Thursday, 28 August 2014

BAMIA HUWEZA KUSAIDIA WAGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO.

Mtandao wa healthandcure.com unawanukuu wataalamu wa afya wakieleza kuwa watu wanaosumbuliwa na maradhi kadha wa kadha ya mfumo wa chakula kama vile vidonda vya tumbo na mengine yanayofana na hayo wanaweza kupata ahuweni au kupona kabisa ikiwa watakula bamia.
Unafahamu kuwa kwa kula bamia unaweza ukawa umejiondoa katika hatari ya kupata maradhi mbalimbali?
Mtandao wa healthandcure.com unawanukuu wataalamu wa afya wakieleza kuwa watu wanaosumbuliwa na maradhi kadha wa kadha ya mfumo wa chakula kama vile vidonda vya tumbo na mengine yanayofana na hayo wanaweza kupata ahuweni au kupona kabisa ikiwa watakula bamia.
Wataalamu hao wanaendelea kuzitaja faida nyingine zinazotokana na ulaji wa bamia ni pamoja na kuboresha uwezo wa macho kuona.
Bamia ni chanzo kizuri cha Vitamin A na beta carotene ambavyo ni virutubisho vinavyosaidia kuboresha uwezo wa kuona.
Bamia inasaidia kuweka kawaida kiwango cha sukari mwilini na nyuzinyuzi zake zinasaidia kurahisisha ufyonzwaji wa sukari mwilini.
Pia hudhibiti pia kiwango cha lehemu mwilini na hasa pale inapokuwa mtu ametumia vyakula vingi vyenye mafuta.
Husaidia pia kulainisha choo. Vilevile ni mboga ambayo kwa Waafrika huongeza hamu ya kula na hata kurahisisha kazi ya kumeza.
Wataalamu wanaeleza kuwa ina virutubisho vinavyoweza kupambana na bakteria wanaoshambulia utumbo na kusababisha vidonda vya tumbo.
Pamoja na haya yote bamia huimarisha mifupa, huongeza kinga dhidi ya magonjwa ya figo, saratani pamoja na pumu.

Faida nyingine ya kutumia Bamia hii hapa 
Chimbuko la Bamia ni Abyssinia (Ethiopia) Kisha ikaenea Duniani kote.

1. Michirizi na utonvu unaopatikana katika Bamia, husaidia kusawazisha Kisukari kwa kuzuia kiwango cha Sukari inayotumika katika mwili kutoka kwenye utumbo mkubwa.

2. Utelezi wa bamia huchuja uchafu unaoingia katika Kolestorali (cholesterol) na asidi ya Nyongo unaoingia kutoka kwenye Ini ambao usipo dhibitiwa huenda ikasababisha matatizo ya ki-afya.

3. Bamia husaidia kulainisha Utumbo mkubwa (large intestines) kutokana na kazi yake ya kulainisha choo.

4. Bamia hutumika kwa kutibu vidonda vya Tumbo inasaidia kusawazisha Asidi.
Magonjwa Maalum


Asidi ya Kujirudia rudia na Kufunga Choo

Tafuna vipande sita vya Bamia bila kutumia dawa nyigine kilasiku na Asidi ya Kujirudia rudia na kufunga choo kutakwisha, inashusha Sukari kutoka 135 hadi 98

Pumu
Bamia ina Vitamin C ambayo inawafana watoto wanaougua ugonjwa wa pumu kupumua vizuri wanapoitumia. Nusu kikombe ya Bamia iliyopikwa huwa na miligramu 13 ya vitamin C.

Kidonda Ndugu (Cancer)
Bamia husaidia kuweka Utumbo kuwa na hali nzuri hivyo kupunguza uwezakano wakuugua ugonjwa huu wa Kansa hasa kwenye utumbo mkubwa.

Mishipa midogo ya Damu Kula Bamia kwa wingi kunasaidia kuimarisha Mishipa midogo ya Damu.


Cataracts
Nusu kikombe cha Bamia iliyopikwa inakua na kiwango cha 460 IU ya vitamin A.ambayo inapunguza uwezakano wa kupata ugonjwa wa mtoto wa jicho (cataracts).

Usongo (Depression) na Kukosa Nguvu. Bamia ni mboga bora zaidi kwa wale wanaojisikia dhaifu, Kuchoka na wanao athirika na Usongo (depression).

Related Posts:

  • CHOROKO HUIMARISHA AFYA YAKO Je wewe ni miongoni mwa wapenzi wa choroko? Kama unatumia utakuwa miongoni mwa wanaofaidika na virutubisho muhimu kwa afya mwilini. Wataalamu waliofanya uchunguzi kuhusu choroko ambayo ni jamii ya kunde, wanasema utam… Read More
  • VIUNGO NA MATUMIZI YAKE KWA KILA SIKU KWA AFYA YAKO. Viungo ni kitu muhimu kwenye chakula na huleta ladha ya kufanya  chakula kiwe na hamu zaidi ya kuliwa. Lakini viungo ni si tu huleta  ladha katika chakula lakini pia ni muhimu kwa afya. Leo tuangalie baadhi y… Read More
  • VIUNGO NA MATUMIZI YAKE KWA KILA SIKU KWA AFYA YAKO PART 2 Leo nimeona tuangalie baadhi ya viungo, matumizi yake na faida zake kwa afya zetu. Viungo vimekua vikitumika sana kuleta ladha katika chakula au vinywaji mbalimbali,lakini pia huleta afya katika miili yetu.Endelea kusom… Read More
  • UWEZO WA AJABU WA JUISI YA KITUNGUU-2 leo tunaendelea kufafanua faida zake hasa kwa nywele za binadamu. Jambo muhimu la kuzingatia wakati wa usiku ni muda wa kumaliza kula na kunywa juisi hiyo. Hakikisha unakunywa juisi yako angalau masaa mawili baada ya kul… Read More
  • UWEZO WA AJABU WA JUISI YA KITUNGUU Kuna magonjwa mengine yakikupata hujui hata namna ya kujitibu. Lakini kwa kutumia vyakula na matunda unaweza ukashangaa namna ambavyo unaweza kuliondoa tatizo ambalo pengine ulidhani halina tiba. Katika makala haya ya l… Read More

0 comments:

Post a Comment