Friday 25 July 2014

FAIDA LUKUKI ZA FENESI KIAFYA KWA MWILI WA BINADAMU



Wataalamu wa afya wanasema fenesi huongeza ufanisi wa mfumo wa kinga mwilini na kusaidia kuongeza kinga dhidi ya kifua, mafua na kikohozi. Hii ni kwa sababu ya kuwa na vitamini za aina mbalimbali.

Fenesi ni miongoni mwa matunda ya msimu yenye umbo la kipekee na ladha tamu ya aina yake. Tunda hili linatajwa kuwa na faida lukuki kiafya kwa mwili wa mwanadamu. Kula gramu 100 tu ya fenesi huweza kuupatia mwili nguvu ya kalori 95. 
  • Tunda hili lina nyama laini iliyojaa sukari aina ya fructose na sacrose inayoweza kuupatia mwili nguvu na kuuhuisha kwa haraka.
  • Fenesi limejaa ufumweli au fibre, sifa inayosaidia kulainisha choo.
  • Tunda hili lina virutubisho kadha wa kadha vyenye faida kubwa mwilini. Baadhi ya virutubisho hivyo ni vitamini A, C, B complex, vitamin B6, folic acid, niacin, riboflavin na madini za aina mbalimbali kama vile potassium, magenesium, manganese na chuma. Katika tunda la fenesi kuna protini, mafuta, wanga na antioxidants. Fenesi pia linatajwa kuwa chanzo kizuri cha nishati kisichokuwa na mafuta. Si hayo tu, bali pia kwa kuwa na virutubisho vyenye uwezo wa kuondosha sumu mwilini.
  • Ttunda hilo linaweza kuukinga mwili dhidi ya saratani na magonjwa mengine
  • Pia kuongeza uwezo wa kuona.
  • Kiasi kikubwa cha madini ya potassium kinachopatikana katika fenesi hulifanya tunda hili liwe na uwezo pia wa kuimarisha mifupa na afya ya ngozi.

Wataalamu wa afya wanasema fenesi huongeza ufanisi wa mfumo wa kinga mwilini na kusaidia kuongeza kinga dhidi ya kifua, mafua na kikohozi. Hii ni kwa sababu ya kuwa na vitamini za aina mbalimbali. Faida nyingine ni kurekebisha msukumo wa damu na pia husaidia kurahisisha mmeng'enyo wa chakula tumboni pamoja na kuukinga mwili dhidi ya magonjwa ya moyo na kupooza. Sio vibaya kuelewa kuwa inasadikika kwamba tunda hili lina uwezo wa kuukinga mwili dhidi ya ugonjwa wa pumu na kupunguza makali ya ugonjwa huo. Si hivyo tu, bali fenesi lina vitamini muhimu zinazohitajika kwa ajili ya utengenezaji wa damu mwilini

0 comments:

Post a Comment