Sunday 11 May 2014

KUHARIBIKA KWA CHUJIO ZA FIGO ( ACUTE BLOMERULONEPHRITIS)



Kuharibika kwa chujio amaGlomerulonephritis ni aina ya ugonjwa wa figo unaoathiri sehemu maalum ya figo (chujio) inayohusika na uchujaji wa maji pamoja na uchafu kutoka katika damu. Sehemu hii huitwaglomelurus au chujio kama tutakavyokuwa tukitumia katika mada hii.
Visababishi
Mara nyingi chanzo halisi cha kuharibika kwa chujio za figo(glomerulonephritis) huwa hakijulikani. Hata hivyo wakati mwingine uharibifu huu unaweza kusababishwa na kushambuliwa na mfumo wa kinga ya mwili. Uharibifu katika chujio husababisha damu pamoja na protini kuingia katika mkojo.
Tatizo hili hukua kwa haraka na figo linaweza kupoteza uwezo wake wa kuchuja maji na uchafu kwa kasi ndani ya muda mfupi wa kati wiki chache mpaka miezi kadhaa. Aina hii ya kuharibika kwa chujio za figo kwa haraka hujulikana kitalaamu kama rapidly progressive glomerulonephritis.
Ukubwa wa tatizo na vihatarishi vyake
Takribani robo ya watu wanaopatwa na tatizo sugu la glomerulonephritishuwa hawana historia ya kuwa na ugonjwa wowote wa figo hapo kabla.
Kuna mambo kadhaa yanayoweza kumfanya mtu awe katika hatari ya kupataglomerulonephritis. Mambo hayo ni pamoja na:
  • Matatizo katika mfumo wake wa damu au lymph
  • Kuwahi kutumia vimiminika vilivyotengenezwa kwa kemikali zahydrocarbon
  • Wenye historia ya saratani
  • Maambukizi ya bakteria aina ya streptococcus, virusi, majipu au maambukizi katika moyo
  • Mambo mengine yanayoweza kuongeza hatari ya kupatwa naglomerulonephritis ni pamoja na:
  • Magonjwa ya mishipa ya damu kama vile vasculitis au polyarteritis
  • Matumizi yaliyopitiliza ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non steroidal anti-inflammatory drugs kama vile aspirin
  • Magonjwa ya mfumo wa kinga ya mwili kama vile Anti-glomerular basement membrane antibody disease na IgA nephropathy
  • Makovu katika chujio (Focal segmental glomerulosclerosis) au hali ya chujio kuwa na kuta nene kuliko kawaida (Membranoproliferative GN)
  • Magonjwa yanayoathiri viungo mbalimbali vya mwili kama vileHenoch-Schonlein purpura, Goodpasture’s syndrome au Lupus nephritis
  • Ugonjwa wa kimetaboliki wa Amyloidosis
Dalili
Dalili kuu za glomerulonephritis ni kuwa na damu katika mkojo (hali inayoufanya mkojo kuwa na rangi kama nyeusi, kutu au samawati; mkojo kuwa kama wenye povu jingi (kwa sababu ya kuwa na protini nyingi kuliko kawaida) na kuvimba uso, macho, miguu au tumbo (hali inayojulikana kamaedema)
Dalili nyingine ni pamoja na
  • Maumivu ya tumbo
  • Kutapika damu
  • Kuharisha au kupata choo kikubwa chenye kuchanganyika na damu
  • Kukohoa pamoja na kupumua kwa shida
  • Kukojoa kupita kiasi
  • Homa
  • Maumivu ya misuli na viungo, uchovu, maumivu ya mwili mzima pamoja na kukosa hamu ya kula
  • Kutokwa na damu puani
Baada ya muda, figo hushindwa kufanya kazi na mgonjwa huanza kuwa na dalili za mtu mwenye ugonjwa sugu wa figo.

Uchunguzi na vipimo
Kwa kawaida tatizo la uharibifu wa chujio za figo hutokea tatratibu sana hali inayoweza kufanya ugunduzi wake kuchelewa pia. Wengi wa wagonjwa wenye tatizo hili hugunduliwa pale wanapokwenda hospitali kwa ajili ya uchunguzi wa matatizo mengine. Mara nyingi hali hii hujidhihirisha kwa kuwepo na hitilafu katika kipimo cha urinalysis.
Mambo makuu matatu yanaweza kuonesha kuwepo kwa uharibifu katika chujio za figo. Mambo hayo ni upungufu wa damu (anemia), shinikizo la damu kuwa juu na ishara za kupungua kwa utendaji kazi wa figo.
Vipimo vinavyoweza kufanywa hujumuisha vipimo vya mkojo, damu pamoja na picha kama vile Ultrasound, CT au SPECT/CT.
Vipimo vya mkojo kama vile urinalysis husaidia kuonesha:
  • Utendaji kazi wa figo yaani Creatinine clearance pamoja na Urine creatinine
  • Uchunguzi wa mkojo kwa kutumia hadubini
  • Kiasi cha protini katika mkojo
  • Kiasi cha tindikali ya urea katika mkojo
  • Chembe nyekundu za damu (RBC) katika mkojo
  • Specific gravity ya mkojo na kiasi cha chumvi kwenye mkojo (yaaniurine osmolality)
Vipimo vingine ni pamoja na CT scan, ultrasound ya figo, X-ray ya kifua auIntravenous pyelogram (IVP)
Vipimo vya damu husaidia kuonesha:
  • Kiasi cha protini ya albumin katika damu
  • Utendaji kazi figo kuchunguza kiasi cha BUN na creatinine katika damu
  • Viasili vinavyohusika katika mfumo wa kinga ya mwili kama vile Anti-glomerular basement membrane antibody, Anti-neutrophil cytoplasmic antibodies (ANCAs), Anti-nuclear antibodies au Complement levels.
Ili kuthibitisha uwepo wa tatizo hili na aina yake, kipimo cha biopsy (renal biopsy) hutumika.
Matibabu
Matibabu ya glomerulonephritis hutegemea sana na kisababishi cha tatizo hili, aina yake pamoja na ukubwa wa tatizo lenyewe yaani wingi wa dalili pamoja na uzito wake. Dalili ya muhimu sana kuithibiti ni ongezeko la shinikizo la damu ingawa kwa kawaida huwa ni ngumu sana kuthibiti shinikizo la damu kuwa katika kiwango cha kawaida.
Mgonjwa anashauriwa pia kupunguza kiasi cha chumvi katika chakula chake na pia kiasi cha protini na maji anayokunywa ili kusaidia utendaji kazi wa figo.
Dawa zinazoweza kutumika kwa mgonjwa mwenye tatizo hili ni pamoja na:
  • Zile za kushusha na kuthibiti shinikizo la damu hususani za jamii yaAngiotensin-converting enzyme (ACE) inhibitors kama vilecaptoprilLisinopril au Enalapril; na zile za jamii ya Angiotensin receptor blockers kama vile losartan, Valsartan na Irbesartan.
  • Zile za jamii ya Corticosteroids kwa ajili ya kupunguza na kuondoa mcharuko mwili
  • Zile za kupunguza nguvu ya mfumo wa kinga ya mwili
Iwapo dawa za kupunguza nguvu ya kinga ya mwili zimeshindwa kufanya kazi na kuna uthibitisho kuwa glomerulonephritis imesababishwa na mashambulizi ya seli za kinga ya mwili katika figo, mgonjwa anaweza kufanyiwa tiba inayoitwa plasmapheresis. Katika tiba hii, sehemu ya damu yenye seli za kinga ya mwili zijulikanazo kama antibodies huondolewa kwa kubadilishwa na maji maji (plasma) yasiyo na antibodies zozote zile. Kuondoa antibodies husaidia kupunguza mcharuko mwili na uharibifu zaidi katika chujio za figo.
Iwapo figo zitashindwa kufanya kazi kabisa, mgonjwa anaweza kuhitaji kufanyiwa dialysis au kupandikizwa figo mpya.
Matarajio
Kuharibika kwa chujio za figo kunaweza kuwa ni tatizo la muda na lenye kurekebishika au linaweza kudorora na kuwa la kudumu. Kudorora kwa chujio za figo kunaweza kusababisha kupungua kwa utendaji kazi wa figo au ugonjwa sugu wa figo kushindwa kufanya kazi (chronic renal failure), au kufa kabisa kwa figo zote (end-stage renal disease).
Madhara
Pamoja na kusababisha shinikizo la damu kuwa juu, uharibifu katika chujio za figo unaweza pia kusababisha mlinganyo usio sawa wa madini katika damu (electrolytes imbalance) kama vile ongezeko la madini ya potassium(hyperkalemia); maambukizi yanayojirudia katika njia ya mkojo, uwezekano wa kupata maambukizi ya mwili, mrundikano wa maji mwilini hali inayoweza kusababisha moyo kushindwa kufanya kazi (congestive heart failure) au maji kujaa katika mapafu (pulmonary edema); au ugonjwa wa figo ujulikanao kama Nephrotic syndrome (utaelezwa katika makala zijazo).
Kinga
Inawezekana kuzuia uharibifu wa chujio za figo kwa baadhi ya watu ingawa, kwa ujumla ni ngumu kufanya hivyo. Baadhi ya mambo ya kufanya ili kuepuka kupatwa na tatizo hili ni pamoja na kuepuka matumizi ya vimiminika vyenye kemikali za hydrocarbons, matumizi ya madini ya zebaki pamoja na matumizi ya muda mrefu ya dawa za jamii ya nonsteroidal anti-inflammatory drugs (NSAIDs) kama vile Aspirin.

1 comments:

  1. Hello, everyone! I,m here to explore blogs and forum about wonderful and most safe cure for (Herpes Virus).I was positive to the deadly virus called herpes and i lost hope because i was out casted and rejected even by my closet friends.i searched on-line to know and enquirer about cure for Herpes and i read someone testimony on how he was cured from Herpes so i decided to contact the same herbalist because i know that nature has the power to heal everything.i contacted him to know how he can help me and he told me never to worry that he will heal me with the natural herbs from God!after 2 days of contacting him, he told me that the cure has been ready and he sent it to me via DHL and it got to me after 3 days!i used the med as he instructed me (MORNING and EVENING) and i was cured!its really like a dream but i am so happy!thats the reason i decided to also add more comment of Him so that more can be saved just like me!and if you need his help, you can email him on nativehealthclinic@gmail.com, or whatsapp +2348140073965 I,m neme amber and you can get in touch with me via nemeamber@gmail.com..Contact him for help at Herpes virus HIV/AIDS CANCER COPD BRAIN TUMOR All kind of virus and disease

    ReplyDelete