba. Mkunyato unaotokea huzuia utokaji wa damiu uliozidi na husaidia mji wa mimba kurudia ukubwa wake wa kawaida.
Ikiwa mama atanyonyesha mtoto bila ya kutumia maziwa mbadala ama vyakula vingine kipindi chake cha kuingia mwezini kitacheleweshwa.Tofauti na akina mama ambao huwalisha watoto wao kwa kutumia chupa, ambao kwa
kawaida huingia mwezini baada ya majuma sita hadi manane, akina mama wanaonyonyesha wanaweza kukaa bila ya kuingia mwezini kwa kipindi cha miezi kadhaa. Hali hii ina manufaa muhimu ya kuhifadhi chuma katika mwili wa mama na mara kwa mara hutoa nafasi asili baina ya uja uzito.
Kunyonyesha ni kuzuri kwa akina mama wapya na vile vile kwa watoto wao. Hakuna chupa za kufisha vijidudu,hakuna haja y a kununua maziwa ya mtoto,kupima na kuyachanganya.Inaweza kuwa rahisi kwa mama anayenyonyesha kupoteza uzani wa uja uzito vile vile kwani kunyonyesha kunatumia vizio vya joto. Kunyonyesha pia husisimua mji wa mimba kukunyata na kurudia ukubwa wake halisi.
Mwanamke anayenyonyesha huzalimishwa kupumzika ambako anahitaji sana.Ni lazima akae chini na kupumzika kila baada ya masaa kadhaa ili anyonyeshe.Kunyonyesha wakati wa usiku ni rahisi pia. Ikiwa amelala chini, mama anaweza kulala huku bado ananyonyesha.
Kunyonyesha pia ni njia asili ya kuzuia mimba-hata ingawaje sio ya kutegemewa.Kunyonyesha mara kwa mara huzuia uzalishaji wa mayai na hivyo kupunguza uwezekano wa mama anayenyonyesha kuingia mwezini, kutoa mayai ama kupata uja uzito. Hakuna hakikisho hata hivyo. Mama ambao
hawataki watoto wengi wanapaswa kutumia mbinu za kuzuia mimba hata ikiwa bado wananyonyesha. Kujidunga homoni na vipandikizi wakati wa kunyonyesha ni salama kama zilivyo mbinu za kinga za kuthibiti uzazi.Maelezo kwenye vidonge vya kuthibiti uzazi vinasema ya kwamba ikiwezekana mbinu nyingine ya kuzuia uja uzito inafaa kutumiwa hadi mtoto achishwe ziwa.
Kunyonyesha pia hupunguza gharama.Hata ingawaje mwanamke anyenyonyesha huwa na hamu kubwa ya chakula na hula kalori zaidi, chakula chake cha ziada sio ghali ukilinganisha na kununua maziwa ya mtoto. Kunyonyesha hupunguza matumizi ya pesa ilhali hutoa chakula ambacho ni bora zaidi kwa mtoto.
Manufaa ya Kipindi Kirefu ya Kunyonyesha
Sasa imeanza kuwa bayana ya kwamba kunyonyesha humpatia mama zaidi ya manufaa ya kipindi kifupi katika kipindi cha hapo mwanzoni baada ya kujifungua.
Utafiti umeonyesha manufaa mengine ya kiafya ambayo mama anaweza kuyafurahia kwa kunyonyesha.Manufaa haya yanajumuisha afya bora, kupungua kwa hatari ya baadhi ya saratani na manufaa ya saikolojia.
Kitu kingine muhimu kinachotumiwa katika kuzalisha maziwa ni kalshiamu.Utafiiti wa hivi sasa unaonyesha ya kwamba baada ya kuachisha watoto ziwa,uzito wa mfupa wa mama anayenyonyesha hurudia ule wa kabla ya uja uzito ama huwa hata wa juu zaidi. Mwishowe,kunyonyesha kunaweza kusababisha mifupa yenye nguvu zaidi na hupunguza hatari ya ugonjwa wa mifupa (osteoporosis) “mifupa iliyokonda.”Utafiti wa hivi sasa umethibitisha ya kwamba wanawake ambao hawakunyonyesha wako katika hatari kubwa ya kuvunjika kwa nyonga baada ya kukoma hedhi.
Wanawake ambao hawanyonyeshi wameonekana katika utafiti mwingi kuwa katika hatari kubwa ya kupata saratani za uzazi. Saratani ya ovari na ile ya mji wa mimba zimepatikana kuwa za kawaida katika wanawake ambao hawakunyonyesha.
Hitimisho: Kunyonyesha hupunguza hatari ya matatu kati ya magonjwa mabaya sana katika wanawake-saratani za wanawake, ugonjwa wa moyo na ugonjwa wa mifupa-bila ya tishio lolote la kiafya.
Masuala ya Kisaikolojia Kwa Akina Mama Wanaonyonyesha
Kunyonyesha ni zaidi ya kutoa tu lishe na kumlinda mtoto dhidi ya magonjwa kupitia kwa maziwa ya mama.Kunyonyesha hutoa njia ya kipekee ya kuingiliana baina ya mama na mtoto, kukaribiana kwa papo hapo kwa ngozi –kwa-ngozi na malezi ambayo akina mama wanaotumia chupa wanapaswa kufanya jitihada ili wayarudufu.
Prolactin ambayo ni homoni inayotengeneza maziwa,huonekana kutoa utulivu maalumu kwa akina mama na kuwasaidia kupambana na mfadhaiko kwa njia iliyo bora.
Wednesday, 20 August 2014
MUHIMU KUJUWA WAKATI UNA MIMBA
Related Posts:
TATIZO LA KUSHINDWA KUJIZUIA KUJIKOJOLEA (URINARY INCONTINENCE) Tatizo hili la kujikojolea bila sababu yoyote ya msingi ni tatizo linaloathiri watu wengi sana na ambalo huleta usumbufu na aibu kubwa kama litampata mtu. Tatizo hili huwakumba sana wanawake kuliko wanaume na inakisiw… Read More
MAUMIVU KATIKA TITI (BREAST PAIN) Karibu asilimia 20 hadi 40 ya wagonjwa maumivu hayo huweza kuisha yenyewe, iwapo vipimo havijaonyesha vivimbe au uvimbe kwenye titi basi dawa hutolewa ili kutoa maumivu hayo. Zipo dawa za kunywa au kuchoma katika ziwa,… Read More
TATIZO LA MIMBA KUTUNGA NJE YA MFUKO WA UZAZI (ECTOPIC PREGNANCY) TATIZO LA MIMBA KUTUNGA NJE YA MFUKO WA UZAZI (ECTOPIC PREGNANCY) Mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi wa mwanamke au ectopic pregnancy ni tatizo ambalo limetokea kuathiri wanawake mbalimbali. Kwa kawaida, isipokuwa mara c… Read More
SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO WAKATI WA UJAUZITO Maumivu ya tumbo wakati wa miezi mitatu ya kwanza ya mimba ni mojawapo ya matatizo yanayolalamikiwa na kina mama wengi.Kuna matatizo mengi ambayo yanahusiana tu na mimba, hata hivyo, ni muhimu kukumbuka kwamba hali yo… Read More
TATIZO LA YEAST INFECTION WAKATI WA UJA UZITO Yeast infection ni aina ya fungus inayokua kwenye sehemu ya uke. Wakati wa ujauzito kwa ajil ya mabadiliko mbali mbali ya kikemikali na hormone basi mwili unashindwa kuregulate hali ya eneo hili. Kwa … Read More
0 comments:
Post a Comment