Wednesday 14 May 2014

DAWA YA UGONJWA WA VIDONDA VYA KOO.



Uvimbe kooni husababishwa na mambo mengi 
na mara nyingi huwa haisababishi shida kubwa sana.Ukifungana mapua, makamasi hupitia kooni na hivyo basi kusababisha uvimbe.Baridi kavu inaweza pia kufanya koo likauke na mtu ahisi likiwashawasha.Unaposhikwa na mafua, pia unaweza kusababisha kidonda kooni kinachoweza tu kutibiwa na dawa.

Jinsi ya kutibu vidonda vya kooni:
Sukutua maji ya chumvi yaliyo vuguvugu
Mumunya dawa za koo, usiwape watoto inaweza kumnyonga akimeza kwa bahati mbaya.
Muulize mfamasia wako akuuzie kipulizo (spray) cha kutuliza uchungu kooni.
Ikiwa koo linawasha au limekauka, pumua mvuke wa maji moto itakusaidia.

Muite daktari ikiwa:
Umefura tezi za limfu shingoni.
Una mabakabaka meupe huko nyuma ya koo lako.
Kwa gafla tu unashikwa na kuumwa na koo huku ukiwa na joto jingi.
Koo linavimba na kuuma zaidi ya juma moja.
Ukishindwa kunywa chochote umu hatarini mwa kuishiwa maji mwilini.
Huku mbele kwa shingo lako pia kumevimba pamoja na koo lako
Tiba ya vidonda vya koo
chukua Vitunguu Maji kiasi kumi au vinane, uviponde halafu Uchanganye na maji kiasi kikombe cha chai kimoja Ukoroge viziru Uvichuje halafu Unywe vijiko vitatu kila siku asubuhi, mchana na jioni vijiko vitatukwa muda wa siku 7 utapona inshallah.

5 comments:

  1. Mzizi Mkavu- nahisi ninatatizo kubwa kooni, mwanzoni chakula lilikuwa kinakwama kooni, yaani nikila chakula baada ya kama 5 hours vinatoka vipunje nikivusugua kene kidole vinatoka harufu mbaya sana!
    Hali hiyo imeenda kama 3 years, sasa mwezi uliopita nilishikwa sana kiungulia kila nikila chakula kinakuwa kama kinataka kurudi naanza kubeua beua, hali hiyo imeisha baada ya koo kuanza kupata maumivu makali sana, nikiamka usiku linakuwa kavu sasa naona hali imezidi siwezi kula wala kuweza mate! Could it be kansa ya koo?, naogopa.

    ReplyDelete
  2. Habr mm Nina ttz koon ninahis km kun kitu kimekwama kooni hii ilitokea baad ya kunywa dawa aina ya amoxcillin ndo nkhs kutpk baad ya mda ndo nikw nahs hivi

    ReplyDelete
  3. Mimi nilienda hospital ni kaambiwa nina maambukiz ya bacteria helicobacteria,lakin cha kushangaza nimetoka vijipele kwny koo yani nikiachama mdomo kwa ndani kule mgongoni kuna vipele vidogo vidogo, miguu inakufa ganzi na inauma Na inawaka moto,upande wa moyo kwa juu mpk kwny bega nyuma, kizungu zungu, na masikio yana unguruma,kama nimechoma quinine! Je linaweza kuwa tatizo la ukoo

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nakushauri uende hospital ya ekenywa wako vizuri Sana

      Delete